Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,079
UNAPOAMUA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI NA KWA WAKATI SAHIHI...
Baadhi ya watu hupenda kukukatisha tamaa!
STORY YA NAZI: Mnamo mwaka 1998 nilinunua miche 12 ya nazi (mbegu ndefu) maeneo ya kwa
mfipa, kibaha, mkoa wa Pwani kwa bei ya Tshs. 800 kwa kila mche. Nilisafirisha minazi hiyo hadi
Mwanza na yote ilifika salama. Nilijaribu kuomba ushauri jinsi ya kupanda vizuri miche ya minazi
kwa mzee mmoja wamakamu ambaye ni jirani yangu. Alichoniambia sitasahau mpaka
sasa...."kijana kuna miti mingine ni mikosi tu, wewe ulishaona wapi aliyepanda miti ya minazi huwa
anakula matunda yake? utakufa kabla ya kuziona hizo nazi" Nilifikiri na nikafanya maamuzi ya
kuendelea na utaratibu wangu kupanda miche hiyo. Bahati mbaya miche 4 ilikufa baada ya
kupanda na ikabaki 8. Baada ya miaka 9 nilianza kuona nazi zinatoka na baada ya muda nikaanza
kuvuna nazi. Kama ilivyokawaida ya ujirani mwema, niliamua kumpatia nazi 8 baada ya mvuno wa
kwanza alishukuru sana. Baada ya muda kupita hivi toka nimpatie nazi nikamuona naye anachimba
mashimo na kuniomba ushauri afanyeje ili aweze kupanda vizuri hiyo miche ya minazi, nilistaajabu
sana!! Na wala hakukumbuka tena yale maneno alioniambia. Baada ya muda nikaona mwamko
mkubwa wa majirani zangu kupanda miti ya minazi na sasa karibu kila nyumba zinazonizunguka
wamepanda minazi.
Photo: Huuni mmoja wa mti wa mnazi, ambao naendelea kuvuna matunda yake....minazi hii ina
uwezo wa kuzaa mpaka miaka 100.
KILIMO KINALIPA. Chanzo.Copy and Paste