popote ulpo agza chakula ntakuja kulpa umeongea fact saaaaan✌️✌️✌️Hata kama ni kampeni, si vema kumdanga mtu mzima mwenye akili timamu ambaye pia si kipofu. Wafanyabiashara wengine ni sisi na tunaona kodi ilivyobana. Ndugu yangu alifunga duka Kariakoo kwa sababu ya kodi kubwa. Katika familia yetu kuna vijana 4 walimaliza chuo bila ajira hadi sasa. Bei za vitu madukani kwa miaka hii ziko juu kuliko 2015, mfano, sukari. Shuleni hakuna walimu wa kutosha kwa kuwa hakuna walimu walioajiriwa kipindi hiki cha miaka 5. Wana vijiji waliahidiwa mlioni 50 kila kijiji hawakupewa hivyo hawana furaha, komputa mpakato walizoahidiwa? Hawana furaha. Wafanyakazi hawakupandishwa mishahara wala madaraja hivyo hawana furaha. Uchumi wa kati ni suala kisomi ambalo mwananchi wa kawaida halielewi kwa kuwa haliakisi maisha yao moja kwa moja. Uchumi wa kati na maisha magumu.... ! Hata bima yua afya kwa wanayoitumia wamepunguza aina za dawa na baadhi ya huduma zinazolipiwa na bima, zahanati vijijini hakuna dawa za kutosha, na hakuna waganga na wauguzi wa kutosha na kila skta iko hoi.
Watu hawaji kwenye mikutano yenu kwa hiari zao. Shule zinafungwa na wanafunzi wanatakiwa wavae kiraia wahudhurie, ofisi zinafungwa na wafanyakazi wanatakiwa kuhudhuria kwa lazima, malori yanakodiwa kuleta watu kutoka mbali ambapo wale wa mbali sana hupewa elfu 5 ya kula na kadhalika. Magazeti yote, radio zote, tv zote mnatumia ninyi. Hata mango yote ya uraisi ni ninyi tu, hivyo watu hawafuriki kwa sababu ya furaha na kuridhika. Hali ni mbaya ila basi tu!