Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,153
Wakuu Kwema?
Wengi wetu tumekua tukimsikia Mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM, Bw. John Joseph Magufuli akizitoa kauli hizi mbili za "Maendeleo Hayana Vyama" na "Mkinichagulia Wapinzani Sintoleta Maendeleo" katika maeneo mbalimbali kwenye Kampeni zake.
Amekua akizitoa aidha kwa wakati mmoja, au kauli mojawapo katika mikutano yake mbalimbali ya kampeni anayofanya. Ingawa kubagua kupeleka maendeleo sehemu zisizo na Mbunge wa CCM ni kuwasaliti hata madiwani wa CCM wa Jimbo hilo husika lakini hapa ninazungumzia maana ya kauli hizi katika lugha ya Kiswahili.
Mimi kwa uelewa wangu, na natumai wengi wetu tunaelewa hivyohivyo ni kua kauli hizi zinakinzana zenyewe. Yaani panapokuwepo na kauli mojawapo katika hizi basi ingine haiwezi kuwepo.
Huwezi ukabagua kupeleka maendeleo sehemu ambazo hawakumchagua mpinzani kisha kauli ya "Maendeleo Hayana Vyama" ikaendelea kua na mantiki. Hizi kauli mbili ni sawa na urushe "Shillingi" kisha matokeo yawe ni both "Head and Tail" kwa wakati mmoja, kitu ambacho ni haiwezekani.
Kwa Magufuli kuendelea kuhubiri kauli hizi ni kuthibitisha aidha ye mwenyewe hajui maana halisi ya kiswahili ya hizi kauli, au anazielewa vyema ila ameamua kutudhihaki Watanzania akijua kama hata kama anaongea vitu visivyoendena lakin mwishowe hatutakua na cha kumfanya.
Inawezekana hata wafuasi wake nao hawaelewi kwanini anaendelea kukosea kuhubiri kaulizi hizi mbili kwa pamoja lakini kwa kumuogopa wanashindwa cha kumfanya.
Wito wangu Kwa Ndugu Mgombea huyu ni achague tu upande mmoja bdio auhubiri huo huo. Yaani awe moto au baridi, lakini sio vuguvugu au kuuma na kupuliza kama anavyofanya, ni hayo tu.
Wengi wetu tumekua tukimsikia Mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM, Bw. John Joseph Magufuli akizitoa kauli hizi mbili za "Maendeleo Hayana Vyama" na "Mkinichagulia Wapinzani Sintoleta Maendeleo" katika maeneo mbalimbali kwenye Kampeni zake.
Amekua akizitoa aidha kwa wakati mmoja, au kauli mojawapo katika mikutano yake mbalimbali ya kampeni anayofanya. Ingawa kubagua kupeleka maendeleo sehemu zisizo na Mbunge wa CCM ni kuwasaliti hata madiwani wa CCM wa Jimbo hilo husika lakini hapa ninazungumzia maana ya kauli hizi katika lugha ya Kiswahili.
Mimi kwa uelewa wangu, na natumai wengi wetu tunaelewa hivyohivyo ni kua kauli hizi zinakinzana zenyewe. Yaani panapokuwepo na kauli mojawapo katika hizi basi ingine haiwezi kuwepo.
Huwezi ukabagua kupeleka maendeleo sehemu ambazo hawakumchagua mpinzani kisha kauli ya "Maendeleo Hayana Vyama" ikaendelea kua na mantiki. Hizi kauli mbili ni sawa na urushe "Shillingi" kisha matokeo yawe ni both "Head and Tail" kwa wakati mmoja, kitu ambacho ni haiwezekani.
Kwa Magufuli kuendelea kuhubiri kauli hizi ni kuthibitisha aidha ye mwenyewe hajui maana halisi ya kiswahili ya hizi kauli, au anazielewa vyema ila ameamua kutudhihaki Watanzania akijua kama hata kama anaongea vitu visivyoendena lakin mwishowe hatutakua na cha kumfanya.
Inawezekana hata wafuasi wake nao hawaelewi kwanini anaendelea kukosea kuhubiri kaulizi hizi mbili kwa pamoja lakini kwa kumuogopa wanashindwa cha kumfanya.
Wito wangu Kwa Ndugu Mgombea huyu ni achague tu upande mmoja bdio auhubiri huo huo. Yaani awe moto au baridi, lakini sio vuguvugu au kuuma na kupuliza kama anavyofanya, ni hayo tu.