abduel paul
Senior Member
- Nov 23, 2010
- 133
- 5
Wazee wetu wana kila sababu ya kusherehekea maendelea ya tangu kupatikana kwa uhuru yani miaka 50 iliyopita, mfano ongezeko la miundo mbinu, nyenzo, mawasiliano, nk, lakini Tanzania inapaswa kutambua kizazi cha umri wa miaka 30, ambacho kimekua pakiwepo na utandawazi, kasi ya maendeleo inaweza kulinganishwa kila dakika, na uelewa ambao kizazi hiki unao, katu hawawezi kukubali kama kuna hatua za maendeleo zinazo lingana na muda ulio tumika, kijana wa miaka 30 mpaka 18 hawezi katu kushangilia maendeleo ya upungufu wa uzalishaji, ongezeko la miundo mbinu ikiwa kuna sehemu bado hazifikiki, uwekezaji wa wa wageni unao leta hasara kubwa kwa wananchi na faida ndogo kwa serikali, ongezeko la ukosefu wa ajira,kuporomoka kwa thamani ya Shs na ugumu wa maisha,nafasi ya wasomi kupuuzwa, nk.