Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Tatizo mmekuja mjini juzi, hizo ni plan za JK ulizeni muambiwe.
Mipango si matumizi. Hata JKN naye alipanga Makao Makuu yahamishiwe Idodomya, Mzee Mwinyi juzi kathibitisha kwamba wao wote walishindwa ila Chuma ndiye kaweza, tena ndani ya muda mfupi sana.
 
Binafsi nimefurahishwa na kasi ya Rais Dkt. Magufuli. Naamini wapo pia wengi wanaoungana nami katika furaha hii. Rais Magufuli ameanza kwa kasi ambayo kama ataimaintain, Tanzania haimalizi miaka mitano itakuwa tayari ni nchi yenye kipato cha kati.

Hata hivyo wapo baadhi yetu ambao wanakejeli kasi hiyo. Hao kwangu ni watu waliozoea ubwete na bora liende!. Wanamwona Magufuli kuwa ni mtu atakayekuwa kauzibe kwao!

Wapigaji wote, wavivu wote na wazee wa madili wote watamchukia Rais Magufuli ila mi niseme na niwaombe tu kwamba tumpe support huyu jamaa kiukweli atatufikisha mahali fulani!

Tuwafichue wote wanaopanga kumhujumu (najua wanajulikana), tuwakatae kwani hawana nia njema na taifa letu.

Habari zaidi, soma => Mafanikio ya Rais Magufuli 2015 - 2020

=>Toka kwa Wananchi: Kero na Vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa...
Daaah
 
Watanzania ni viumbe wanafiki sana Duniani. Nlijifunza kitu kwa wazungu.

"Mzungu anaweza kusema kabisa Komeo simkubali,simpendi ila jambo hili alilifanya lilikuwa zuri. Lakini bado simpendi"

Sisi Waswahili tukimchukia mtu tunamchukia na kila analolifanya hata kama jema. Tunendeleza mihemko,jazba na chuki binafsi. Hata jamaa akitembea juu ya maji lets say baharini au ziwani tutasema
"jamaa anatumua vumbi sana na kuchafua mazingira"

Mazuri ya Magufuli:
1. Miradi ya madaraja kupunguza msongamano ni miradi mizuri iliyotumika kwa pesa za watanzania. Hata kama kuna waliowaza before lakini kuwaza si kutenda

2. Mradi wa SGR ni mradi superb kwa ajili ya maendeleo ya mikoa husika na Tanzania kwa ujumla. Miaka ya nyuma mradi kama huu ungekwamishwa sana kwa sababu ya wamiliki wa magari ya mizigo kutoupenda kabisa. Aliweza kuchukua hatua.

3. Daraja la Busisi na miradi mingi ya Barabara nchi nzima. Lakini alijitahidi sana kuzuia Ufisadi uliokuwa umeota mizizi awamu zilizopita.

Mabaya ya Magufuli.
1. Aliamini mtu anayempiga au asiyekubaliana naye ni adui yake. Hivyo akasababishwa kuzungwa na wanafiki wengi sana ndani na nje ya chama chake isipokuwa wapinzani wachache.

2. Alikuwa anaamini WAPINZANI WOTE NI WAPIGA DEAL TU kama ambavyo aliona waliokuwa wakipiga deal kupitia siasa awamu zilizopita.

3. Aliamini Wafanyiabiashara wengi walikuwa wapigaji kama ilivyokuwa awamu za awali. Hivyo akagombana nao wengi sana hasa pia waliokuwa kweli wapigaji kama akina Manji Kwa Mujibu wa Chadem List of Shame na Mafisadi Papa.


Ongezeeni MATAGA NA NYUMBU

MIMI MTANZANIA NIMEISHIA HAPO.

Pia nakaribisha mapozi mengi tu kwa wale ambao watu wao watakuwa wameguswa. Hamna cha kunifanya Hili ni Jukwa Huru sijavunja sheria yoyote ile.
 
Labda Mtanzania wewe ndio Mnafiki,ni vizuri kutumia neno ...baadhi ya... .lakini unaposema Watanzania wote hapo inabidi uwombe razi.
 
Na hata kwa Mwenyezi Mungu ,kama unafanya udhalimu basi hata ukifanya mema mangapi ile zambi ya kuzulumu itakuingiza motoni. Ni kweli Magu alikuwa na kautaalamu fulani wa kula na vipofu.

Tatizo ilikuwa hasikiki katika kadhia za wananchi wake kushambuliwa,kupoteza roho kwa kuuliwa na watu wasio julikana, Kijana Magufuli ilikuwa anakaa kimya kama hakujatokea kitu,sa faida ya kuwakalia kimya watu wasio julikana imeonekana.
 
Ngoja niwaibie siri ndugu zangu wana-JF mnaopenda kuja kuwa viongozi wa kisiasa katika siku za usoni.

Nadhani leo sote, tumeona jinsi JPM alivyokuwa anapendwa na watanzania. Sio kupendwa tu bali hata kuaminiwa.

Nadhani kilichomkuta Mbowe leo ni ishara tosha ili ukubalike kwa watanzania njoo kwa sera za Magufuli maana ni kiongozi aliyechaguliwa na Mungu. Sauti ya wengi, no sauti ya Mungu, chaguo la wengi, ni chaguo la Mungu.

Magufuli kafa ila yupo mioyoni mwa wengi.

Nimewaibia siri!

NB: Kasomeni comment kwenye post ya milady Ayo inayosema "Mbowe ataka chanjo iwe lazima" ndio mtajua watu walio nyuma ya JPM ni wengi kuliko inavyoaminishwa hapa JF
 
Kwa sasa tuna ombwe la kiuongozi..Itatuchukua muda sana kurudi kwenye mstari!Mambo ambayo naona tunahitaji kwa sasa ni maamuzi magumu na uharaka wa kutoa hayo maamuzi!Kasi ya mafisadi kurudi imekua juu mno ukiacha wahalifu na vibaraka wa mabeberu au wanaharati hewa.

Vitu kwa sasa vinaenda kimwinyi sana..Kauli nyingi ni "mlifanyie kazi", "serikali tumeliona tunaenda kuliangalia", "nitawaagiza walifuatilie" n.k..Hizi kauli hazina matumaini kabisa zaidi ya siasa!!
 
Kwa sasa tuna ombwe la kiuongozi..Itatuchukua muda sana kurudi kwenye mstari!Mambo ambayo naona tunahitaji kwa sasa ni maamuzi magumu na uharaka wa kutoa hayo maamuzi!Kasi ya mafisadi kurudi imekua juu mno ukiacha wahalifu na vibaraka wa mabeberu au wanaharati hewa...
Kweli mkuu! mama anafanya kazi akisikia kelele lakini ubunifu na kuweka mifumo ridhishi kwa wananchi imekuwa ngumu kwake! Uongozi kama unavyosema umekuwa wa kuagiza na tutaangalia tufanyeje !
 
Ngoja niwaibie siri ndugu zangu wana-JF mnaopenda kuja kuwa viongozi wa kisiasa katika siku za usoni.

Nadhani leo sote, tumeona jinsi JPM alivyokuwa anapendwa na watanzania. Sio kupendwa tu bali hata kuaminiwa...
Yaani bado upo kwenye ndoto za alinacha hadi leo?

Watanzania walishatoka huko mara tu baada ya kufanya maziko na hadi sasa wanao kumbuka chato ni watoto na wajane tu
 
Kweli mkuu! mama anafanya kazi akisikia kelele lakini ubunifu na kuweka mifumo ridhishi kwa wananchi imekuwa ngumu kwake! Uongozi kama unavyosema umekuwa wa kuagiza na tutaangalia tufanyeje !
Wewe ni mnyarwanda au mushuti habari za watanzania zinakuhusu nini? Ndugu yako alisha kufa hi vyo huna budi urudi kwenu gisenyi
 
Kwa sasa tuna ombwe la kiuongozi..Itatuchukua muda sana kurudi kwenye mstari!Mambo ambayo naona tunahitaji kwa sasa ni maamuzi magumu na uharaka wa kutoa hayo maamuzi!Kasi ya mafisadi kurudi imekua juu mno ukiacha wahalifu na vibaraka wa mabeberu au wanaharati hewa.

Vitu kwa sasa vinaenda kimwinyi sana..Kauli nyingi ni "mlifanyie kazi", "serikali tumeliona tunaenda kuliangalia", "nitawaagiza walifuatilie" n.k..Hizi kauli hazina matumaini kabisa zaidi ya siasa!!
Pumba tupu kutoka kwenye akili pumba
 
Back
Top Bottom