Maduka ya Dawa yaliyo nje ya mageti ya Hospitali za Serikali huwa na dawa muda wote lakini ndani ya Hospitali husika hamna dawa

Siyo kwamba huruhusiwi kuandika.

Ila ukiandika Dawa ambazo hazipo store ya hospitali maana yake mgonjwa akanunue ndio utapata lawama kama hizi.

Kwahiyo, inadhauriwa Umwandikie mgonjwa Dawa zilizopo store ili kukwepa lawama kama hizi.
Hivi huwa tatizo ni nini kwenye ishu ya dawa? Kwamba serikali haina pesa ama ni vile sio kipaumbele?

Maana serikali inaweza agiza Land Cruiser hata 700 za 150M mpaka 200M!

Hivi kwa billion 100 ni dawa kiasi gani zinaweza nunuliwa?

Yani mie nikipewa hii nchi naweza nikaiendesha kwa namna ya tofauti sana! Its high time matatizo madogo madogo yanatakiwa yaishe haya.
 
Hata wakati wa jpm mfumo ulikuwa huu huu
Dawa hospital hakuna ila maduka ya dawa nje
Zipo!
Nchi ngumu hii kuanzia juu mpaka chini

Ova
Na sio kwamba dawa hamna ila ni hujuma tu zinafanyika! Hata ununue dawa kontena 100 lazma watatengeneza deficit tu kuwa dawa hamna au zimeisha ili ukanunue duka la nje ya hospitali!
 
Umedanganya , Sheria ilimzuia Magufuli kufunga maduka ya dawa karibu na Hospitali , akaamua kuanzisha maduka ya MSD ili kuyashinda maduka binafsi , huku akisahau kwamba kila wodi ya Wagonjwa kule ndani , sewahaji , Mwaisela nk zinayo maduka humo humo vyumbani , kifupi alichemsha vibaya .

Maduka ya dawa hukaguliwa na Mamlaka ya chakula na dawa , hakuna dawa ya serikali inaweza kuuzwa mle , maana dawa zao zina nembo
Kumbe sheria ilimzuia? Si mnasema alikuwa hafuati sheria?

Mabavicha kuna wakati huwa mnajikaanga kwa mafuta yenu wenyewe!
 
Hivi huwa tatizo ni nini kwenye ishu ya dawa? Kwamba serikali haina pesa ama ni vile sio kipaumbele?

Maana serikali inaweza agiza Land Cruiser hata 700 za 150M mpaka 200M!

Hivi kwa billion 100 ni dawa kiasi gani zinaweza nunuliwa?

Yani mie nikipewa hii nchi naweza nikaiendesha kwa namna ya tofauti sana! Its high time matatizo madogo madogo yanatakiwa yaishe haya.
Tatizo kubwa lipo kwenye budgeting.

Unaweza kuaguza dawa za magonjwa fulani kulingana na takwimu zako. Halafu ghafla ukapata idadi kubwa sana ya wagonjwa husika kuliko kiasi cha dawa ulichonacho.

Na ukiagiza tena huwa inachukua muda mrefu kuleta.

Vile vile unaweza ukaagiza dawa na usiletewe kiwango ulichoomba.

Pia, vituo vya afya vimewekewa ceiling ya bajeti.

Huwezi kupanga bajeti (ikiwemo ya dawa ) zaidi ya kuwango ulichowekewa.

Na hii ceiling inatokana na takwimu kutoka kituo husika.
 
Tatizo kubwa lipo kwenye budgeting.

Unaweza kuaguza dawa za magonjwa fulani kulingana na takwimu zako. Halafu ghafla ukapata idadi kubwa sana ya wagonjwa husika kuliko kiasi cha dawa ulichonacho.

Na ukiagiza tena huwa inachukua muda mrefu kuleta.

Vile vile unaweza ukaagiza dawa na usiletewe kiwango ulichoomba.

Pia, vituo vya afya vimewekewa ceiling ya bajeti.

Huwezi kupanga bajeti (ikiwemo ya dawa ) zaidi ya kuwango ulichowekewa.

Na hii ceiling inatokana na takwimu kutoka kituo husika.
Maybe ila wenye pharmacy nje wao wanawezaje kuwa na range kubwa ya dawa?
 
Watu wa famasi hawafuati taratibu zozote za manunuzi. Mzigo ukiisha unaagizwa.

Mambo ya serikali hayaendi hivyo.

Drug editing ya nguvu huwa inafanyika. Unaweza kufungwa.
Duh basi serikali yenyewe kumbe inafeli
 
Maybe ila wenye pharmacy nje wao wanawezaje kuwa na range kubwa ya dawa?
Tena kwa wakati wote, hata nesi anaefanya kazi serikalini ukimwambia nataka dawa fulani kesho anakuletea unampa hela yake, lakini ukienda huko Hospital kesho yake dawa ile ile hakuna unaandikiwa.
Inavyooenekana ni kuwa kila mtu anakula kulingana na urefu wa kamba yake,na usimamizi mbovu
 
Tena kwa wakati wote, hata nesi anaefanya kazi serikalini ukimwambia nataka dawa fulani kesho anakuletea unampa hela yake, lakini ukienda huko Hospital kesho yake dawa ile ile hakuna unaandikiwa.
Inavyooenekana ni kuwa kila mtu anakula kulingana na urefu wa kamba yake,na usimamizi mbovu
Yani inashangaza na hao madaktari wanaoandika hizo dawa wao kwanini wasimshauri mtu wa bohari kwamba alete varieties za dawa! Yani kwanini iwe Paracetamol tu na sio Aspirin, Diclopar,Ibuprofen?

Yani kwanini dawa iwe aina moja tu!
 
Na
Watu wa famasi hawafuati taratibu zozote za manunuzi. Mzigo ukiisha unaagizwa.

Mambo ya serikali hayaendi hivyo.

Drug editing ya nguvu huwa inafanyika. Unaweza kufungwa.
Inakuwaje miaka yote tangu uhuru serikali inashindwa kudili na swala muhimu kama hilo ambalo linahusu afya ya binadamu? Je mbona Hospital binafsi mara nyingi hukosi dawa? Ifike mahali sasa Hospital za serikali ziwe ndo kimbilio la wananchi kutokana huduma bora zitolewazo
 
Duh basi serikali yenyewe kumbe inafeli
Mkuu, mambo ya serikali unaweza kudhani yanakisewa ila ukiwa kwenye mfumo ndio utajua kwanini yako hivyo yalivyo.

Kwanza kwa mfumo wa Afya ulivyo, vituo havina CEOs wala wahasibu.

Na vinaongozwa na na Waganga kama CEOs.

Siku hizi kila kituo cha afya kina Account bank, na pesa zote za CHF, NHIF, basket fund na User fees ( cost sharing ) huwa zinaingia kwenye akaunti husika.

Hawa maCEOs wa vituo ndio watungaji wa Mpango wa bajeti, na tatizo wengi hawajui huwa wanaandika andika tu ilimradi wameshinikizwa na Makatibu wa Afya.

Mimi kuna kakituo nipo, huwa tunapata user fees kama 7M kwa mwaka lakini tumebajeti mpaka tunakunywa chai na mikate, manesi wanapata vitambaa na pesa za uniform pamoja na extra duties.

Ila kuna kituo kikubwa tu, huwa wanapata mpaka 15M kwa mwaka lakini wana maisha magumu sana kutokana na ukilaza wa CEO wao( Daktari ).

Ili upunguze tatizo hili inabidi uwe makini sana na takwimu ili ukiagiza dawa au kupanga bajeti usiwe na DEFICIT.
 
Mkuu, mambo ya serikali unaweza kudhani yanakisewa ila ukiwa kwenye mfumo ndio utajua kwanini yako hivyo yalivyo.

Kwanza kwa mfumo wa Afya ulivyo, vituo havina CEOs wala wahasibu.

Na vinaongozwa na na Waganga kama CEOs.

Siku hizi kila kituo cha afya kina Account bank, na pesa zote za CHF, NHIF, basket fund na User fees ( cost sharing ) huwa zinaingia kwenye akaunti husika.

Hawa maCEOs wa vituo ndio watungaji wa Mpango wa bajeti, na tatizo wengi hawajui huwa wanaandika andika tu ilimradi wameshinikizwa na Makatibu wa Afya.

Mimi kuna kakituo nipo, huwa tunapata user fees kama 7M kwa mwaka lakini tumebajeti mpaka tunakunywa chai na mikate, manesi wanapata vitambaa na pesa za uniform pamoja na extra duties.

Ila kuna kituo kikubwa tu, huwa wanapata mpaka 15M kwa mwaka lakini wana maisha magumu sana kutokana na ukilaza wa CEO wao( Daktari ).

Ili upunguze tatizo hili inabidi uwe makini sana na takwimu ili ukiagiza dawa au kupanga bajeti usiwe na DEFICIT.
Dah usimamizi hapo sasa naelewa, kila mtu ana utashi wake kwenye kusimamia rasilimali
 
Na

Inakuwaje miaka yote tangu uhuru serikali inashindwa kudili na swala muhimu kama hilo ambalo linahusu afya ya binadamu? Je mbona Hospital binafsi mara nyingi hukosi dawa? Ifike mahali sasa Hospital za serikali ziwe ndo kimbilio la wananchi kutokana huduma bora zitolewazo
Wewe unajua ndani ya mwaka mzima familia yenu mtaugua nini na wangapi ?

Mambo huwa yanafanyika kwa makisio tu.

Je, ukikadiria kuwa kwa mwaka huu wa 2022/23 tunatarajia kupata wagonjwa wa pressure 500 halafu ghafla ukapata 800 hujapungukiwa na dawa hapo?

Au unadhani mifumo ya serikali dawa zikiisha unapoga tu simu mzigo unaletwa🤣
 
Ni kweli mkuu ila pia dunia ya sasa usipojitambua ukawa na ujinga mwingi unaweza ukalipishwa kiingilio na mkeo kwenye nyumba yako ambayo umeinjenga mwenyewe.

Huwezi kulipa kodi na tozo halafu ulipie na huduma ambazo kimsingi zilitakiwa ziboreshwe na kodi ambazo umelipia.

Serikali haiombwi kuboresha huduma kwa hisani ni wajibu wake kuboresha ila kwa wajinga wajinga wanaweza kuhisi kuwa eti kutoa rushwa ni lazima ili upewe huduma.
Ulicho sema ni sahihi kabisa ila kutaka kutuamisha ya kwamba kipindi cha JPM hili tatizo halikuwepo ni kundekeza siasa uchwara na propaganda ambazo hazita saidia kutatua tatizo.
Ifikie hatua Wtz tukubali ya kwamba taifa letu lina mfumo mbovu wa kiutawala na kiuwajibikaji na sio kumlaumu mtu mmoja.
 
Ulicho sema ni sahihi kabisa ila kutaka kutuamisha ya kwamba kipindi cha JPM hili tatizo halikuwepo ni kundekeza siasa uchwara na propaganda ambazo hazita saidia kutatua tatizo.
Ifikie hatua Wtz tukubali ya kwamba taifa letu lina mfumo mbovu wa kiutawala na kiuwajibikaji na sio kumlaumu mtu mmoja.
Hapo umeongelea Point sasa! Mjadala unafungwa
 
Umedanganya , Sheria ilimzuia Magufuli kufunga maduka ya dawa karibu na Hospitali , akaamua kuanzisha maduka ya MSD ili kuyashinda maduka binafsi , huku akisahau kwamba kila wodi ya Wagonjwa kule ndani , sewahaji , Mwaisela nk zinayo maduka humo humo vyumbani , kifupi alichemsha vibaya .

Maduka ya dawa hukaguliwa na Mamlaka ya chakula na dawa , hakuna dawa ya serikali inaweza kuuzwa mle , maana dawa zao zina nembo
Hebu jaribu kueleweka kwa kuijibu hoja ya KUKOSEKANA dawa...
 
Kipindi cha awamu ya tano Mheshimiwa Raisi Magufuli alipiga marufuku sana ya maduka yaliyo nje ya hospitali za serikali, kwani ilionekana kuwa hayo maduka ndo chanzo cha Kukosekana dawa ndani ya hospitali hizi za serikali.

Wengi tulishuhudia huduma nzuri pamoja na upatikanaji wa dawa ndani ya hospitali lakini leo mambo yamejirudia pale pale.

Leo hii Mwananchi wa kawaida anaona ni bora akapate huduma katika Hospitali binafsi kuliko ya serikali kutokana na huduma mbovu zitolewazo katika Hospitali za umma.

Ndani ya hospitali za serikali mara nyingi utapimwa vipimo lakini baada ya majibu kuja utaandikiwa paracetamol na dawa nyingine utaambiwa kanunue duka lililopo nje ya geti.

Kwa upande wa kina mama wanaojifungua tunaambiwa ni bure lakini Hospital nyingi za umma huwa wanalipishwa, huku wajawazito wakiamriwa waje na vifaa vya kujifungulia kama vile pamba. Gloves nk.

Wizara ya afya wafuatilie na pia wawe wakali maana Hospitali za umma zimekuwa changamoto sana kwa wananchi wa kawaida.
Fungua na wewe hizo ni fursa kama fursa zingine
 
Back
Top Bottom