Maendeleo tangu uhuru yapo, lkn je maendeleo baada ya miaka 20 tangu uhuru ni sawa?

abduel paul

Senior Member
Nov 23, 2010
133
5
Wazee wetu wana kila sababu ya kusherehekea maendelea ya tangu kupatikana kwa uhuru yani miaka 50 iliyopita, mfano ongezeko la miundo mbinu, nyenzo, mawasiliano, nk, lakini Tanzania inapaswa kutambua kizazi cha umri wa miaka 30, ambacho kimekua pakiwepo na utandawazi, kasi ya maendeleo inaweza kulinganishwa kila dakika, na uelewa ambao kizazi hiki unao, katu hawawezi kukubali kama kuna hatua za maendeleo zinazo lingana na muda ulio tumika, kijana wa miaka 30 mpaka 18 hawezi katu kushangilia maendeleo ya upungufu wa uzalishaji, ongezeko la miundo mbinu ikiwa kuna sehemu bado hazifikiki, uwekezaji wa wa wageni unao leta hasara kubwa kwa wananchi na faida ndogo kwa serikali, ongezeko la ukosefu wa ajira,kuporomoka kwa thamani ya Shs na ugumu wa maisha,nafasi ya wasomi kupuuzwa, nk.
 
Je! Vijana washangilie? Kwa maana nyingine maendeleo ya miaka 50, ni yale tu yaliyojengwa na Hayati Baba wa Taifa, toka pale, haya yanayoitwa maendeleo hata kama Watanzania wote tungeondoka Tanzania kwa miaka 30, tungerudi tukakuta yamesogea, tena pasipo hata uharibu ambao umefanyika sasa,
 
Baada ya uhuru we earned a reputed identity throughout the world because of what we chose to be and follow. Unfortunately, Leo hii hatuna tena identity in the international platform. Tumekuwa watoto tusio na baba. Tunachezeshwa mziki wa aina yoyote and willingly we dance to the tune of our new masters. Maendeleo tutayapataje sasa? Imagine a person with no identity anakuwaje kuwaje!
 
Umesahau kuwa kuna kitu kinaitwa "NWO"

dunia ilikuwa mahala salama pa kuishi, wajinga wahuni wachache wakajifanya kutaka sifa kuipiga marekani.

mtaisoma sana na bado.

mtaletewa sana vyandarua in exchange of minerals and other natural resources.

mpaka marekani wa-break even.
 
Tupate wapi watafiti watao leta matokea ya uchunguzi wa uharibifu katika yale tunayoita mapambano ya kimaendeleo, maana kwetu tafsiri ya maendeleo ni... Mtu Kuuza miguu au macho kwa wazungu, alafu pesa tununue suti walau tukisimama nao tulingane kimavazi,heti tumependeza hali tuvilema.
 
SI kwamba maendeleo hayapo; lakini si ya kujivunia kwa sababu hayalingani na umri wa nchi; na kibaya zaidi hayalingani na mabaya tuliyotendewa na watawala wetu kwa kipindi hiki cha mwishoni. Binafsi naweza kusema kuwa kulikuwa na unafuu kipindi cha Mwl. Nyelele ambaye aliiacha shilingi 500/= ikiwa sana na dola 1; alipokuja Mwinyi aliiporomosha hadi kufika kwenye dola 1 sawa na Tshs. 1100/=; Benjamini akairudishia thamani hadi kufikia dola 1 sawa na Tshs 850/=; Kiboko huyu wa sana ambaye anajitahidi dola 1 ifikie Tshs. 2000/=
Kwa maelezo hayo mafupi nafikiri tunapiga hatua moja mbele tunarudi hatua tatu nyuma; kuna haja ya kushangilia au ni kukaa kujadili tufanye nini!?
 
Back
Top Bottom