Tatizo sio kufanya anayoyafanya, yaani ni kama serikali haijiamini na inakaririsha wananchi tuiamini yenyewe ndio imefanya makubwa zaidi
kwa maelezo yako, hakuna sababu ya JPM kuzunguka 2020 kuomba Kura kwa watu ambao tayari ameshawafahamisha kila siku aliyoyafanya.
 
Cc tz hatuna akil ndio maana tuna aman,wajinga wana cfa ya kutojali ,babu yangu ni mzee lakn ni membe damu
 
Hahaahh kitu cha wali harage........ na chai ya bure huku ukisafisha macho kwa ujenzi wa barabara ya lami
 
10102ac521314716b0cdeb7f1e57ec04.jpg


Wanajukwaa poleni na misukosuko ya kujibadili kutoka kuwa walaji wa Mwisho kuelekea nchi ya Viwanda.

Uwanja huu ni maalumu kama ule wa Safari za nje za Jakaya kikwete ila huu ni mahususi kukusanya mambo mazuri ya Awamu ya tano chini ya Rais Magufuli juu ya maendeleo yetu hasahasa kauli yake kuu Juu ya Nchi ya Viwanda na Elimu Bure nk.

Unaruhusiwa kugusia miundo mbinu, Afya, Usafiri, Maendeleo ya Majeshi Yetu, Uvuvi,Michezo, Habari, Siasa, Viwanda,Teknolojia, Pato la Taifa nk.
Ila tu iwe kwa tulipotoka na Alipofanikiwa na nini tufanye kumsaidia kujiongeza zaidi.

Mpaka sasa kafanya haya;

Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 ziko mbioni kuja).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dsm
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.
------------

Na haya ameanza tarehe 12/4/2017;

Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.
Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba

Kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.

Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.

Miradi Mikubwa ya Maji :

Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga

============
emie emie posted: Kwa kweli Rais wetu kafanya makubwa sanaa..
Kila upitapo sasa hivi ni ujenzi unaendelea...Dar es Salaam kila kona Barabara ya Tandale-Sinza- Mawasiliano inajengwa
Madaraja yanajengwa

Upanuzi wa barabara kuu ya Ubungo hadi chalinze unafanywa

Daraja Kilombero miaka yote wapigaji walikuwa wanakula hela za wananchi kuwavusha ila sasa limejengwa

Flyovers zinajengwa

Miradi ya umeme inajengwa na miradi mingi ni kwa hela za watanzania wenyewe

Miaka yote maeneo ya Mbezi na kimara walikuwa hawapati maji japo yanapita njia hiyo hiyo lakini sasa maji yamefika mbezi, na bado wanaendelea kutandaza mabomba ili kupeleka maji. Awali waliokuwa wanakula hela za wananchi ni wenye miradi ya kuuza maji kwa magari. Ila sasa wananchi wamekombolewa.

Utendaji kazi umeimarika, sasa hivi kila mmoja anaona cheo akipewa ni kama kakalia kaa la moto..Yale mambo ya kupiga hela na kukaa ofisini kupiga usingizi yameisha watu ni kazi la sivyo unawajibishwa.

Madawa sasa yanapatikana hospitali, ile hali ya madawa ya hospitali yanapelekwa katika Pharmas binafsi imeisha.

Hospitali sasa za serikali ukienda mgonjwa anajaliwa sio kama ilivyokuwa awali.

Taasisi za serikali wafanyakazi wamekuwa wanawajibika ....hakika nidhamu imeimarika.
Kwa sasa taasisi za serikali zinajiendesha kibiasara bali si kihasara kama ilivyokuwa awali, ilikuwa ni ulaji tuu wa hela, upigaji dili, taasisi zinakufa, hakuna gawio kwa serikali, ila sasa zinatoa gawio...Hakika kila kitu ni usimamizi imara, ukicheka na kima utavuna mabua.

Awali watu walikuwa wanaulilia uongozi, hata wasio kuwa na elimu walikuwa wanagombea kupata uongozi, sasa uongozi umekuwa mgumu sababu kama wewe si muwajibikaji una ndoto za kupiga tuu, hupati nafasi, Uongozi umekuwa una hadhi kwa sasa.

Hakika Namsifu Rais wetu...
Kasome Article 8 Of The Constitution Of Republic Of Tanzania
 
Sina shaka ya aina yoyote kuwa Rais Magufuli amejitokeza ni Rais mchapa kazi akisimamia kile anachoahidi na kuamini, na anahakikisha kinatekelezwa ipasavyo.
Kauli yake ya hivi karibuni katika ziara yake ya siku tisa mkoani Mbeya inahitimisha ukweli wa hoja yangu hiyo.

Kwenye mji mdogo wa Mbalizi, ambako alisimamishwa na wananchi na kuelezwa kuwa kero ya maji, kukatika umeme na migogoro ya ardhi ni miongoni mwa kero sugu, alisema, nanukuu:

Kwa miaka mingi tangu uhuru wananchi wamekuwa wakisikia maneno ya kisiasa na ahadi, sasa wamechoka.

Ili kusimamia kauli yake hiyo, Rais Magufuli alitoa amri kwa Waziri mhusika akisema, nanukuu:

Waziri (Prof. Mbalawa) ameahidi wiki tatu, lakini mimi ninamwongezea mwezi mmoja ili akamilishe mradi huu na muanze kupata huduma safi ya maji safi ya bomba.

Hakika wananchi tumechoka na maneno ya kisiasa majukwaani na ahadi hewa, tunahitaji viongozi watendaji, ambao watasimamia maneno na ahadi zao zinatekelezwa.

Dar es Salaam, kwa mfano kukatika kwa umeme au maji si jambo geni. Hali kadhalika barabara nyingi zinazokarabatiwa zimebaki na vifusi kwa muda mrefu wala viongozi wa Serikali za Mitaa na Mamlaka husika hawajali adha wanayopata wakazi. Kila mara ni ahadi tu.

Je, Rais Magufuli atembelee kila kona ya nchi na kutoa maagizo ndiyo kero za walipa kodi zisikilizwe na kutatuliwa.

Viongozi wahusika mjitathmini mkitambua kuwa CHEO NI DHAMANA.
 
Sina shaka ya aina yoyote kuwa Rais Magufuli amejitokeza ni Rais mchapa kazi akisimamia kile anachoahidi na kuamini, na anahakikisha kinatekelezwa ipasavyo.
Kauli yake ya hivi karibuni katika ziara yake ya siku tisa mkoani Mbeya inahitimisha ukweli wa hoja yangu hiyo.

Kwenye mji mdogo wa Mbalizi, ambako alisimamishwa na wananchi na kuelezwa kuwa kero ya maji, kukatika umeme na migogoro ya ardhi ni miongoni mwa kero sugu, alisema, nanukuu:

Kwa miaka mingi tangu uhuru wananchi wamekuwa wakisikia maneno ya kisiasa na ahadi, sasa wamechoka.

Ili kusimamia kauli yake hiyo, Rais Magufuli alitoa amri kwa Waziri mhusika akisema, nanukuu:

Waziri (Prof. Mbalawa) ameahidi wiki tatu, lakini mimi ninamwongezea mwezi mmoja ili akamilishe mradi huu na muanze kupata huduma safi ya maji safi ya bomba.

Hakika wananchi tumechoka na maneno ya kisiasa majukwaani na ahadi hewa, tunahitaji viongozi watendaji, ambao watasimamia maneno na ahadi zao zinatekelezwa.

Dar es Salaam, kwa mfano kukatika kwa umeme au maji si jambo geni. Hali kadhalika barabara nyingi zinazokarabatiwa zimebaki na vifusi kwa muda mrefu wala viongozi wa Serikali za Mitaa na Mamlaka husika hawajali adha wanayopata wakazi. Kila mara ni ahadi tu.

Je, Rais Magufuli atembelee kila kona ya nchi na kutoa maagizo ndiyo kero za walipa kodi zisikilizwe na kutatuliwa.

Viongozi wahusika mjitathmini mkitambua kuwa CHEO NI DHAMANA.
Rais anapaswa kuweka misingi au mifumo na siyo kuongoza nchi kwa matamko ya barabarani. Akiondoka madarakani hakika hataacha kitu cha kudumu kwa anaongoza kwa matamko tu. Tunahitaji mifumo ambayo hata aje rais wa namna gani mifumo itamwongoza mfano ni mataifa yaliyoendelea kama USA. Trump hawezi kuiangusha Marekani na ukichaa wake kwani maamuzi ya msingi yanafanywa na wengi na yalishapitishwa na mifumo iliyopo.
 
Back
Top Bottom