Amos Chunji
Member
- Jul 15, 2019
- 22
- 8
Ajira ,bado ni tatizo kubwa
Tusipende kuishi kwa ushabiki kwan maendeleo upimwa kwa namna mtu anavyo ishi na sio namna serikali inavyo ona
Oja yako namba moja ina mashiko ila sio elimu bora n elimu ilimrad watoto waende shule
2-ukiwa wasema kitu sema kwa fact 1.5T zipo wap police walio kamatwa na kuachiwa kuhusu dhahabu ule sio ofisad?
3-mauaji ya kibiti ujawai sikia na kuhusu watu kutekwa na kusemekana wanajiteka ni sahihi unabid utambue wewe mwenyewe ulivyo apo n rasili mali unabd kuwaza iliwa kwako je itakuaje?
5- ningependa kutambua umesha fanya safari kwa kutumia izo ndege kwa mara ngap? Ndege inafanya kazi n moja tu ndio iyo itoke dar ipite KIA iende entebe irud chukua watu kia irud dar na hapo watu walikata tiket ya mchana wanakuja chukuliwa saa mbili usiku na sio mara moja n mara kibao wengne ilisha tugarmu mpaka kukata tiket zingne zaid ya mara tatu,ndege mnasafiri watu kum apo unazani faida ipo wap?
6- sawah uchumi wa maneno ila sio uchumi wenye pumzi tunao uona kila siku dollar inapanda yuan inapanda leo ihii tuan ipo 347 kutoka 330 enzi ya mzee wetu kikwete uchumi umepanda kwenye midomo ya vibaraka au kwenye nn?
8-ameweka jiwe la msingi na sio kujenga hamna mradi mkubwa ata mmoja unaoweza kamilika ndan ya muda mchache iyo treni ataendesha kwa kitu gan umeme wetu binafsi majumban unakatika iyo tren itaendeshwa kwa kitu gan? Tusipende kushadadia ila tuwaze kwa mapana sana
9- mapato ya kuumiza watu n sawa na watu awawez kutumia ela kama mwanzo sababu wanajua kuzipata n shida ila ukiangalia watu wake wote wakarbu wanavyo zitumia hapo bado ufisad upo
10 ni plan ila bado aijatekelezwa na kuwa na plan n jambo jema utekelezaji je?
11 nimekuja tambua kuwa ujawai zunguka na kuona unacho kisema izo sio flyover ila ni kama madaraja tu ya kawaida sana zunguka nchi za wenzetu utaona maana ya flyover na sio ivyo vidaraja vya juu
12- madawa ya kulevya yako pale pale semawanafanya watu wa juu sio kila mtu anafanya saiv
13- aina ukwel wowote dawah hospital azipo juzi tu hapo tuna ambiwa tukanunue madumu ya drip nje hosp yameisha ndio kaborasha nn embu tuanze ulimbuken
14 hapa ni uongo mfano mzur n uhuru wa kujieleza n nan anaeweza mkosoa adharan akabaki salama au ulivyokuwa wa andika ihii point ukuwaza
15 mshikamano gan wakat wawekezaj kila leo wanaondoka kila leo kuja jipya kuhusu nchi yetu na mataifa mengne kama ndege tu kuanza safari ya south na kutoshusha watu hapo uhusiano gan mzuri upo labda wa East African ndio useme ivyo ila sio mataifa mengne
Mkuu are you serious ???Uwanja wa ndege upanuzi umeanza siku nyingi ni ufunguzi tu, fly over zimejengwa wakati wa Kikwete ni umaliziaji na pesa za world bank, daraja la salenda linajengwa kwa msaada wa korea walisema haya kuanzia wakati wa kikwete. Ndege ndiye kanunua yeye barabara ya Dar Moro ilianza zamani lakini wamesimamisha. Treni ilianza zamani wakaiharakisha lakini mradi ulikiwepo. Mradi wa umeme umeanza lakini ndiyo umeanza tu...... naona mna kuza mambo kuliko yalivyo hiyo miradi haijakamilika na mingi sio yake. Shule bure ndiyo mradi wake pekee na mabweni yaani raisi kujenga mabweni yawe agenda wakati wenzake waligenga chuo cha Dodoma kizima na plan zote wanafunzi 40,000 wenzake waliweka pipeline ya gas,
Mkuu are you serious ???
Hauko serious kabbisa.
Vipi kuhusu Ubungo interchange??
Ile fly over ya mfugale ni awamu ya tano.
Mradi wa daraja la kigamboni na muhimbili cardiac institute ndio awamu ya kikwete.
Mkuu are you serious ???
Hauko serious kabbisa.
Vipi kuhusu Ubungo interchange??
Ile fly over ya mfugale ni awamu ya tano.
Mradi wa daraja la kigamboni na muhimbili cardiac institute ndio awamu ya kikwete.
Waambie wasio nazo.Fanyeni shughuli vijana badala ya kushinda mitandaoni tu wakati hamna kitu mifukoni nchi ni maendeleo ya vijana msisubiri serikali pekee na ushabiki kwenye kila kitu kidogo kinachojegwa ni mambo ya kawaida
Ukitaka kujua nchi imetulia kwa sasa baada ya rais Magufuli kuingia madarakani 2015, tofauti na kikundi cha watu wachache ambao mirija yao imezibwa ,wakitumia kichaka cha kujiteka na kiupakazia serikali.
Hata hivyo drama hii imeshindwa ku-hit kama kigenge hiki kilivyotarajia.
Yafuatayo ni matukio sugu hayapo kwa sasa na ni kiashiria tosha kwamba nchi inaendeshwa kwa ustadi na umakini
1-Hakuna migomo ya wafanyakazi na maandamano ya mara kwa mara ,wafanyakazi wako bize kutoa huduma kwa jamii
2-Hakuna migomo na maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu mara kwa mara kama ilivyokua awali.mikopo inatoka kwa wakati na hakuna upendeleo
3-vurugu za maandamano na uporaji wa vyama vya upinzani ulioshamiri kila uchao ,yamekoma
4-ujambazi rate inmeshuka sana
5-utapeli na udhulumati wa wazi rate imeshuka .
Mengine ongeza na wewe
Habari wanabodi,
Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wote wanabodi.
Ni kwamba kumekuwa na tuhuma nyingi sana za ajabu na kijinga ambazo hazina hata miguu ya kusimamia kwamba Mr. President ameshindwa kuiongoza nchi na kusababisha mpasuko katika chama cha CCM.
Hakika uamini usiamini hizo tuhuma zimekuwa zikitolewa na wanachama ambao ni wapigaji ambao ile mizizi yao ya upigaji imekatwakatwa na kutupwa baharini. Hivyo basi, kwa sababu ya kuzibwa ile mianya ambayo waliitumia kuwaibia wananchi wake leo hii wameamua kuja na tuhuma ambazo hazina mashikohata kidoo ili waonekane wao ni bora sana kuliko Mr. President.
Mr. President ukimuondoa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere hakuna Rais mwingine aliyeweza kutokea mwenye uwezo mkubwa na akili kubwa kama wewe. Mbali na uwezo wako mkubwa, wewe ni Rais mbunifu sana tumeshuhudia ubunifu wa hapa na pale mfano ni pale ambapo ulipoanzisha akaunti ya pamoja y kukusanya mapato ya taifa. Huu ubunifu umeweza kuzuia upigaji wa fedha za umma kwa asilimia 85/%.
Kadhalika, Mr. President, wewe ni mfano mkubwa wa kuigwa ulipoanzisha mapambano dhidi ya wahujumu uchumi wala rushwa kitu ambacho hakuna Rais yoyote aliwahi kufanya hiki kitu bali kuna ambao walibariki hayo mambo kama yalivyotajwa hapo juu.
Pia, tumeshuhudia miradi mikubwa sana kujengwa katika taifa letu kwa muda mchache sana tena kwa fedha za watanzania ambazo zinatokana ukusanyaji wa kodi. kiukweli hili jambo linathibitisha uwezo wako mkubwa katika utawala. Tangu nchi hii ipate uhuru hapjawahi kutokea miradi mikubwa ya namna hii.
Aidha, kwa muda mchache uliweza kununua ndege kitu ambacho pia kimesababisha uonekane shujaa katika taifa na kimataifa kwa ujumla.
Mr. President umeweza kuondoa akili mgando kwa baadhi ya watanzania kwamba Maisha mazuri ni lazima upate ajira. Umeweza kuwaonesha kwamba Maisha siyo kuajiriwa serikalini tu bali hata kujiajiri ni jambo la msingi sana.Hii ni jambo la kishujaa sana kwani leo hii vijana wako wanapambana sana na kufanya kazi kwa bidi ili waweze kujiajiri wenyewe. Indeed, unastahili pongezi sana.
Mr.president huwa unaenda mbali sana kwa kuwaadhibu viongozi wazembe na wasiojitambua na ambao wanashindwa kwendana na falsa yako ya Hapa kazi. kwa hili hakuna pingamizi kwani watanzania tumeshuhudia ukiwaadhibu hao viongozi kwa sababu ya uzembe wao na kukosa uzalendo kwa taifa. Mr. President hongera sana kwa kunapenda sana viongozi wanaojibika wenye kujituma na wabunifu.
Mr. President unastahili pongezi kwa kuhakikisha watoto wa watanzania wanapata elimu bure.Ingawa kuna changamoto yingi sana katika hili jambo, umejitahidi sana kwa hili na hizi changamoto zitaisha tu kwani hakuna changamoto ambayo inaweza kuwa ya milele bali changamoto hutokea tu kwa kipindi kifupi. Pia kumbuka hakuna jambo lisilokuwa na changamoto.
Mr. President ninakuomba ukiwa kama baba wa cha cha CCM hakikisha wanachama wenye nia mbaya na chama chako na kwa taifa kwa ujumla. Wanachama wako wengi wao walizoea vya kunyongwa leo hii wanapata shida sana kula vilivyochinjwa. Walipenda sana mtelezo bila kufanya kazi. Leo hii wanataka kutuaminisha kwaamba wao ni wasafi kuliko wewe. Kitu ambacho ni uongo mtupu.
Tumekuwa tukiwashuhudia wakifanya madudu mengi sana na kupelekea wananchi wao kuteseka, watu ambao walikosa huruma na uzalendo kwa wananchi na kwa Taifa leo hii wanataka kutuaminisha kuwa wao ni wasafi. Usafi huo wameutoa wapi? wanachuki binafsi
dhidi ya utendaji kazi wako uliojaa weledi na ubunifu mkubwa sana. Walishindwa nini tangu zamani kuwa wazalendo ila wanataka kutuaminishia leo hii kuwa wanapenda nchi hii?
Mr. President, wewe nimti wa matunda, kumbuka ule usemi kwamba mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe. Huwezi kuona mti ambao hauna matunda ukirushiwa mawe hata siku moja. Mbali na hili, chuki zao binafsi na lawama zao ambazo hazina miguu wala kichwa usikubali vikuyumbishe.
NB. Kila mtu ana mapangufu yake ingawa mazuri aliyoyafanya Mr. President yanafunika/yamefunika mapungufu yake yote katika utendaji kazi wake.
Mr. president hii ni Summary ya mambo makubwa uliyofanya kwa taifa letu.
1. Kujenga miradi mikubwa mfano Stigler's Gorge project, Ujenzi wa barabara ya Agakhan to Masaki, Flyover, Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni.
2. Kuanzisha mahakama maalum za kushughulikia ufisadi na kuwafunga wahujumu uchumi.
3. Kuanzisha akaunti ya taifa ya pamoja kwa ajili yakutunza mapato.
4. Elimu bure kwa Watanzania.
5. Kuhimiza suala la uzalendo nchini.
6. Ununuzi wa Ndege.
7. Kuondoa safari za nje ya nchi ili kupunguza matumizi mabaya ya kodi za wananchi.
8. Ujenzi mkubwa wa uwanja wa ndege.
9. Serikali kuhamia mkoani Dodoma.
10. Dhana ya kujiamini na kuthamini vya kwetu na siyo vya wazungu.
11. Kuhamasisha watanzania kufanya kazi na waache maisha ya uvivu, uzembe na kupenda mtelezo(Falsafa ya hapa kazi tu)
Karibuni Tumpongeze Mr. President kwa mapinduzi na mafanikio makubwa nchini. Ingawa kuna watu wenye chuki zao binafsi watapinga hili suala kwa hoja nyepesi na ambazo hazina kichwa wala miguu.
Mimi Ngajapo kwa akili niliyopewa na mwenyezi mungu na kuongeza kidogo elimu ya dunia (digrii) niliyonayo na akili niliyopata kutokana na mwenendo wa kimaisha. ni vigumu na haitawezekana kuniaminisha kwamba eti viongozi wa CCM waliopita wana ubora au unafuu katika uongozi kuliko Magufuli???? never ever!!!!
Hao viongozi waliopita mnaowasifia eti walikuwa bora kuliko Magufuli labda walikuwa wajomba zenu au mlikuwa mna maslahi nao lkn mimi nakataa hamtaniaminisha hata siku moja ili niwakubalie hoja zenu. Na sitaki niandike mengi lakini kila mmoja anajua udhaifu wao katika kusimamia rasilimali za taifa.
-Hao kila siku walikuwa wanafikiria kugawana rasilimali za nchi
-Nchi ilibaki ukiwa kama vile haina viongozi wa kitaifa.
-Muelekeo wa maisha ulikuwa mbovu, tulikuwa hatujui hatma ya maisha tunakolelekea.
-Viongozi wakati wote ni kufanya sherehe huku umaskini ukitamalaki kwa watanzania ukijaribu kupaza sauti unambiwa una wivu.
-Mjinga ndio anayemuongoza msomi, mfano bunge lijalo kama sio magufuli tungejikuta tunaongozwa na standard seven na wasanii ambao hata kutunga sera za nchi hawewezi zaidi ya porojo na vichekesho bungeni.
mambo ni mengi yalikuwa hovyo mno....acha tu magufuli abadilishe ili tuende sawa.
Waambie wasio nazo.
Maana mm nina maendeleo ya baba na mama wameniandalia.
Bado yangu nayaongezea.
Kwahiyo usione twashinda net ukadhan hoe hae.
Huwez kumkuta msomali Tz anakufa na njaa.
Nimekupata kaka.Tumia muda kujifunza maana madogo wa siku hizi mnaingia kwenye mijadala na kutoa pumba tu
Kaka tafuta Cha kufanya acha kulialia muda unakwenda haurudi pale unapopataka wewe.hakuna mgomo mbaya kama mgomo wa kimyakimya
Muanzisha uzi, kwa kuwa huu uzi umefika page zaidi ya 1,2000, ili anayeufungua leo aweze kupata kuyajua makubwa aliyoyafanya Rais Magufuli ungeyachukua kuyaweka kwenye updates za post yako ya kwanza.
Wanajukwaa poleni na misukosuko ya kujibadili kutoka kuwa walaji wa Mwisho kuelekea nchi ya Viwanda.
Uwanja huu ni maalumu kama ule wa Safari za nje za Jakaya kikwete ila huu ni mahususi kukusanya mambo mazuri ya Awamu ya tano chini ya Rais Magufuli juu ya maendeleo yetu hasahasa kauli yake kuu Juu ya Nchi ya Viwanda na Elimu Bure nk.
Unaruhusiwa kugusia miundo mbinu, Afya, Usafiri, Maendeleo ya Majeshi Yetu, Uvuvi,Michezo, Habari, Siasa, Viwanda,Teknolojia, Pato la Taifa nk.
Ila tu iwe kwa tulipotoka na Alipofanikiwa na nini tufanye kumsaidia kujiongeza zaidi.
Mpaka sasa kafanya haya;
Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 ziko mbioni kuja).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dsm
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.
------------
Na haya ameanza tarehe 12/4/2017;
Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.
Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba
Kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.
Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.
Miradi Mikubwa ya Maji :
Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga
============
emie emie posted: Kwa kweli Rais wetu kafanya makubwa sanaa..
Kila upitapo sasa hivi ni ujenzi unaendelea...Dar es Salaam kila kona Barabara ya Tandale-Sinza- Mawasiliano inajengwa
Madaraja yanajengwa
Upanuzi wa barabara kuu ya Ubungo hadi chalinze unafanywa
Daraja Kilombero miaka yote wapigaji walikuwa wanakula hela za wananchi kuwavusha ila sasa limejengwa
Flyovers zinajengwa
Miradi ya umeme inajengwa na miradi mingi ni kwa hela za watanzania wenyewe
Miaka yote maeneo ya Mbezi na kimara walikuwa hawapati maji japo yanapita njia hiyo hiyo lakini sasa maji yamefika mbezi, na bado wanaendelea kutandaza mabomba ili kupeleka maji. Awali waliokuwa wanakula hela za wananchi ni wenye miradi ya kuuza maji kwa magari. Ila sasa wananchi wamekombolewa.
Utendaji kazi umeimarika, sasa hivi kila mmoja anaona cheo akipewa ni kama kakalia kaa la moto..Yale mambo ya kupiga hela na kukaa ofisini kupiga usingizi yameisha watu ni kazi la sivyo unawajibishwa.
Madawa sasa yanapatikana hospitali, ile hali ya madawa ya hospitali yanapelekwa katika Pharmas binafsi imeisha.
Hospitali sasa za serikali ukienda mgonjwa anajaliwa sio kama ilivyokuwa awali.
Taasisi za serikali wafanyakazi wamekuwa wanawajibika ....hakika nidhamu imeimarika.
Kwa sasa taasisi za serikali zinajiendesha kibiasara bali si kihasara kama ilivyokuwa awali, ilikuwa ni ulaji tuu wa hela, upigaji dili, taasisi zinakufa, hakuna gawio kwa serikali, ila sasa zinatoa gawio...Hakika kila kitu ni usimamizi imara, ukicheka na kima utavuna mabua.
Awali watu walikuwa wanaulilia uongozi, hata wasio kuwa na elimu walikuwa wanagombea kupata uongozi, sasa uongozi umekuwa mgumu sababu kama wewe si muwajibikaji una ndoto za kupiga tuu, hupati nafasi, Uongozi umekuwa una hadhi kwa sasa.
Hakika Namsifu Rais wetu...
Haya usha-post, mrudishie shemeji yako smartphone yake manake watu aina yako hamkawagi kuanza kusoma na messages zake za whatsapp.