Maduka ya Vodacom kuwa wazi kwa masaa 24 kuanzia tarehe 20

Chachasteven

JF-Expert Member
Jul 4, 2014
1,878
1,849
Mchakato wa kusajili laini za simu kwa alama za vidole bado ni mgumu sana kwa sababu kadhaa. Moja na kubwa ikiwa ni ya NIDA kushindwa kutoa vitambulisho kwa wakati kulingana na idadi ya watu pamoja na mahitaji na muda uliopangwa. Pamoja na kuwa siku za kukamilisha usajili ziliongezwa, bado kuna changamoto kubwa ya watu ambao bado hawajasajiliwa.

Ukiacha taarifa ya usalama wa pesa za watu watakaofungiwa laini zao - yaani pesa zitakuwa salama kwa miezi mitatu tu na baada ya hapo mmiliki wa laini atatakiwa kufuatilia kwenye kampuni husika - Vodacom pia imekuja na mbinu itakayowezesha mchakato wa kusajili laini kwa alama za vidole uwe wa haraka. Baadala ya kufunga masaa ya kawaida ya kazi, wao watakuwa wazi kuwahudumia wateja kwenye maduka yao kwa masaa 24 hadi tarehe mbili (2) mwezi wa pili. Kazi kwenu.

Yajayo yanafurahisha. Upo tayari!
 
Wangebadili kabisa ratiba ya muda wao kufanya kazi iwe 24/7.
.
Ni ushamba baadhi ya huduma kutolewa kwa masaa 11-12 kwa siku 5 za wiki na huduma pekee sijui wanaiitaje ya kuwapigia simu na kuchati nao ndio haina kikomo cha muda.
 
Mchakato wa kusajili laini za simu kwa alama za vidole bado ni mgumu sana kwa sababu kadhaa... Moja na kubwa ikiwa ni ya NIDA kushindwa kutoa vitambulisho kwa wakati kulingana na idadi ya watu pamoja na mahitaji na muda uliopangwa. Pamoja na kuwa siku za kukamilisha usajili ziliongezwa, bado kuna changamoto kubwa ya watu ambao bado hawajasajiliwa.

Ukiacha taarifa ya usalama wa pesa za watu watakaofungiwa laini zao - yaani pesa zitakuwa salama kwa miezi mitatu tu na baada ya hapo mmiliki wa laini atatakiwa kufuatilia kwenye kampuni husika - Vodacom pia imekuja na mbinu itakayowezesha mchakato wa kusajili laini kwa alama za vidole uwe wa haraka. Baadala ya kufunga masaa ya kawaida ya kazi, wao watakuwa wazi kuwahudumia wateja kwenye maduka yao kwa masaa 24 hadi tarehe mbili (2) mwezi wa pili. Kazi kwenu.

Yajayo yanafurahisha. Upo tayari!
Kila mtu analalamika NIDA wakati jukumu lao ni zito.Pengine Mh. Rais atatoa uamuzi wa kutoa nyongeza ikifika saa tano usiku kulingana na repoti zitakazomfikia na hashindwi kufanya hivyo.
 
Kila mtu analalamika NIDA wakati jukumu lao ni zito.Pengine Mh. Rais atatoa uamuzi wa kutoa nyongeza ikifika saa tano usiku kulingana na repoti zitakazomfikia na hashindwi kufanya hivyo.
Hakuna anayelalamika. Kwanza kwanini unachanganya kulalamika na kuongea ukweli?? Kuongea ukweli ni kulalamika??

Hebu tafuta kamusi usome maana ya "lalamika" halafu uje tuendelee kujadili.
 
Wangebadili kabisa ratiba ya muda wao kufanya kazi iwe 24/7.
.
Ni ushamba baadhi ya huduma kutolewa kwa masaa 11-12 kwa siku 5 za wiki na huduma pekee sijui wanaiitaje ya kuwapigia simu na kuchati nao ndio haina kikomo cha muda.
Jamaa hawajali. Watafanya hivyo endapo wanakaribia kula hasara ili kuokoa pesa. Vinginevyo utalalamika sana, kaka.
 
Mchawi mbn anajulikana!
Voda, tigo, airtel etc wamewasambaza watu wao wengi Mtaani wa nasajili?
Ila tatizo ni kitambulisho cha taifa

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli. Hilo ndiyo tatizo kubwa... Kama Serikali ingekuwa inajiongeza ingefanya hii ishu iwe ni endelevu sio yenye kikomo, haswa kwa muda mfupi kama huo, au labda ingeweka muda wa kutosha kufanikisha shughuli yote. Acha tuone.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom