MpigaFilimbi
JF-Expert Member
- Apr 30, 2008
- 1,169
- 182
Daniel Mjema, Moshi
MADIWANI watatu wa Baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, wametoa kali ya mwaka baada ya kuchapana makonde wakigombea kuingia kwenye kamati ya mipango miji ya halmashauri hiyo.
Haijafahamika mara moja kamati hiyo ina maslahi gani manono ukilinganisha na kamati nyingine, lakini kamati hiyo ndiyo inasimamia suala la ugawaji viwanja, suala ambalo ni nyeti kwa mkoa Kilimanjaro kutokana na uhaba wa ardhi.
Habari za uhakika zilizopatikana jana zilidokeza kuwa kiini cha kasheshe hilo kilitokana na mmoja wa madiwani wa jinsia ya kiume kutaka diwani mwingine mwenye jinsia ya kike ndiye aingie katika kamati hiyo badala ya diwani mwanaume aliyekuwa akitaka.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilisema kutokana na mvutano huo, diwani mmoja alinyanyuka na kudai diwani mwenzake alikuwa akimfuatafuata na kuamua kumzaba kibao diwani mwenzake.
Habari hizo zilisema kuwa baada ya kuzabwa kibao, diwani huyo alitaharuki na kuamua kujibu mapigo ambapo walianza kutangwana ngumi na mateke, ugomvi ambao ulimkumbwa diwani wa kike ambaye naye alizabwa vibao.
Inaelezwa kuwa madiwani hao wamekuwa wakiingia katika kamati hizo kwa kupokezana lakini mmoja kati ya madiwani hao alikuwa akishinikiza yeye ndiyo apewa fursa hiyo badala ya Diwani wa viti maalumu.
Makamu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Alhaji Omar Shamba alithibitisha kupokea taarifa za vurugu hizo lakini akasema hawezi kuzizungumzia kwa kuwa zilitokea nje ya vikao vya Baraza la Madiwani.
Ni kweli nimezipata hizo habari lakini siwezi kuzizungumzia kwa sababu na mimi nimezipata kama wewe ulivyozipata tunasubiri kama zitaletwa kama malalamiko zitafanyiwa kazi na kamati ya maadilialisema Shamba.
Hata hivyo Alhaji Shamba ambaye pia ni Diwani wa kata ya Njoro kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM) alisema tukio hilo limewadhalilisha madiwani hao ambao kimsingi walipaswa kuwa kioo cha jamii na kuonyesha mfano.
Manispaa ya Moshi inaongozwa na madiwani wa CCM ambao ndio wengi lakini wapo pia madiwani watano kutoka chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA). Madiwani waliotangwana wanatoka moja ya vyama hivyo.
Source: Mwananchi
Kamati hizo zinasababisha watu wazipige, unadhani nini wanakimbilia huko? Fedha za rushwa au posho? Kila mtu alipo anataka kula tu??
MADIWANI watatu wa Baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, wametoa kali ya mwaka baada ya kuchapana makonde wakigombea kuingia kwenye kamati ya mipango miji ya halmashauri hiyo.
Haijafahamika mara moja kamati hiyo ina maslahi gani manono ukilinganisha na kamati nyingine, lakini kamati hiyo ndiyo inasimamia suala la ugawaji viwanja, suala ambalo ni nyeti kwa mkoa Kilimanjaro kutokana na uhaba wa ardhi.
Habari za uhakika zilizopatikana jana zilidokeza kuwa kiini cha kasheshe hilo kilitokana na mmoja wa madiwani wa jinsia ya kiume kutaka diwani mwingine mwenye jinsia ya kike ndiye aingie katika kamati hiyo badala ya diwani mwanaume aliyekuwa akitaka.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilisema kutokana na mvutano huo, diwani mmoja alinyanyuka na kudai diwani mwenzake alikuwa akimfuatafuata na kuamua kumzaba kibao diwani mwenzake.
Habari hizo zilisema kuwa baada ya kuzabwa kibao, diwani huyo alitaharuki na kuamua kujibu mapigo ambapo walianza kutangwana ngumi na mateke, ugomvi ambao ulimkumbwa diwani wa kike ambaye naye alizabwa vibao.
Inaelezwa kuwa madiwani hao wamekuwa wakiingia katika kamati hizo kwa kupokezana lakini mmoja kati ya madiwani hao alikuwa akishinikiza yeye ndiyo apewa fursa hiyo badala ya Diwani wa viti maalumu.
Makamu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Alhaji Omar Shamba alithibitisha kupokea taarifa za vurugu hizo lakini akasema hawezi kuzizungumzia kwa kuwa zilitokea nje ya vikao vya Baraza la Madiwani.
Ni kweli nimezipata hizo habari lakini siwezi kuzizungumzia kwa sababu na mimi nimezipata kama wewe ulivyozipata tunasubiri kama zitaletwa kama malalamiko zitafanyiwa kazi na kamati ya maadilialisema Shamba.
Hata hivyo Alhaji Shamba ambaye pia ni Diwani wa kata ya Njoro kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM) alisema tukio hilo limewadhalilisha madiwani hao ambao kimsingi walipaswa kuwa kioo cha jamii na kuonyesha mfano.
Manispaa ya Moshi inaongozwa na madiwani wa CCM ambao ndio wengi lakini wapo pia madiwani watano kutoka chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA). Madiwani waliotangwana wanatoka moja ya vyama hivyo.
Source: Mwananchi
Kamati hizo zinasababisha watu wazipige, unadhani nini wanakimbilia huko? Fedha za rushwa au posho? Kila mtu alipo anataka kula tu??