OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 48,778
- 102,143
Kama mnakumbuka CAG Prof.Assad alihoji malipo ya matibabu ya Spika zaidi ya dola 12,000,000 mwaka 2017.
Mpaka leo CAG hajajiridhisha na malipo Ndugai hajapeleka nyaraka kufunga hoja.
Humu JF tunataka kuona nyaraka zote zinawasilishwa kwa CAG vyeti vya matibabu na madaktari walifanya operesheni.
Wananchi tunataka vyeti vyote vya hospitali, hesabu ya madaktari, alifanyiwa operesheni ngapi. Tunataka hesabu kamili ya miezi yote ya matibabu kama zimefika Dola za kimarekani milioni 12.
Kama ameshindwa arudishe hela,ili CAG wa watu afanye mambo mengine anachoka kusubiri toka 2017.