Madiwani wateule wa Chadema-Moshi waandamana kwa DED kupinga uonevu.................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Gazeti la Nipashe limeripoti ya kuwa Madiwani wateule wa Chadema wameandamana hadi kwa DED kupinga uonevu ambao Manispaa hiyo ya Moshi imekuwa ikiwaonea wamachinga..................

Nilifikiri sasa siyo wakati tena wakuandamana ila kujiandaa kuanza kuchapa kazi ukizingatia hiyo Manispaa ya Moshi sasa ipo mikononi mwao Chadema na watakuwa na sauti ya turufu juu ya hilo jiji la Moshi litakavyokuwa likiendeshwa.............
 
hivi soko kuu Arusha siku hizi hakuna serikali....wamama wameamua kukaa barabarani kabisa hakuna hata njia ya kupita....ukienda na gari labda ulibebe kichwani....hapo nyuma walikuwa wanaanza kukaa barabarani baada ya ofisi za manispaa kufungwa....siku hizi ni kuanzia saa mbili asubuhi mpaka jioni......ukijaribu kuwatetea inakuwa ngumu maana wanapitiliza sasa....sometimes mgambo wana faida jamani
 
Usafi ni mpango wa mji,watanzania tumezoea kulalamika sana badala ya kutafakari.
Ukiacha watu wakifanya watakalo mjini,watauza hadi vibarazani mwa maduka maana njia zote zimejaa vitumbua,mandazi,mchicha.maembe,ndizi na vinginevyo.
Serikali ndio wapangaji kua hapa pawe soko pale gulio na pale pabaki wazi.Ukiachia tu mji unatapakaa uchafu kisha serikali ikaingia hasara ya kufanya usafi kilasiku,wakati pesa hizo zingeelekezwa katika miradi mingine mfano kuboresha uwezo wa kufanya usafi,kuboresha masoko yetu na magulio.
Hawa wamachingo ndo wachafuzi miji yetu na haohao ndo wakwepa ushuru hodari,sasa kama mnakwepa mnadhani hao waliopewa tenda ya usafi watalipwa nini!
Minaipa hongera manispaa ya Moshi kwa kudumisha usafi na kuwatoza faini wachafuzi wamazingira.
Ieleweke vizuri kua sina negative attitude na wamachinga kwa vile wanatusaidia kupata bidhaa kwa urahisi pia na kwao ni sehemu ya ajira yao,pia natambua kua uwepo wao mtaani kumepunguza wimbi la vibaka.machangudoa na wategemezi katika familia zetu.
Wito wangu kwa serikali nikua halimashauri zitazame maeneo ambayo yanamazingira mazuri ili kuwatengea maeneo yenyefaida siyo alimradi eneo. Kwawamachinga wao pia kama wanamalalamiko wajiunge na kuweka uongozi ili iwe rahisi kuwatetea na pia kuheshimu maamuzi ya serikali kwani wao ndio wanao panga.Zaidi wamachinga wajiunge na kupeleka malalamiko yao panapohusika.
 
hivi soko kuu Arusha siku hizi hakuna serikali....wamama wameamua kukaa barabarani kabisa hakuna hata njia ya kupita....ukienda na gari labda ulibebe kichwani....hapo nyuma walikuwa wanaanza kukaa barabarani baada ya ofisi za manispaa kufungwa....siku hizi ni kuanzia saa mbili asubuhi mpaka jioni......ukijaribu kuwatetea inakuwa ngumu maana wanapitiliza sasa....sometimes mgambo wana faida jamani
Vurugu hii ilianza wakati wa uchaguzi lakini taarifa niliyonayo ni kuwa baada ya uchaguzi kupita basi watawaondoa ....maana kura zao hawazihitaji...........
 
CHADEMA, fanyeni mabadiliko ktk miji ya moshi, mwanza na arusha, ili ccm waone kuwa walikuwa wakifanya pumba ktk hizi halimashauri
 
Pole mami usiende soko kuu kila siku watakuuguza vidonda vya tumbo kwa mawazo, mbona umesahau na wale vijana wauza mifuko wanavyomfuata mtu nyuma kama kawaibia? Au wanavoongoza watu kupark gari kuanzia kule rushda wanavyo bore, mi nadhani wangeanza kushughulikiwa hao kwanza, then wa mama badae, sababu ukitaka veg na fruit nzuri na fresh ni kwa hao wa mama. Nadhani wanahitaji kusaidiwa tu.
 
Pole mami usiende soko kuu kila siku watakuuguza vidonda vya tumbo kwa mawazo, mbona umesahau na wale vijana wauza mifuko wanavyomfuata mtu nyuma kama kawaibia? Au wanavoongoza watu kupark gari kuanzia kule rushda wanavyo bore, mi nadhani wangeanza kushughulikiwa hao kwanza, then wa mama badae, sababu ukitaka veg na fruit nzuri na fresh ni kwa hao wa mama. Nadhani wanahitaji kusaidiwa tu.

tule tutoto na twenyewe ni moja ya kero....vingine vinatakiwa viwe shule lakini ndio kwanza viko sokoni vikifanya biashara na wizi.....hope halmashauri ya jiji itashughulikia hili
 
Mwanza kwa issue ya wa machinga wamejitahidi kidogo waliwatimua wote maeneo husika, pia hata mikoko10 hairuhusiwi kabisa kukatiza maeneo ya town.
 
CHADEMA, fanyeni mabadiliko ktk miji ya moshi, mwanza na arusha, ili ccm waone kuwa walikuwa wakifanya pumba ktk hizi halimashauri
Hata mbeya itakua chini ya chadema kwa sababu itapata viti maalum vingi kuliko ccm
 
Back
Top Bottom