View attachment 837432
Kama ambavyo Watanzania tunavyomkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa kusaidia ukombozi wa upatikanaji wa uhuru ama kama ambavyo Hayati Moringe anavyokumbukwa kwa mapambano ya ubadhirifu wa mali za umma, pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anazidi kujenga historia ya kipindi chote isiyofutika kutokana na utendaji, uchapakazi na uzalendo wake kwa Taifa.

Haya hapa ni baadhi ya Mambo ya kihistoria na yenye heshima kubwa kwa Taifa ambayo Rais Dkt. Magufuli aliyoyafanya;-

*(i) Kuhamia Dodoma*
Wazo la Serikali kuhamia kwenye makao makuu ya nchi mkoani Dodoma liliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mwaka 1973 lakini lilishindwa kutekelezwa katika awamu zote. Si awamu ya kwanza, wala ya pili, ama ya Tatu au ya nne bali limeweza kufanikiwa kwenye utawala wa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli. Leo hii karibia Serikali yote imehamia Dodoma. Wizara, taasisi na idara za Serikali, Waziri Mkuu wameshahamia Dodoma. Mwishoni mwa mwaka huu Rais Magufuli naye atahamia Dodoma. Iliasisiwa na Mwalimu Nyerere, ikahaidiwa kwenye ilani ya uchaguzi, imekuja kutekelezwa vyema na Rais Magufuli. Hii ni historia isiyofutika ya uthubutu, uzalendo alionao Rais Magufuli.

*(ii) Ujenzi wa Miundombinu*
Hili halina ubishi kwa asilimia kubwa kabisa miundombinu ya nchi hii imejengwa chini ya usimamizi wa Dkt. Magufuli toka alipokuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Waziri wa Ujenzi na sasa Rais wa nchi. Hauwezi ukazungumzia uwepo wa mitandao ya barabara nchi nzima pasipo kumtaja Rais Magufuli; hauwezi kuzungumzia uwepo wa madaraja makubwa ya kisasa kama ya Daraja la Nyerere, Daraja la Mkapa pasipo kumtambua mchango wa Rais Magufuli. Leo hii nchini tunajivunia uwepo wa flyovers. Rais Magufuli ameonyesha uwezo na heshima kubwa ya ujenzi wa Miundombinu nchini ambayo imekuwa msaada mkubwa wa kimawasiliano, usafirishaji wa Watu na mizigo, kukuza utalii, kuimarisha shughuli za kibiashara na kuongeza mapato ya nchi.

*(iii) Kulifufua Shirika la Ndege*
Tangu mwaka 1977 nchi yetu ilikuwa na shirika la ndege linalosua sua na linalojiendesha kihasara kubwa. Mara baada ya Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli imefanikiwa kununua ndege mpya 7 na mpaka sasa zimeshawasili ndege mpya 4 ikiwamo ndege kubwa aina ya Boeing 787-8. Wale baadhi wanaosema ndege si kipaumbele wala muhimu kwa Watanzania inabidi watambue Leo hii makusanyo ya mapato ndani ya Shirika la ndege (ATCL) yametoka Tsh. Milioni 700 mpaka kufikia Tsh. Bilioni 4.5. Hii ndio faida ambayo Watanzania tumeipata ya kuwa na kiongozi mwenye maono na mtazamo wa mbali zaidi, Rais Magufuli.

*(iv) Ujenzi wa Stiegler’s Gorge*


Utawala wa awamu ya kwanza uliokuwa ukiongozwa na Mwalimu Nyerere ulikuja na wazo wa kujenga Stiegler’s Gorge mnamo mwaka 1981 lakini umeshindwa kufanyika mpaka awamu hii ya 5 inayoongozwa na Rais Magufuli umeamua kufufua na kuliendeleza wazo hili. Mradi wa Stiegler’s Gorge kupitia Mto Rufiji utafanikiwa kuzalisha Megawattz 2100 utakapo kamilika. Ukamilifu wa mradi huu utajenga uhakika wa umeme nchini, utashusha bei ya umeme nchini na pia utamjengea Rais Magufuli heshima kubwa isiyofutika.

*(v) Mapambano dhidi ya Rushwa na ufisadi nchini.*
Rais Magufuli ameingia kwenye historia ya kiongozi ambaye Serikali anayoiongoza kuwa na mapambano ya dhahiri ya rushwa na ufisadi nchini. Tumeshuhudia Mafisadi Papa ambao walikuwa hawashikiki wala kukamatika wakipandishwa Mahakamani. Katika miaka ya nyuma ilikuwa suala gumu sana kwa Watuhumiwa “Mapapa” kuguswa tu, achilia mbali kupandishwa Mahakamani. Haya ni mapambano ya wazi wazi ya Serikali ya Rais Magufuli ya vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini. Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

*(vi) Uwazi wa taarifa na udhibiti wa rasilimali za nchi*
Tumeshuhudia Serikali ikiweka uwazi kwenye mikataba na uchunguzi wa rasilimali za Taifa na kuweka makubaliano mapya yenye tija Mathalani tumeona uwazi wa sekta ya madini ya dhahabu, almas na Tanzanite ambapo Taifa tumeona namna ambavyo tulivyokuwa tukiibiwa na Serikali kuweka mikakati mipya ya kutokuibiwa tena. Kama haitoshi tumeshuhudia wawekezaji wakibanwa vilivyo juu ya mikataba isiyokuwa na tija kwa Taifa. Ni Serikali ya Rais Magufuli iliweka uthubutu wa kuwabana wawekezaji wa madini wa ACACIA iliyozaa matunda kwa Serikali ya Tanzania kumiliki asilimia 16 ya hisa katika makampuni ya uchimbaji wa madini, Serikali kupata gawio la faida ya madini ya asilimia 50 kwa 50. Yote haya yamewezekana kwa sababu ya uzalendo wake Rais Dk. Magufuli

*(vii) Ujenzi wa Bomba la Mafuta*
Serikali ya Rais Magufuli imefanikisha vilivyo kushirikiana na nchi ya Uganda kujenga Bomba la Mafuta linalotoka nchini Uganda mpaka Tanga nchini Tanzania. Ujenzi huo wa bomba la mafuta utazalisha ajira nchini na utaongeza pato la Taifa. Hayo yote yamefanikiwa kutokana na Serikali ya Rais Magufuli kuzidi kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi nyinginezo.
afu ujue unazingua sana we jamaa inama SGR hujaiona ama? mbona unasahau vitu muhimu kama
1.Kufufua TTCL
2.upanuzi wa bandari
3.ujenzi wa meli ziwa nyasa na nyingime ya victoria itasainiwa aiku yoyote kuanzia sasa
4.maendeleo ya mzungumzo ya ujenzi wa bandali ya bagamoyo ambayo yanaenda vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ameondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki lakini ametengeneza watumishi hewa wenye vyeti halali. Alipo teua wagurugenzi zaidi ya 160 wapya huku wale wa zaman wakiendelea kula mshahara ule ule wa ukurugenzi, kwa hyo cheo kimoja analipa mara mbili, hili n kosa na ndio maana anakosa pesa za maendeleo yanayo mgusa mwananchi moja kwa moja.

Tatizo lingine la usiri wa serikali yake juu ya rasilimali za nchi, kuzuia bunge lisirushwe mbashara huu ni usiri na uwoga wa kuogopa kuona serikali yake inakosolewa

Kuingilia mamlaka ya mihimili mingine, kwa mfano kuingilia bunge na kusema bajet hii isipopita atavunja bunge na wabunge wengine hawatorud, huku ni kuingilia muhimili wa bunge katika uhuru wake wa kufanya maamuzi

Kuwa na double standard, huku anatumbua kule anafunikia jipu na kuliacha kana kwamba halioni.

Yako mengi mno ambayo yanafanywa kinyume cha katiba kama kubaka democrasia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
10102ac521314716b0cdeb7f1e57ec04.jpg


Wanajukwaa poleni na misukosuko ya kujibadili kutoka kuwa walaji wa Mwisho kuelekea nchi ya Viwanda.

Uwanja huu ni maalumu kama ule wa Safari za nje za Jakaya kikwete ila huu ni mahususi kukusanya mambo mazuri ya Awamu ya tano chini ya Rais Magufuli juu ya maendeleo yetu hasahasa kauli yake kuu Juu ya Nchi ya Viwanda na Elimu Bure nk.

Unaruhusiwa kugusia miundo mbinu, Afya, Usafiri, Maendeleo ya Majeshi Yetu, Uvuvi,Michezo, Habari, Siasa, Viwanda,Teknolojia, Pato la Taifa nk.
Ila tu iwe kwa tulipotoka na Alipofanikiwa na nini tufanye kumsaidia kujiongeza zaidi.

Mpaka sasa kafanya haya;

Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 ziko mbioni kuja).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dsm
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.
------------

Na haya ameanza tarehe 12/4/2017;

Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.
Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba

Kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.

Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.

Miradi Mikubwa ya Maji :

Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga
Ukiondoa esigiara na stigilas goji ni kitu gani jiwe amefanikisha??jibu tafadhali!
 
Hizo milioni 50 kila kijijini wala siwezi kumkumbusha maana najua hawezi kutoa.
Maendeleo hayaletwi kwa kutumia ubabe,dharau, kiburi, jeuri, nguvu , kwani kazi anafanya peke yake?
Watu kama wewe bila ubabe hakuna lolote. Nchi hii bila ubabe ni kulalamika tu. Mtu mwenyewe hata unaiba hadi sindano !!
 
Yote hayo yamemsaidia vipi mwananchi alieko Tandahimba?
Unaambiwa kuna barabara ya kwenda Tandahimba. Unavyouliza yote hayo yanamsaidia nini mwananchi wa Tandahimba ni upuuzi mtupu. Kitu cho chote kinachofanyika hakiwezi kuwasaidia moja kwa moja Watanzania wote kwa ujumla. Acha utoto. Tumuunge mkono Rais wetu katika jitihada zake za kuendeleza nchi.
 
1)uwezeshaji wa kupotea kwa pesa 1.5trillion bila mtu kuhoji
2)uendelezaji wa kazi nzuri ya kusaidia watu kuhama vyama na kupata tena vyeo walivyokuwa navyo bila mtu kuhoji
3)viwanda 3000+ kuanzishwa na uchumi kupanda kwa kasi nzuri wapinzani na wananchi kumuunga mkono
4)polisi kusimamia haki katika vituo vyetu vya uchaguzi na kulinda amani mitaani
Uwanja wa ndege chato
 
Tatizo kubwa la waafrika tumejenga dhana kwamba raisi na Viongozi wengine tuliowachagua wanatusaidia wananchi, siyo kwamba wanatimiza majukumu yao. Uongozi ni ajira, kwani unalipwa na kodi za wananchi. Yampasa raisi wetu, Viongozi na watanzania watambue kuwa raisi ni mtumishi, siyo mfalme. Kufanya hili au lile ni jukumu lake. Endapo tutalazimishwa kusifu, basi tutambue michango ya watendaji wakuu na wafanyakazi wanaofanya kazi kwa bidii na kuleta maendeleo katika jamii zetu. Tuwe wakweli, sifa siyo za raisi peke yake. Raisi anapaswa kukosolewa zaidi ili ajitume zaidi kwa waajiri wake ambao ni raia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi namshukru kwani Barbara ya mtaani kwangu Bombamzinga -Tabora imewekewa lami kwa Mara ya kwanza endelea hivyo mheshimiwa wananchi Wa mtaani Sana juju bal
 
Hivi jaman tukiachana na masuala ya kujenga jenga pesa si angepeleka na sector nyingine. Ili mzunguko wa pesa uwe mkubwa.

Maana ukifuatilia makampuni mengi ya ujenzi ni ya foreigners so pesa haibaki nchini. Hivyo uchumi kuzidi kudorora zaidi
Hapana na ndiyo! Hapana kwa sababu hii miradi ya ujenziinatoa fursa za kazi au ukipenda ajira; haijalishi ni kwenye ngazi au kiwango gani, lakini wananchi wetu, Watanzania wa kawaida wanapata kazi huko. Kazi hizo zinaweza kuwa zile za moja kwa moja (direct employment) au zile zisizokuwa za moja kwa moja (indirect employment). Nadhani unanielewa, kwa hiyo pesa, hata kama ni chache kiasi gani zitabaki humu nchini! Hicho kiasi kinacho kwenda nje ni kadri ya mikataba ilivyo. Hii ndiyo ninyi mnaita win - win situation! Usitarajie wajenge tu na wao wasipate cha kurudisha kwao; fahamu kwamba haya ni makampuni yana ofisi na staff wengine huko na ni halali wapeleke pesa kwao!
 
Ulietoa mada,unaonekana bado upo karne ya 20 na sio ya 21..Why?
*Nikiangalia,Trump na JPM wameingia madarakani muda sawa....yeye Trump,ameweza kuzalisha kati ya ajira 157,000 kila mwezi,huku kiwango hicho kikitarajiwa kuongezeka hadi 190,000 kwa kila mwezi..kwa takwimu za wachumi na maswala ya jamii.
*Trump ameweza kushusha ukosefu wa ajira kwa 3.9% kutoka 5%,na inaendelea kupungua...UDSM pale wanamaliza watu 5000 na wote HAMNA KAZI,Mitaani vijana hawaelewi cha kuwapa riski ya siku...kuna nchi ambazo hayo ni ‘hadithi za kusadikika’
*Trump hakuishia hapo,ameweza kuongeza ujira kwa lisaa kufikia $27.5 ikiwa ni ongezeko kwa 0.3%,na kufanya 27% kama ongezo la kipato kwa saa.
*Na pia Mfufumuko wa bei na riba vimedhibitiwa kwa 1.75%-2%......Sasa kati ya watu hawa wawili NANI AMEFANIKIWA?
 
Back
Top Bottom