Maendeleo ya ujenzi wa fly over ya Ubungo

Kwani mpaka world bank wakakubali kufadhili ujenzi wa interchage, unafikiri hawakuyumia numbers? Unafikiri afisa mmoja aliota na kuspecualate halafu fasta wb wakasema pesa hizo

WB ni mtoa mkopo, unavyokopa zaidi ndivyo anavyopata. Wewe ukiomba mkopo milioni mia benk wakauidhinisha ila ulipopiga hesabu ukajikuta unahitaji milioni 75, utachukua mkopo wa milioni mia kwa vile tu benki imeishinisha?

Come up with something imperical.
 
WB ni mtoa mkopo, unavyokopa zaidi ndivyo anavyopata. Wewe ukiomba mkopo milioni mia benk wakauidhinisha ila ulipopiga hesabu ukajikuta unahitaji milioni 75, utachukua mkopo wa milioni mia kwa vile tu benki imeishinisha?

Come up with something imperical.

Inawezekana hauja deal na mabenki ya biashara sembuse world bank. Mkopo unatolewa dhidhi ya mpango (business plan) uliokubaliwa na wenye kueleza namna mradi utavyo zalisha mpaka urudishe mkopo. Pia huwa hela inalipwa kwa wakandarasi kutokana na hatua iliyofikiwa - siyo kwa mkopaji. Na japo wb inatoa concessionary loans, bado wanafuata basic tenets of economic viability ya mradi kabla hawajatoa hela.

Hauwezi uka negotiate mkopo wa kujenga jengo la ghorofa 10, halafu ukaamua ujenga ghorofa 4 halafu benki ichekelee tu. Wb walishakubali mpango wa interchange, kama kweli khna mabadiliko, basi khna sababu kubwa kuliko hii unayosema eti tumegundua flyover inatosha.

Anyway, sina sababu ya kutumia nguvu kubwa sana kukufundisha vitu ambavyo labda hauko tayari kukubali. Let us agree to disagree ☺
 
ndugu huna haja ya kunifundisha, wewe taja namba twende na hesabu. Hii ndio sababu kubwa wana miradi tunaamua kwenda agile. Nawe na wenzio vile hampendi kujifunza na kubadilika basi mnakariri na kwenda as a waterfall.

Hivyo basi, kama kujenga flyover kunakidhi malengo haina haja ya kujenga interchange. Kuna vipaumbele vingi na muhimu vinavyohitaji funding kama upatikanaji maji safi na salama maeneo mengi ya nchi, etc kuliko kung'ang'ania interchange hapa Dar.

Kama una personal interest njooni na namba tujadili.
 
Kwa aliyekusoma vizuri kwenye hili bandiko, umeuliza pasipo NIA NJEMA. Essentially kwa akili yako unataka mradi ufail iwe aibu kwa Maghufuli na CCM yake. Unachoshindwa kujua ni kwamba Tanzania is bigger than JPM na wanasiasa. Tanzania ilikuwepo na itaendelea kuwepo. Kwa hiyo wote tuna maslahi kuona miradi yote inafanikiwa kwa faida ya vizazi vya leo na kesho.

Ukitaka kila kitu kinachofanywa na Magufuli kukiangalia kwa mrengo wa siasa utakuwa disappointed big time!
Akili zako kweli bashite,sasa watu wasihoji??
 
Back
Top Bottom