Maeneo/Miji/Centers zinazokua kibiashara kwa kasi sana hapa Dar es Salaam

LaRosa

JF-Expert Member
Jul 3, 2020
952
2,871
Kwema wajumbe?

Kama kawaida miji ina tabia ya kukua na kufifia, mfano mji wa Bagamoyo na kilwa kwa miaka ya kuanzia 1800 ndio ilikuwa miji Mikubwa kibiashara kwa Africa mashariki na pwani yote ya bahari ya Hindi lakini kutokana na mabadiliko ya maisha leo hii hii miji imebaki magofu na hakuna mfanyabiashara mkubwa mwenye hamu napo

Ilhali center Kama Tegeta zamani ilikuwa mbuga ya ngedere lakini leo hii ndo center inayoingiza mapato mengi zaidi kwa Kodi na mzunguko mkubwa wa kibaishara kuzidi Bagamoyo. Tegeta imekua kwa kasi kubwa mno.

Dhumuni kubwa la Uzi huu Ni kushirikishana sehemu ambapo ukuaji wake wa kiuchumi na kibiashara unakua kwa Kasi ili wanajf tunufuaike napo mapema kabla hapajawa magofu kama Bagamoyo.

Karibuni, tuchangie afu tuone.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom