Madirisha ya udahili TCU na mkopo HESLB yamefunguliwa: Je, JKT itawaruhusu vijana walio makambini kurudi kupeleka maombi?

Masiya

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
7,578
7,281
Kichwa cha uzi kinajieleza. Hadi leo sijaona dalili za vijana kupewa muda wa kurudi nyumbani ili wa process maombi yao kwa kushirikiana na familia zao. Miaka iliyopita nini kilifanyika?
 
Kichwa cha uzi kinajieleza. Hadi leo sijaona dalili za vijana kupewa muda wa kurudi nyumbani ili wa process maombi yao kwa kushirikiana na familia zao. Miaka iliyopita nini kilifanyika?
Huwa wanaruhusiwa wakaaply.
 
Kichwa cha uzi kinajieleza. Hadi leo sijaona dalili za vijana kupewa muda wa kurudi nyumbani ili wa process maombi yao kwa kushirikiana na familia zao. Miaka iliyopita nini kilifanyika?
Sikuhizi vijana wanaombea uko uko kama ana details zote na maombi yanatumwa na jeshi kupunguza usumbufu
 
Sikuhizi vijana wanaombea uko uko kama ana details zote na maombi yanatumwa na jeshi kupunguza usumbufu
Tatizo wengi hawana uelewa wa kutosha na wanahitaji ushauri vinginevyo wataishia kuchagua programs ambazo hawana uhakika nazo. Hapa wanafanya maamuzi ambayo itabidi wayaishi maisha yao yote na sidhani kama kambini kuna mazingira wezeshi kwa maamuzi hayo.
 
Tatizo wengi hawana uelewa wa kutosha na wanahitaji ushauri vinginevyo wataishia kuchagua programs ambazo hawana uhakika nazo. Hapa wanafanya maamuzi ambayo itabidi wayaishi maisha yao yote na sidhani kama kambini kuna mazingira wezeshi kwa maamuzi hayo.
Wawakilishi wa bodi ya mikopo pia tcu huwa wanapita kila kambi kutoa elimu kwa kuruti
 
Sisi mwaka jana hatukupewa ruhusa ya kurudi...bali waliturudishia simu zetu tutume taarifa ya Vyuo na kozi tunazozitaka kwa watu au ndugu waliopo nyumbani watufanyie admission.
 
Sisi mwaka jana hatukupewa ruhusa ya kurudi...bali waliturudishia simu zetu tutume taarifa ya Vyuo na kozi tunazozitaka kwa watu au ndugu waliopo nyumbani watufanyie admission.
Bado naamini kushiriki kwa familia kwa ukaribu ni kitu muhimu. Kuna strategies za kuchagua chuo sio ťu chuo ukipendacho bali ufaulu wako ukoje na ushindani umekaaje. Sio wote wanao omba mkopo watapata hivyo wazazi wanatakiwa wajipange. Mwishowe muombaji ndio anatakiwa ajaze na si mtu mwingine. Sisi wengine tushauri na kusaidia na sio kuchukua jukumu la kujaza. Vinginevyo tuwe tayari kubeba lawama. JKT wasiangalie upande wao tu bali wawaweke vijana mbele.
 
Back
Top Bottom