Nyota Njema
Senior Member
- Nov 18, 2010
- 148
- 16
Wadau, sisi tuliokuwepo kwenye mkutano wa hadhara wa Dr. Slaa pale Sengerema tulijulishwa na wadau kuwa madiwani wote wa CCM walikuwa wamefungiwa ndani ili wasihudhurie mkutano wa hadhara wa Dr. Slaa kwa hofu kuwa huenda na wao wangelirudisha kadi za chama chao na kujiunga na CDM kama alivyofanya mwezao ndugu Tabasamu. Hofu hii ilitokana na ukweli kuwa diwani Tabasamu alikuwa aeleze jinsi ambavyo fedha nyingi za Halmashauri ya Sengerema zilivyofujwa na uongozi wa halmashauri hiyo huku documents muhimu za wizi huo zikifichwa.
Akielezea tukio la wizi huo, mheshimiwa Tabasamu aliueleza umati mkubwa uliohudhuria mkutano huo wa hadhara kuwa hata yeye asingelijua ni nini kilichofanyika katika kuficha uozo huo mpaka pale alipozipata nyaraka za mkaguzi wa serikali wa hesabu za halmashauri hiyo kupitia vyanzo mbalimbali kwa msaada wa ndugu Godbless Lema na vyanzo vinginevyo. Tukio hilo la kuwafungia madiwani hao pia lililenga kuwaficha madiwani hao juu ya uozo huo ingawa kwa sasa sio siri tena na huenda suala hili likaendelea kuitafuna CCM ndani ya Wilaya hiyo anakotoka Waziri wa Nishati na madini, ndugu Wiliam Gereja.
Hata hivyo suala hilo lilikuwa limeshaelezwa na mheshimiwa Tabasamu katika mkutano wa hadhara uliotangulia katika mkoa mpya wa Geita, na huenda jambo hilo ndilo lililoufanya uongozi wa CCM wilaya ya Sengerema kuwafungia madiwani wake katika mkutano uliofanyika katika Wilaya yao.
Mkutano huo uliofanyika huku mvua ikinyesha, ulishudia hujuma iliyotaka kufanywa na viongozi wasio waaminifu ndani ya CDM jimbo la Sengerema katika muendelezo wa hujuma za Ngereja pale tulipokuta hakuna viti wala vyombo vya kupazia sauti jambo lililolazimu kutumika kwa vyombo vilivyokuwepo kwenye gari ya msafara wa Dr. Slaa.
Katibu wa CDM mkoa wa Mwanza aliweza kuinusuru hali hiyo pale alipofanya juhudi iliyozaa matuma kwa kutafuta vifaa hivyo na hivyo mkutano kupata usikivu mzuri kama ilivyotarajiwa. Akihutubia umati huo mkubwa, Dr. Slaa aliwaahidi wapenzi wote wa CDM kuwa angeliwachukulia hatua viongozi wote ndani ya Wilaya na Jimbo hilo waliohusika na hujuma hiyo, ikiwa ni pamoja na tuhuma nyinginezo ambazo zilikuwa zimeshawasilishwa kwenye ofisi yake pamoja na ushahidi uliokuwa utolewe kwenye mkutano wa ndani uliofanyika baada ya mkutano huo wa hadhara.
Habari zilizopatika baadaye kutoka kwenye kikao cha ndani ni kuwa uongozi wote wa jimbo pamoja na baraza la mashauriano la Wilaya ya Sengerema walisimamishwa kazi na hivyo kuundwa uongozi wa muda wa watu wanne kulisimamia jimbo la Sengerema mpaka pale uongozi mpya utakapochaguliwa katika vikaao vya kikatiba vitakavyokaa hapo baadaye.
Katika mikutano yote ya ndani na nje Dr. Slaa alizungumzia suala la kukisafisha chama katika harakati za kukiandaa kuchukua madaraka ya nchi ifikapo mwaka 2015. Alinukuliwa akisema kuwa, alipokuwa akigombea nafasi ya urais wa nchi aliahidi kuusafisha uozo wote uliopo serikalini, hivyo katika kuonyesha kuwa alikuwa anamaanisha hivyo, ameamua kufanya usafi huo ndani ya chama chake pia akiamini kuwa hawezi kuwa na serikali safi kama hana chama kisafi. Katika kutimiza azima hiyo, pamoja na kuuvua madaraka uongozi wa Wilaya na Jimbo la Sengerema, lakini pia alisimamia kumvua uanachama Mwenyekiti wa Wilaya ya Geita ambaye pia ndiye diwani wa Katoro ndugu Gervas Daudi, uongozi wa vijana wa Wilaya na Jimbo la Geita, pamoja na kuwavua uanachama baadhi ya viongozi hao wa vijana. Tukio jingine lilikuwa ni kumpa onyo kali diwani mmoja wa viti maalum ndani ya jimbo la Geita kwa kitendo chake cha kushiriki katika vurugu zilizokuwa zikiendeshwa na vijana hao kwa lengo la kukidhohofisha chama.
Akielezea tukio la wizi huo, mheshimiwa Tabasamu aliueleza umati mkubwa uliohudhuria mkutano huo wa hadhara kuwa hata yeye asingelijua ni nini kilichofanyika katika kuficha uozo huo mpaka pale alipozipata nyaraka za mkaguzi wa serikali wa hesabu za halmashauri hiyo kupitia vyanzo mbalimbali kwa msaada wa ndugu Godbless Lema na vyanzo vinginevyo. Tukio hilo la kuwafungia madiwani hao pia lililenga kuwaficha madiwani hao juu ya uozo huo ingawa kwa sasa sio siri tena na huenda suala hili likaendelea kuitafuna CCM ndani ya Wilaya hiyo anakotoka Waziri wa Nishati na madini, ndugu Wiliam Gereja.
Hata hivyo suala hilo lilikuwa limeshaelezwa na mheshimiwa Tabasamu katika mkutano wa hadhara uliotangulia katika mkoa mpya wa Geita, na huenda jambo hilo ndilo lililoufanya uongozi wa CCM wilaya ya Sengerema kuwafungia madiwani wake katika mkutano uliofanyika katika Wilaya yao.
Mkutano huo uliofanyika huku mvua ikinyesha, ulishudia hujuma iliyotaka kufanywa na viongozi wasio waaminifu ndani ya CDM jimbo la Sengerema katika muendelezo wa hujuma za Ngereja pale tulipokuta hakuna viti wala vyombo vya kupazia sauti jambo lililolazimu kutumika kwa vyombo vilivyokuwepo kwenye gari ya msafara wa Dr. Slaa.
Katibu wa CDM mkoa wa Mwanza aliweza kuinusuru hali hiyo pale alipofanya juhudi iliyozaa matuma kwa kutafuta vifaa hivyo na hivyo mkutano kupata usikivu mzuri kama ilivyotarajiwa. Akihutubia umati huo mkubwa, Dr. Slaa aliwaahidi wapenzi wote wa CDM kuwa angeliwachukulia hatua viongozi wote ndani ya Wilaya na Jimbo hilo waliohusika na hujuma hiyo, ikiwa ni pamoja na tuhuma nyinginezo ambazo zilikuwa zimeshawasilishwa kwenye ofisi yake pamoja na ushahidi uliokuwa utolewe kwenye mkutano wa ndani uliofanyika baada ya mkutano huo wa hadhara.
Habari zilizopatika baadaye kutoka kwenye kikao cha ndani ni kuwa uongozi wote wa jimbo pamoja na baraza la mashauriano la Wilaya ya Sengerema walisimamishwa kazi na hivyo kuundwa uongozi wa muda wa watu wanne kulisimamia jimbo la Sengerema mpaka pale uongozi mpya utakapochaguliwa katika vikaao vya kikatiba vitakavyokaa hapo baadaye.
Katika mikutano yote ya ndani na nje Dr. Slaa alizungumzia suala la kukisafisha chama katika harakati za kukiandaa kuchukua madaraka ya nchi ifikapo mwaka 2015. Alinukuliwa akisema kuwa, alipokuwa akigombea nafasi ya urais wa nchi aliahidi kuusafisha uozo wote uliopo serikalini, hivyo katika kuonyesha kuwa alikuwa anamaanisha hivyo, ameamua kufanya usafi huo ndani ya chama chake pia akiamini kuwa hawezi kuwa na serikali safi kama hana chama kisafi. Katika kutimiza azima hiyo, pamoja na kuuvua madaraka uongozi wa Wilaya na Jimbo la Sengerema, lakini pia alisimamia kumvua uanachama Mwenyekiti wa Wilaya ya Geita ambaye pia ndiye diwani wa Katoro ndugu Gervas Daudi, uongozi wa vijana wa Wilaya na Jimbo la Geita, pamoja na kuwavua uanachama baadhi ya viongozi hao wa vijana. Tukio jingine lilikuwa ni kumpa onyo kali diwani mmoja wa viti maalum ndani ya jimbo la Geita kwa kitendo chake cha kushiriki katika vurugu zilizokuwa zikiendeshwa na vijana hao kwa lengo la kukidhohofisha chama.