Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Ukweli usemwe magufuli kwenye miundo mbinu aisee shkamoo kweli hakuna Alie mkamilifu ungefanya hivi kwenye demokrasia ungekuwa the best president ever. Kama binadamu tuna udhaifu wetu ila kwenye miundo mbinu aisee shkamoo mzee baba.
 
Salam wakuu,

To cut the story short, mheshimiwa JPM kiukweli anajitahidi sana kuleta maendeleo katika nchi yetu. There reaches a time inabidi kuweka Mambo ya kisiasa kando na kumuunga mkono Mh. Kiongozi wa watu katika harakati za kuendeleza maendeleo ya nchi yetu tusogee zaidi kuliko hapa tulipofikia.

Jana niliweza kupita pale shule ya mfano (Dodoma), aisee kama hii shule ikikamilika na kila mkoa na wilaya ikajengwa shule Kama hii basi tutakua tumepiga hatua kubwa Sana. Wapo watakaobeza kwamba shule sio majengo na kusahau kwamba huko dar itabidi wanafunzi wanaoingia kidato Cha kwanza wasome kwa shift ( can you imagine?).

Zikijengwa shule Bora Kama hii ya mfano ambayo unaambiwa kwamba itakua kuanzia darasa la kwanza hadi form six, kutasaidia kutoa ajira kwa walimu wazalendo na kuleta hamasa kwa wazazi kua shule bora sio za private tu, hata za serikali zinaweza kua Bora.

Mungu ibariki Africa, Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Magufuli
 
Najiuliza tu, hivi Mr Mzungu angeweza kweli!??? Maana ni wazi na dhahiri shahiri kwamba anapapia mambo mawili: Kimalkia na matusi. No more, no less.

NB: ^Nikishindwa uchaguzi huu, nawaingiza wananchi barabarani!^
 
Habari wadau..!
Hii ni kauli ya JPM leo kwenye utiaji saini kati ya serikali na kampuni ya LZ Nickel ya Uingereza.

Ss kazi imeanza vijana watarajie zile ajira 8Mil kupatikana soon ,ila sitoshangaa baadhi ya watu wasio penda maendeleo ya nchi yetu na wasio na uzalendo kuanza kutaka kuturudisha nyuma .

Hii Kabanga Nickel Deposit wale wataaram wa uchimbaji na jeolojia wameisikia sana historia yake na kwa wengi ilikuwa kama ndoto lakini ss JPM amegeuza ndoto hiyo kuwa kweli.

Najua hapa wataaaramu wa Geology,Mining,Mineral Processing,Chemistry ,ME,CE n.k wanafurahia tu kuona fursa nyingine ,uzuri wake kampuni ni ya mwingereza mzungu ambaye hanaga longolongo kabisa.
 
Nimekaa na kutafakari kwanini kipindi cha miaka 6 ya utawala wa JPM miradi mingi imeanzishwa na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa je ni mabadiliko makubwa za kiuchumi anayoyaleta Mheshimiwa Rais Magufuli toka tupate uhuru ?

Pamoja na hali ya biashara kuwa ngumu kipindi hiki cha Covd19 lakini ukusanyaji wa kodi umekuwa mkubwa kupita wakati wowote na leo watanzania kwa mara ya kwanza tunashuhudia madini yakichukua nafasi ya kuongoza katika kuingiza pato la taifa. JPM ataingia katika kumbukumbu ya kuwa muasisi wa Tanzania yenye uchumi Imara.
 
Ukweli usemwe magufuli kwenye miundo mbinu aisee shkamoo kweli hakuna Alie mkamilifu ungefanya hivi kwenye demokrasia ungekuwa the best president ever. Kama binadamu tuna udhaifu wetu ila kwenye miundo mbinu aisee shkamoo mzee baba.
Demokrasia ni muhimu kiuchumi kuliko miundombinu uchwara
 
Back
Top Bottom