Ndugu wana JF.
Mifumo ya EPZ au kama inavyojulikana kwa majina mengine kama SEZ, Freeport, Industrial Zones au majina mengine kama hayo imekuwa ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya viwanda na uwekezaji kwa nchi nyingi sana duniani, China karibu asilimia 75 ya uchumi wake ni viwanda vilivyo chini ya mfumo wa SEZ, hata ndugu zetu wa Kenya uchumi wao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na muundo huo. Pamoja na dhamira nzuri ya Serikali kuanzisha mfumo huu wa EPZ kwa ajili ya maendeleo na tija kwa Taifa, adhma hii inakwamishwa sana na baadhi ya wakurugenzi wa EPZA, wakurugenzi hawa wamekuwa kazi yao ni kuongea tu na kutaja taarifa za uongo huku wakijua kabisa kuwa wanadanganya serikali na umma kwa ujumla.
Baadhi ya mambo ambayo hata mtoto mdogo akifanya utafiti atagundua ni haya yafuatayo;
1. Uongo katika taarifa na takwimu wanazozitoa serikalini na kwa jamii
Ukisikiliza presentation zao utaona wanajigamba kuwa Taasisi ya EPZ imezalisha mpaka sasa ajira 16,500, lakini ukweli ni kuwa hakuna hata wafanyakazi elfu tano 5000, anayebisha apitie viwanda vya EPZ akikuta wafanyakazi zaidi ya hao arudi jamvini kusema mimi muongo. Hali hii imeendelea hata katika takwimu ya viwanda vinavyofanya kazi chini ya EPZ, takwimu zao zinaonyesha kuwa kuna viwanda zaidi ya 80 lakini ukipitia viwanda vyote hivyo ukweli ni kwamba ni viwanda chini ya kumi 10 tu vinavyofanya kazi. Mitaji na mauzo ya nje vyote ni vya kupikwa, haya yote yanafanywa na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Taasisi hiyo Bi Zawadia Nanyaro huku Mkurugenzi Mkuu akibariki uongo huo. Nashauri wakaguzi wanaokagua maendeleo ya EPZ wasiishie tu kwenye nyaraka za ofisini wanazopewa na wakurugenzi waende kwenye hivyo viwanda vinavyodaiwa kuwepo.
2. Kutoa Leseni kwa upendeleo kwa baadhi ya watu wasiokidhi vigezo
Chini ya muundo wa EPZ utoaji leseni upo chini ya mkurugenzi wa maendeleo Bi Zawadia Nanyaro ambaye amekuwa akitoa leseni kwa wawekezaji marafiki zake wasiokidhi vigezo vya uwekezaji wengine mpaka leo wamekamata plots ambazo hawajaziendeleza kwa zaidi ya miaka mitatu licha ya kuwepo kwa sheria ya kuwanyanganya kama wasipoendeleza ndani ya miezi sita kuanzia walipopewa leseni, amekuwa akiwakumbatia na kuwatetea kwa Mkurugenzi Mkuu Dr Meru, na Dr Meru bila kufahamu kuwa kufanya hivyo ni kinyume na taratibu na vilevile ni kujihushia credibility yake anakubaliana naye. Hali hii inasababisha wawekezaji wazalendo walio tayari kuwekeza na wenye vigezo kukosa nafasi.
3. Uhusiano mbaya kazini, Staha kwa wafanyakazi na matumizi mabaya ya rasilimali za umma
Hapa sasa ndo hali mbaya, kwani ukimuuliza mfanyakazi yoyote EPZA ni nani ana personality mbaya na bad image jibu utakalopata haraka ni Zawadia Nanyaro, Zawadia amekuwa siku zote akilalamikiwa kwa kauli zake mbaya kwa wafanyakazi, fitina na majungu kupeleka maneno ya kuwaua wafanyakazi wenzake tena wa chini yake kuwa hawawezi kutenda kazi na Mkurugenzi mkuu kwa sababu inasemekana wana mahusiano ya kimapenzi kazini inamlazimu akubali ili kumridhisha kumbe anachofanya ni kujichafulia career yake hasa kipindi hiki anachokaribia kustaafu, nadhani uhusiano huu ndo unaomfanya ashindwe kumchukulia hatua pale anapotumia mali ya taasisi kwa shughuli binafsi, kwa mfano ratiba ya gari la serikali STK 5768 limekuwa likifanya kazi za binafsi za Mkurugenzi Zawadia Nanyaro kwa ratiba ifuatayo, asubuhi linakuwa school bus kupeleka watoto katika shule mbili tofauti, mchana linafanya kazi za nyumbani, ikifika saa nane tu haijalishi kuna shughuli gani kiofisi gari lazima liondoke kufata watoto na kuwarudisha nyumbani huku shughuli za serikali zikilala, achilia mbali jumamosi na jumapili kupeleka watoto kuimba kanisani, sijui kama kila mkurugenzi angekuwa anafanya hivi kama shughuli za kiofisi zingefanyika. Me namshauri Mkurugenzi Mkuu aangalie yasije kumkuta ya wenzake wa TBS na TANTRADE ambazo zote pamoja na EPZA ni taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda.
Naomba nieleweke kuwa lengo si majungu ndo maana nimeleta takwimu, lengo ni kurekebisha baadhi ya watendaji wakuu wa hizi taasisi zetu za umma wanaodhani kuwa taasisi ni mali zao, huku wakifanya ubadhilifu wa mali za umma na utendaji sifuri. Naomba niachie wanajamvi wengine wachangie then nitarudi baadaye na taarifa nyingine. Mabadiliko ya kweli huanzia JF. Nawasilisha!
Mifumo ya EPZ au kama inavyojulikana kwa majina mengine kama SEZ, Freeport, Industrial Zones au majina mengine kama hayo imekuwa ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya viwanda na uwekezaji kwa nchi nyingi sana duniani, China karibu asilimia 75 ya uchumi wake ni viwanda vilivyo chini ya mfumo wa SEZ, hata ndugu zetu wa Kenya uchumi wao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na muundo huo. Pamoja na dhamira nzuri ya Serikali kuanzisha mfumo huu wa EPZ kwa ajili ya maendeleo na tija kwa Taifa, adhma hii inakwamishwa sana na baadhi ya wakurugenzi wa EPZA, wakurugenzi hawa wamekuwa kazi yao ni kuongea tu na kutaja taarifa za uongo huku wakijua kabisa kuwa wanadanganya serikali na umma kwa ujumla.
Baadhi ya mambo ambayo hata mtoto mdogo akifanya utafiti atagundua ni haya yafuatayo;
1. Uongo katika taarifa na takwimu wanazozitoa serikalini na kwa jamii
Ukisikiliza presentation zao utaona wanajigamba kuwa Taasisi ya EPZ imezalisha mpaka sasa ajira 16,500, lakini ukweli ni kuwa hakuna hata wafanyakazi elfu tano 5000, anayebisha apitie viwanda vya EPZ akikuta wafanyakazi zaidi ya hao arudi jamvini kusema mimi muongo. Hali hii imeendelea hata katika takwimu ya viwanda vinavyofanya kazi chini ya EPZ, takwimu zao zinaonyesha kuwa kuna viwanda zaidi ya 80 lakini ukipitia viwanda vyote hivyo ukweli ni kwamba ni viwanda chini ya kumi 10 tu vinavyofanya kazi. Mitaji na mauzo ya nje vyote ni vya kupikwa, haya yote yanafanywa na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Taasisi hiyo Bi Zawadia Nanyaro huku Mkurugenzi Mkuu akibariki uongo huo. Nashauri wakaguzi wanaokagua maendeleo ya EPZ wasiishie tu kwenye nyaraka za ofisini wanazopewa na wakurugenzi waende kwenye hivyo viwanda vinavyodaiwa kuwepo.
2. Kutoa Leseni kwa upendeleo kwa baadhi ya watu wasiokidhi vigezo
Chini ya muundo wa EPZ utoaji leseni upo chini ya mkurugenzi wa maendeleo Bi Zawadia Nanyaro ambaye amekuwa akitoa leseni kwa wawekezaji marafiki zake wasiokidhi vigezo vya uwekezaji wengine mpaka leo wamekamata plots ambazo hawajaziendeleza kwa zaidi ya miaka mitatu licha ya kuwepo kwa sheria ya kuwanyanganya kama wasipoendeleza ndani ya miezi sita kuanzia walipopewa leseni, amekuwa akiwakumbatia na kuwatetea kwa Mkurugenzi Mkuu Dr Meru, na Dr Meru bila kufahamu kuwa kufanya hivyo ni kinyume na taratibu na vilevile ni kujihushia credibility yake anakubaliana naye. Hali hii inasababisha wawekezaji wazalendo walio tayari kuwekeza na wenye vigezo kukosa nafasi.
3. Uhusiano mbaya kazini, Staha kwa wafanyakazi na matumizi mabaya ya rasilimali za umma
Hapa sasa ndo hali mbaya, kwani ukimuuliza mfanyakazi yoyote EPZA ni nani ana personality mbaya na bad image jibu utakalopata haraka ni Zawadia Nanyaro, Zawadia amekuwa siku zote akilalamikiwa kwa kauli zake mbaya kwa wafanyakazi, fitina na majungu kupeleka maneno ya kuwaua wafanyakazi wenzake tena wa chini yake kuwa hawawezi kutenda kazi na Mkurugenzi mkuu kwa sababu inasemekana wana mahusiano ya kimapenzi kazini inamlazimu akubali ili kumridhisha kumbe anachofanya ni kujichafulia career yake hasa kipindi hiki anachokaribia kustaafu, nadhani uhusiano huu ndo unaomfanya ashindwe kumchukulia hatua pale anapotumia mali ya taasisi kwa shughuli binafsi, kwa mfano ratiba ya gari la serikali STK 5768 limekuwa likifanya kazi za binafsi za Mkurugenzi Zawadia Nanyaro kwa ratiba ifuatayo, asubuhi linakuwa school bus kupeleka watoto katika shule mbili tofauti, mchana linafanya kazi za nyumbani, ikifika saa nane tu haijalishi kuna shughuli gani kiofisi gari lazima liondoke kufata watoto na kuwarudisha nyumbani huku shughuli za serikali zikilala, achilia mbali jumamosi na jumapili kupeleka watoto kuimba kanisani, sijui kama kila mkurugenzi angekuwa anafanya hivi kama shughuli za kiofisi zingefanyika. Me namshauri Mkurugenzi Mkuu aangalie yasije kumkuta ya wenzake wa TBS na TANTRADE ambazo zote pamoja na EPZA ni taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda.
Naomba nieleweke kuwa lengo si majungu ndo maana nimeleta takwimu, lengo ni kurekebisha baadhi ya watendaji wakuu wa hizi taasisi zetu za umma wanaodhani kuwa taasisi ni mali zao, huku wakifanya ubadhilifu wa mali za umma na utendaji sifuri. Naomba niachie wanajamvi wengine wachangie then nitarudi baadaye na taarifa nyingine. Mabadiliko ya kweli huanzia JF. Nawasilisha!