Maelezo ya Polisi kuhusu Panya Road hayaeleweki. Kwanini wanaua na siyo kukamata? Je, ni yale yale ya akina Zombe yanajirudia?

field marshall1

JF-Expert Member
Sep 17, 2017
1,171
2,730
Ni mara nyingi sana inatokea kuona polisi wetu wakisimama kwenye podium kuzungumza na waandishi wa habari, wanachozungumza mara nyingi ni "watuhumiwa walipigwa risasi na wakafa wakikimbizwa hospitali" Wakati huo huo hakuna ushahidi wa polisi kushambuliana na hao wanaowaita wahalifu, wananchi hawaoni na kuhakikisha kuwa kulikuwa na milio ya risasi.

Miaka ya nyuma, Zombe na wenzake walileta hadithi inayofanana na haya yanayoendelea....Kirahisi rahisi wafanyabiashara wakauawa, huku wakisingiziwa ni majambazi, hadi tume ilivyoundwa ikathibitisha kuwa wale ni wafanyabiashara waliopelekwa Mabwe pande na kuuliwa huko.

Sasa haya leo yameshamiri, polisi wanatatua matatizo yao kwa kuua, kwa nini wasiwashike? Kweli kuna asiye na akili akataka kupigana na panga na polisi walio na silaha kali? Katika kipindi cha wiki 3, watu/wananchi 19 wameshapoteza maisha mikononi mwa polisi. Maelezo yao polisi wetu hayaeleweki. Yaani ya kuunga unga tu!

Nani leo hii atawaamini polisi wanaoua watu wasio na makosa? Kwanini wasiwakamate washukiwa wa ujambazi ili waweze kuwataja wauaji wengine? Na mbona hawaonyeshi sehemu kulipokuwepo hayo mapambano? Wanaonyesha mapanga yenye damu (Polisi wanajua ukweli kuwa wanadanganya)

Polisi wetu hamna credibility, mnaua, mnatesa na kuumiza wananchi wasio na hatia. Hakuna anayewaamini kwa matendo yenu.
 
Hata mimi napata mashaka wanaouawa na polisi ni panya rodi kweli au polisi wanatuma ujumbe kwa panya rodi halisi? au polisi wanataka kutuaminisha kuwa kazi haijawashinda maana wananchi wamekuwa wakali juu ya polisi kushindwa kudhibiti panya rodi na matukio mengine kwa ujumla.
 
Acha wauwe mbona kafa Binti huko kawe na panya road hao hao, wengine wamekatwa na mapanga na hao hao panya road? Kukamatwa wanakamatwa wanafungwa vifungonvya muda mfupi wanamaliza vifungo vyao wanarud uraiani kufanya Yale yale, dawa yao ni kuuawa!
 
Ukiacha FUTUHI za Polisi za Kuua Panya road ila kiukweli dawa ya kuwaangamiza panya road na majambazi ni "KUWAPA VYUMA WALE" ila wawe panya road na majambazi kweli na isiwe hasira za kugombea mademu tu na kuleta FUTUHI eti kajinyonga na "TAMBALA LA DEKI".
 
Polisi siku hizi wanayafanyia kazi matamko ya wanasiasa kisiasa, wanaona dawa pekee ya kuwaridhisha wananchi dhidi ya panyarodi ni kutangaza wamewaua, sheria kwa sasa ziko kapuni.

Ajabu, sitashangaa hao wanasiasa wakianza kujitokeza na kulaani vitendo vya polisi, hapo ndipo akili zitawarudia polisi waanze tena kufanya kazi zao kiweledi.
 
Kwa vile panya road wanavunja nyumba za watu, wanaiba, wanajeruhi na wanauwa watu wasiokuwa na hatia basi acha na wao wauwawe tu.
Tatizo ni je hao ni panya road? Polisi wa Tanzania wamedanganya mara ngapi?Ni nani asiyewajua polisi wetu, kuanzia kutekwa kwa MO Dewji, Roma na wengineo. Na zile maiti zilizookotwa kwenye viroba? Hapo bado kesi za kufoji wanazotengenezewa watu wengine wanaoikosoa serikali hizi za CCM.
Sina tatizo kama ni Panya road kweli, lakini tunaijua vizuri polisi yetu.
 
Kwa hili nawatetea polisi, panya wanaoperate katika mfumo ambao kumkamata hai ni ngumu sana, wanafanya uhalifu wakiwa wanajificha kwenye kundi la raia wema.
Kwahiyo hapo wanawaua na raia wema, maana wamejichanganya! Ni vema wakawakamata Kisha wahojiwe. Halafuraia wema waachiwe na wahalifu wapelekwe mahakamani.
 
Iron boy hawezi kutumia akili anaamini matumizi ya nguvu.


Tuwavumilie maana hawajielewi bado tupo zama za kikoloni..

Tatizo Ni Elimu! Elimu! Elimu
 
Back
Top Bottom