Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Je hawa ipp hawajui kuwa huyu Bwana alijiuzuru sio kustaafu na Hapo chini pekundu huyu jamaa alikuwa ana maanisha nini?
Madiwani, wabunge badilisheni maisha ya wananchi-Lowassa
Na Cynthia Mwilolezi
5th January 2011
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, ametoa wito kwa wabunge na madiwani waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu liliofanyika mwaka uliopita, kuhakikisha kuwa wanafanya kila liwezekanalo kubadilishahali ya maisha ya wananchi wao kiuchumi.
Kadhalika, amewataka viongozi hao kuweka kipaumbele katika kujali maslahi ya wapigakura wao, ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wakuwakopesha, ili waweze kuanzisha miradi ya kujikwamua kiuchumi, kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi wengi nchini.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Manyire,Kata ya Mlangarini, wilayani Arumeru, alipokuwa akizungumza katika sherehe za kuwapongeza na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua Diwani wao, Mathias Manga (CCM).
"Wakati umefika kwa viongozi katika maeneo mbalimbali hapa nchini kubadilika na kuacha tabia na mazoea ya kujinufaisha wao wenyewe na familia na jamaa zao na kuhakikisha kuwa wanajikita zaidi kuwatumikia wananchi hususani kujali wanakula nini," alisema Lowassa.
Pia, Lowasa alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uamuzi wake wa kukubali mabadiliko ya katiba na kutoa wito kwa wananchi, kuhakikisha kuwa wakati ukifika wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao.
"Rais wetu hakusubiri wananchi waandamane na ndio maana kaamua kutangaza rasmi kuunda tume ya kurekebisha katiba, naomba wakati ukifika wananchi wengi jitokezeni na zoezi hilo lifanyike kwa amani na Utulivu," alisema Lowassa.
Ama kwa upande wake, Diwani Manga aliwashukuru wananchi wa kata yake kwa kumchagua na kusema kuwa hawakukosea na atawalipa kwa utendaji wake kwa kuhakikisha kuwa anajitahidi kutatua kero sugu ambazo zimekuwa zikiwakabili kwa muda mrefu.
"Nawaahidi hakuna mtoto hata mmoja katika kata yangu ambaye atashindwa kusoma sekondari kutokana na kukosa ada, nitajitahidi sana kwa hilo kwani hakuna urithi mzuri kama elimu," alisema Diwani Manga.
CHANZO: NIPASHE
Hapo pekundu huyu jamaa alikuwa ana maanisha nini?
Madiwani, wabunge badilisheni maisha ya wananchi-Lowassa
Na Cynthia Mwilolezi
5th January 2011
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, ametoa wito kwa wabunge na madiwani waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu liliofanyika mwaka uliopita, kuhakikisha kuwa wanafanya kila liwezekanalo kubadilishahali ya maisha ya wananchi wao kiuchumi.
Kadhalika, amewataka viongozi hao kuweka kipaumbele katika kujali maslahi ya wapigakura wao, ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wakuwakopesha, ili waweze kuanzisha miradi ya kujikwamua kiuchumi, kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi wengi nchini.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Manyire,Kata ya Mlangarini, wilayani Arumeru, alipokuwa akizungumza katika sherehe za kuwapongeza na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua Diwani wao, Mathias Manga (CCM).
"Wakati umefika kwa viongozi katika maeneo mbalimbali hapa nchini kubadilika na kuacha tabia na mazoea ya kujinufaisha wao wenyewe na familia na jamaa zao na kuhakikisha kuwa wanajikita zaidi kuwatumikia wananchi hususani kujali wanakula nini," alisema Lowassa.
Pia, Lowasa alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uamuzi wake wa kukubali mabadiliko ya katiba na kutoa wito kwa wananchi, kuhakikisha kuwa wakati ukifika wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao.
"Rais wetu hakusubiri wananchi waandamane na ndio maana kaamua kutangaza rasmi kuunda tume ya kurekebisha katiba, naomba wakati ukifika wananchi wengi jitokezeni na zoezi hilo lifanyike kwa amani na Utulivu," alisema Lowassa.
Ama kwa upande wake, Diwani Manga aliwashukuru wananchi wa kata yake kwa kumchagua na kusema kuwa hawakukosea na atawalipa kwa utendaji wake kwa kuhakikisha kuwa anajitahidi kutatua kero sugu ambazo zimekuwa zikiwakabili kwa muda mrefu.
"Nawaahidi hakuna mtoto hata mmoja katika kata yangu ambaye atashindwa kusoma sekondari kutokana na kukosa ada, nitajitahidi sana kwa hilo kwani hakuna urithi mzuri kama elimu," alisema Diwani Manga.
CHANZO: NIPASHE
Hapo pekundu huyu jamaa alikuwa ana maanisha nini?