Maelezo ya Mheshimiwa Rais Kuhusu Ardhi kwa Wawekezaji na Taarifa ya TIC

SolarPower

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
223
27
Wakuu,

Natumaini wote jana mlifanikiwa kusikiliza hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa jana usiku. Kati ya mambo ambayo Rais Kikwete aliyoongelea jana ni pamoja na namna ambavyo serikali hutoa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na wale wa kutoka nje ya nchi yetu.

Katika hili Mheshimiwa Rais alilieleza taifa kuwa Wawekezaji hupatiwa ardhi ya Uwekezaji Kupitia Kituo chetu cha Uwekezaji TANZANIA INVESTMENT CENTRE (TIC). Katika ufafanuzi wake alilieleza taifa kuwa Kila wilaya imetenga maeneo maalum ya ardhi ya uwekezaji ambapo ardhi hizo ziko chini ya Benki ya Ardhi inayosimamiwa na TIC.

Katika kipindi cha TUAMBIE kilichorushwa na TBC kama wiki moja na nusu iliyopita, maafisa wa TIC walilieza taifa kuwa toka TIC ianzishwe ardhi ambayo TIC wameishaitoa kwa wawekezaji wa ndani na nje mpaka sasa haifiki Hekta 17,000. Lakini gazeti la The East African la tarehe 14-20 Mei 2012 katika ukurasa wake wa mbele lilitoa taarifa kuwa nchi yetu inaongoza katika kutoa ardhi kubwa kwa wageni ambapo mpaka sasa tumeishatoa kiasi cha Hekta 2,200,000 (kiasi cha kama ekari mil 5.6---mpaka sasa taarifa ya gazeti hilo bado haijakanushwa na Serikali yetu).

Je ni kwanini ardhi hii (Hekta mil 2.2) TIC hawakuhusika katika kuitoa kama ambavyo Mheshimiwa Rais alivyoeleza jana katika hotuba yake kuwa TIC wao ndiyo wahusika wakuu katika kutoa ardhi kwa ajili ya uwekezaji.

Taarifa hiyo ya Gazeti la The East African inaonyesha pia kuwa kampuni moja tu ya Sweden imepewa Hekta 797,000 ( kama ekari mil 2.02438).

Naomba kuwasilisha
 
Kwa nini na watanzania wasipewe au ni kwa ajili ya waupe tu?
 
Kila anachosema rais Kikwete si kweli. Unakumbuka 2007 alituambia kufikia Desemba tatizo la umeme litakuwa historia? Vile vile alituhakikishia kuwa Richmond haijalipwa hata senti moja?
 
Ardhi ya TIC ni ile ardhi rasmi ilitotolewa kupitia TIC, na ile story ya Citizen ni jumla ya ardhi yote inayomilikiwa na wageni ambayo wameinunua direct bila kupitia TIC.

Hao wa Sweeden wamemilikishwa eneo kubwa hivyo ili kuzalisha biofuel. Pia kampuni ya Sunbiofuel inamiliki ekari 8,200 kule Kisarawe kwa kilimo cha Mibono Kaburi.

Hata Watanzania wenye uwezo, ruksa kumiliki ardhi kwa ajili ya uwekezaji, tatizo letu kubwa ni hatuna uwezo!.
 
Ardhi ya TIC ni ile ardhi rasmi ilitotolewa kupitia TIC, na ile story ya Citizen ni jumla ya ardhi yote inayomilikiwa na wageni ambayo wameinunua direct bila kupitia TIC.

Hao wa Sweeden wamemilikishwa eneo kubwa hivyo ili kuzalisha biofuel. Pia kampuni ya Sunbiofuel inamiliki ekari 8,200 kule Kisarawe kwa kilimo cha Mibono Kaburi.

Hata Watanzania wenye uwezo, ruksa kumiliki ardhi kwa ajili ya uwekezaji, tatizo letu kubwa ni hatuna uwezo!.

Pasco,

Asante kwa post yako. Moja ya tatizo kubwa hapa ni kwanini utoaji wa ardhi kubwa kiasi hicho TIC hawahusishwi. Pia ni uwezo upi huo unaouzungumzia ambao sisi Watanzania hatuna.
 
Kila anachosema rais Kikwete si kweli. Unakumbuka 2007 alituambia kufikia Desemba tatizo la umeme litakuwa historia? Vile vile alituhakikishia kuwa Richmond haijalipwa hata senti moja?

Hilo la umeme nalikumbuka vizuri sana. Pia katika Kampeni za 2005 alisema Mwanza ataigeuza kuwa Calfornia na katika Kampeni za 2010 aliahidi kuiendeleza kigoma na kuwa kama Dubai.
 
Back
Top Bottom