Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,979
Lipo zoezi lililoendeshwa na Dkt. Bashiru na Polepole kwa udhamini wa mwenyekiti lililopewa jina la kuunga juhudi mkono. Zoezi lile lilijaa uhalifu ikiwemo matumizi ya vitisho kwa waliokataa kuunga juhudi mkono.
Moja ya zawadi waliyopewa wale waliounga mkono juhudi ilikuwa ni kuakikishiwa usalama wao, kulipwa maslahi yote hata Yale yaliyopaswa kulipwa kwa wabunge na madiwani walifanikisha kufika mwisho wa miaka mitano wakiwa kwenye nafasi.
Watu walipewa pia mitaji yakuwawezesha kujitegemea na baadhi walipewa nafasi za utawala kama takrima.
Hoja yangu, kwanini usifanyike ukaguzi maalumu kuhusu kundi hili lililopelekea Kodi za wananchi kutumika kurudia uchaguzi lakini Kodi hizo hizo kutumika kuwalipa mafao na takrima mbalimbali?
Moja ya zawadi waliyopewa wale waliounga mkono juhudi ilikuwa ni kuakikishiwa usalama wao, kulipwa maslahi yote hata Yale yaliyopaswa kulipwa kwa wabunge na madiwani walifanikisha kufika mwisho wa miaka mitano wakiwa kwenye nafasi.
Watu walipewa pia mitaji yakuwawezesha kujitegemea na baadhi walipewa nafasi za utawala kama takrima.
Hoja yangu, kwanini usifanyike ukaguzi maalumu kuhusu kundi hili lililopelekea Kodi za wananchi kutumika kurudia uchaguzi lakini Kodi hizo hizo kutumika kuwalipa mafao na takrima mbalimbali?