Madudu ndani ya Shirika la Viwango (TBS)

TBS inapaswa kusafishwa. Tunalishwa sumu kwa ajili ya akina Ekelege kupokea 10% na kupitisha bidhaa feki nchini zisizo na ubora. Wanatuua na kansa hawa! Ekelege afukuzwe kazi pamoja na mama Kezia Mbwambo ( Mkurugenzi wa Ubora) pamoja na katibu Mkuu Viwanda Joyce Mapunjo waondoke. Kupitia watu hao watatu afya za Watz zipo mashakani na wameiba fedha nyingi sana kwa ufisadi wao wa kupitisha bidhaa zisizo na viwango.
 
Wachunguzi waenda Singapore kuchunguza miradi hewa ya TBS

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imetuma wakaguzi kwa ajili ya kukagua ofisi za ukaguzi wa magari nje ya nchi zinazosimamiwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Hatua hiyo imekuja baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC); Fedha na Uchumi; na Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kudai kuwa Mkurugenzi wa TBS,Charles Ekelege, aliwasilisha taarifa za uongo kwamba Tanzania ina ofisi ya ukaguzi wa magari nje ya nchi wakati siyo kweli.

Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, alisema kutokana na tuhuma zenyewe kuhusisha nje ya nchi, ofisi yake inalazimika kutuma wakaguzi ili kufanya uchunguzi na kuhakiki ukweli kuhusu tuhuma hizo, jambo ambalo anaamini linaweza kupata taarifa sahihi. "Tumelazimika kutuma wakaguzi nje ya nchi kwa ajili ya kufanya uchunguzi na kukagua ofisi za ukaguzi wa magari hayo, hii itasaidia kupata taarifa sahihi kuhusu tuhuma hizo na ukweli wa mambo yenyewe, jambo ambalo linaweza kurahisisha upatikanaji taarifa sahihi za madai hayo," alisema Utouh.

Aliongeza kuwa kutokana na hali hiyo, ofisi yake itakuwa makini katika suala hilo ili uamuzi utakaotolewa na Serikali usiweze kulalamikiwa na kuonekana umetokana na uonevu. Kwa mujibu wa Utouh, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo, aliwasilisha taarifa hizo mwishoni mwa wiki iliyopita na kwamba, tayari wameanza kuifanyia kazi ili kupata ukweli wa madai hayo.

"Siwezi kumuonea mtu katika hili, ndiyo maana naifanya kazi ya kuhakiki kwa umakini zaidi il taarifa yake iweze kukamilika na uamuzi utakaotolewa usiwe wa kumuonea mtu,"alisema. Hata hivyo, kamati hizo zilitoa mapendekezo yao ya kumtaka CAG kuchunguza tuhuma hizo kipindi cha mwezi mmoja kwa kulinganisha na maelezo yatakayotolewa na Mapunjo.

Januari 27, mwaka huu POAC na PAC ilibaini kuwapo kwa tuhuma hizo zilizoelekezwa kwa mkurugenzi huyo na kumtaka asimamishwe kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake.

Wakaguzi waenda Singapore kuchunguza miradi hewa ya TBS
 
Madudu ndani ya mashirika ya umma yamezidi kuibuka ambapo jana Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (POC), ilibaini kuwa Shirika la Viwango nchini (TBS), limedanganya taifa kwa kutumia makampuni hewa ya kukagua magari nje nchi. Utapeli huo ulibainika baada ya timu ya wabunge kufanya ziara katika nchi za Singapore, China na Japan kwa ajili ya kutembelea makampuni yanayoelezwa na TBS kwamba yanahusika na ukaguzi wa magari kabla ya hayajaingia hapa nchini.

Hata hivyo, wabunge hao walijionea vituko baada ya kufika huko nje ya nchi ambapo walibaini hapakuwa na kampuni wala ofisi yoyote inayofanya kazi hiyo ya ukaguzi wa magari. Mmoja wa wabunge hao, Deo Filikunjombe, alisema jana kuwa baada ya kufika walipata aibu mpaka wakafikia hatua ya kukimbilia ofisi za Ubalozi wa Tanzania zilizopo katika nchi hizo kwa ajili ya kujihifadhi. "Huko nje, hakuna ofisi, makampuni wala ofisi ambazo zimekuwa zikidaiwa na TBS zipo huko kwa ajili ya kukagua magari kabla hayajaingia nchini ili kujua ubora wake," alisema Filkunjombe.

Kutokana na utapeli huo kuwa mkubwa, Kamati imemuandikia barua Spika wa Bunge, Anne Makinda, kutaka suala hilo litinge bungeni likajadiliwe na wabunge wote. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa POC, John Cheyo, alisema licha ya wabunge kukosa ofisi za makampuni hayo huko nje ya nchi, lakini pia hakuna mchanganuo wa fedha zilizopatikana kutokana na ukaguzi huo wa magari nje ya nchi.

Alisema TBS kwa miaka 10 mfululizo imekuwa ikifanya vibaya katika mahesabu yake na kueleza kuwa hakuna shirika bovu la serikali kama hilo hapa nchini. Imedaiwa kuwa baadhi ya wabunge waliokwenda nje ya nchi kuangalia makampuni hayo walitaka kumpiga ngumi, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Charles Ekelege, ambaye aliwaongoza baada ya kubaini kwamba walikuwa wanatapeliwa.

Kamati za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na ile ya Hesabu za Serikali (POC), jana zilisema ukaguzi wa magari unaingiza fedha nyingi lakini TBS imeshindwa kueleza mahali zilipo wala mchanganuo wake. "Huko nje ya nchi hatukukuta ofisi wala wakala wa ukaguzi wa magari baada ya kufanya ziara nje ya nchi,” alisisitiza Makamu Mwenyekiti wa POAC, Filikunjombe.

Wabunge hao ambao ni wajumbe wa Kamati hizo, walisema kutokana na utendaji mbovu wa TBS, kwa sasa haijulikani magari mangapi yanayokaguliwa ubora wake kabla ya kuingia nchini na ukaguzi huo unaingiza kiasi gani cha fedha.
Kutokana na utata huo, kamati hizo zimeitaka Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na TBS wiki ijayo kufika mjini Dodoma ili kutoa maelezo ya kina.

SOURCE: NIPASHE
kuan tatizo gani kuweka kituo cha kukagulia hapo nyumbani tanzania ya kwamba magari yote kabla hayjapewa plate numbers yakaguliwe hapo nyumbani kwa kulipia gharama ya USD 200 kwa gari. Hii itawezesha serikali kuingiza mapato mengi zaidi kuliko kungojea mawakala wa nchi za nje waliowaweka. Machine zenyewe zinagharimu Usd kama 50,000 hivi, ambazo zitaleta ajira nyumbani. Wataalam kila siku tunazalisha hasa vijana wa Technical colledges.
 
Tatizo kamati ya zito haijatoa report ya safari, kwa mujibu wa waziri.zitto ajibu hili swali kwanza
 
Kamati za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na ile ya Hesabu za Serikali (POC), jana zilisema ukaguzi wa magari unaingiza fedha nyingi lakini TBS imeshindwa kueleza mahali zilipo wala mchanganuo wake. "Huko nje ya nchi hatukukuta ofisi wala wakala wa ukaguzi wa magari baada ya kufanya ziara nje ya nchi,” alisisitiza Makamu Mwenyekiti wa POAC, Filikunjombe.

SOURCE: NIPASHE

Hawa wabunge wababaishaji tu, huko Singapore na Hongkong na China wanafuata POSHO tu and nothing else.
Information waliyoipata huko wangeweza kuipata hata hapa hapa Tanzania kama wao ni watu makini.

Kama wao ni wazalendo halisi kama wanavyoijidai WAKAWAPIGE NGUMI wahusika wa EPA, RICHMOND na KAGODA walioko humo humo Bungeni.
Wanafuatilia vidagaa na kuyaachia mapapa yakitokomea, unafiki mtupu!!!!
 
TBS Board Ordered to Suspend DG

THE government has directed the Tanzania Bureau of Standards (TBS) Board to suspend its Director General, Mr Charles Ekelege to pave way for investigations over the alleged subcontracting of ghost agents to carry out pre-shipment vehicle-inspection exercise.

Mr Ekelege is accused of contracting ghost offices in some Asian countries, causing massive losses to vehicle importers as well as government revenues.

A scandal surrounding pre-shipment inspection scheme adopted by TBS attracted public attention after the Parliamentary Public Organisations Accounts Committee (POAC) and the Controller and Auditor General (CAG) reports revealed discrepancies in the process.

It was also one of the agenda that created fierce debate in the just-concluded seventh parliamentary meeting in Dodoma last month. The Minister for Industry, Trade and Marketing, Dr Abdallah Kigoda, announced the government decision yesterday in Dar es Salaam while listing various strategies by the new team appointed to head the ministry.

"The alleged TBS scandal is one of the major causes for the ministry's rearrangement, thus to begin with, I have ordered the agency's board of directors to suspend Mr Ekelege pending further procedures, Dr Kigoda said. TBS board chairman, Mr Oliver Mhaiki, however, said the board was yet to receive the government instructions.

Mr Mhaiki said TBS Board would have an extra- ordinary meeting next week to discuss various issues pertaining to its performances, including the minister's suspension order. "Once we receive formal communication from the minister, it will be included in the agenda of the meeting for discussion," he said.

Meanwhile, TBS Board Chairman disclosed that findings during their recent visit to Asian countries where the pre-shipment inspection continues found excellent job being done to inspect goods destined for Tanzania. "We visited all the companies which won tender to carry out pre-inspection and realized an excellent work being done to ensure that Tanzania was not turned into a dumping ground for substandard goods including vehicles," he added.

Mr Ekelege was recently quoted as saying the first verification team went to Dubai and Japan in April 2010 with eight Members of the Parliament led by the then MP for Mbalali, Ms Estelina Kilasi. The second team went to Singapore and Hong Kong in August, last year, led by the POAC Vice-Chairman, Mr Deo Filikunjombe.

In Dubai, a company named Total Automotive Services was later proved to be inefficient prompting TBS to terminate the inspection contract, while in Hong Kong a company named Quality Motors closed shop in August 2011 due to poor business. Mr Ekelege added that during verification trip in Singapore they were to visit a company known as Planet Automotive (PTE) Ltd which he informed the team that it ceased operations since April 2011.
 
Kwani Nyerere alikuwa mwadilifu? Tuambie uadilifu wake ni upi.

Warioba namkumbuka alikuwa afisi ya mwanasharia mkuu. Sina kumukumbu nae.

Lakini nimefanya na watu zaidi ya 50 kutoka Mara akina Nyirabu na wengine wengi kutokea nikiwa wizara ya fedha muungano na mkoa wa Mwanza lakin sijapatapo kumuona mtu wa huko Mwadilifu. Labda nitajie wengine kama wapo waadilifu tuwaone.


Huu ndio upimbi yaani wewe kufanya kazi na watu 50 wa mkoa wa Mara umeshajiona ni mtaalamu wa tabia za zaidi ya watu milioni moja wa mkoa huo!
 
Huu ndio upimbi yaani wewe kufanya kazi na watu 50 wa mkoa wa Mara umeshajiona ni mtaalamu wa tabia za zaidi ya watu milioni moja wa mkoa huo!

Nimekuomba jambo dogo tu nitajie watu 5 tu kutoka mkoa huo walio na vyeo serikalini hususan level ya kimkoa ambaye ni mwadilifu?

Acha porojo.

 
Sitarajii hata siku moja umkubali Nyerere kama kiongozi bora katika nchi hii. Kuanzia kwenye masimulizi ya historia ya wazee wenu wa gerezani, nilikuona rangi zako halisi tunapomzungumzia Nyerere.
Ukweli ni kwamba wenye akili zao timamu na wanaozitumia vizuri wanajua na kukubali kwamba Nyerere alikuwa ni kiongozi muadilifu. Hakuna mtu amewahi kulalamika kwamba Nyerere katumia madaraka yake kumpora shamba, nyumba ama kampuni. Sasa hivi tunashuhudia maraisi wenu bora wanavyokimbizana kufanya biashara wakiwa ikulu. Wanaanzisha makampuni ya kuwaibia watanzania, wanajaza watoto wao, wake zao, wajomba, mashangazi na mabinamu zao serikalini na kwenye mashirika ya umma.

Nyerere kwa uadilifu wake hata siku moja hakuwahi kumbeba mwanaye yeyote, kumuingiza katika serikali ama mashirika ya umma.
Kwa mfano tumeambiwa watumishi wa ofisi za makao makuu ya cuf upande wa bara imejaa wapemba watupu, wenzake na maalim seif lakini upande wa zanzibar watumishi wote ni wapemba. Huo ndio uhuni mnaofanya huko kwenu na ambao mwalimu hakuufanya na asingethubutu kumvumilia mtu aufanye. Je ni sawa kusema kwamba chama chote cha cuf si waadilifu ama huo ni mzigo wa maalim na washikaji zake wachache wanaoshiriki kuchakachua ajira ktk chama?

acha kumtetea nyerere wewe, tatizo la watu mbaomezeshwa wrong history na mkaamini ndio nynyi. I WISH MWAMWINDI WA IRINGA ANGEMPIGA SHABA MSHENZ YULE. REST IN PIECES NYERERE.
 
Back
Top Bottom