Madiwani wa CHADEMA Arusha na strategic plan ya kukusanya mapato ya Halmashauri ya jiji

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
Kabla ya uchaguzi wa July 14 2013 madiwani wa CHADEMA walikuwa wachache, na fedha za halmashauri zilikuwa hazijulikani zinakokwenda.
Baada ya uchaguzi wa July 14 2013, Madiwani wa CHADEMA waliwazidi wale wa CCM, wakaanza kufanya utafiti ambao baadhi yao walishaufanya.
Madiwani wa CHADEMA waligundua kuna sources nyingi za kukusanya mapato tofauti na wamama ambao wanateseka kuuza nyanya sokoni ambao wanalipa ushuru na fedha zinaingia kwenye mifuko ya CCM.
Madiwani wa CHADEMA wakaanza kupanga mpango mkakati wa kuhakikisha hoteli za kitalii, wafanyabiashara wakubwa hapa mjini pamoja na mabango ya biashara wanalipa kodi inavyotakiwa.

Baada ya Uchaguzi wa Naibu Meya ndiyo kwanza kazi imeanza ya kuhakikisha wafanyabiashara wote ambao hawalipi kodi, ambao CCM kupitia kwa madiwani wao wasiotumia akili kwa kufikiri wamewasamehe wasilipe kodi wanalipa kodi.

Wananchi tumegundua baada ya CHADEMA kuwa wenye maamuzi kwenye halmashauri mapato ya Halmashauri ya Jiji yameongezeka kwa Milioni zaidi 700 kwa mwezi.

Hapa ndipo tunapotambua thamani ya ubabe wa Lema kutetea maslahi ya wanyonge ambao walikuwa wamesahauliwa kwa muda mrefu, wanyonge ambao muda mrefu wamekuwa mtaji wa ccm huku wafanyabiashara wakubwa wakisamehemwa kulipa kodi.

Madiwani wa CHADEMA kwenye baadhi ya Halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA wananifanya niamini kuwa CHADEMA sasa ina kila sababu ya kuchukua dola ili wawatumikie watanzania walio wengi.
CCM imechoka, haina mawazo mapya ya kuwatumikia watanzania.

2015 kwa CHADEMA
 
Hapa sasa ndio muda wa mauaji ya wale panya wenye mvi wanaokula pesa za halmashauri. Tumechoka na hati chafu kutoka kwa CAG every year. Muda ndio sasa wa kuonesha kodi zinakokwenda.

Big up madiwani wa CHADEMA.
 
Back
Top Bottom