Maelfu ya wanachama wa CHADEMA wampokea Dr. Magufuli na kujiunga na CCM

mtemi chenge alikua na kihoma kidogo,hajafika mkutanoni


Mkuu acha kupotosha umma. Tunafuatilia sana siasa za Tanzania. Tupo makini.


Chenge alihudhuria ule mkutano. Tena alimuumbua mkuu wa KAYA kuwa hakutimiza ahadi ya mwaka 2005 na 2010 kuhusu ujenzi wa barabara. Haijajengwa hadi leo. Ndipo Magufuli akasema kuwa "ataijenga yeye Magufuli akipewa nchi"


Soma magazeti ya JANA Jumapili 13/09/2015 utaona jinsi Chenge alivyomuumbua JK na ahadi zake feki.





MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Mimi mwana CCM Kindakindaki naapa kuwa nitampigia kura Edward Ngoyai Lowassa anayeiwakilisha CHADEMA kupitia mwamvuli wa Muungano wa vyama vya UKAWA. Kama kunawakati ambapo CCM inahitaji kujipanga vyema na kurekebisha mapungufu yaliyopo wakati huo ndio sasa.Kwa yeyote anayeipenda CCM kama mimi,naomba kwa Moyo Mkunjufu tuiweke CCM pembeni ili ikajikague,ikajitafakari na kisha ijipange kwa ajili ya 2020 - 2025.Gari ama mashine yeyote ile hata iwe tingatinga ikiharibika sharti iwekwe pembeni ili ifanyiwe marekebisho.Ukiilazimisha iendelee na kazi ama iendelee na safari madhara yake ni makubwa sana kwa abiria,mazingira na hata watu waliokaribu na mashine hiyo!!Kataa vitisho,kataa kununuliwa kama bidhaa,kataa uchochezi,kataa michezo michafu ya Kisiasa...Jiandae kupiga kura yako kwa Diwani,Mbunge na Rais wa UKAWA.....MUNGU ibariki TANZANIA na watu wake wote!!
 
Lowassa hana muda mchafu wa kutengenezea watu kadi feki ili eti waonekane wamehama ccm.Mpaka sasa wanachama wa ukawa ni 15m
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom