Madikteta wa Familia tunaweza kudai Demokrasia?

Status
Not open for further replies.

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
ctb5.png

Naomba kujenga hoja kwamba ili tuweze kujenga uhalali wa kudai demokrasia ni muhimu sisi wenyewe tuoneshe mfano wa kuwa wanademokrasia kweli. Ninatumia dhana kwamba, mara zote, utawala wa nchi ni sura halisi ya utamaduni wa wananchi wake. Kwamba viongozi/watawala wa nchi hubeba tabia/ na hulka za jamii wanazoziongoza.

Haiwezekani kutarajia watawala wawe tofauti na wananchi wanaowaongoza kwa sababu utawala wa nchi huzaliwa na wananchi. Ndio maana, kwa mfano, wananchi wanaothamini elimu, hutafuta na kuchagua miongoni mwao viongozi wanaothamini elimu kama wao. Kinyume chake, wananchi wasiothamini elimu (wajinga) huweza, na kwa kweli hufurahia, kuchagua wajinga wenzao kuwa watawala wao. Kadhalika, wananchi wanaopenda njia za mkato kujipatia kipato, huthamini wenzao wajanja wenye kujua kutafuta fedha kirahisi na hatima yake wananchi hawa hujichagulia viongozi wanaokuja baadae kufahamika kama mafisadi. Ndio kusema viongozi hawawezi kuwa tofauti na wananchi.

Tukizitazama nchi zinazosifika kwa demokrasia tunabaini kuwa demokrasia katika nchi hizo ni utamaduni wa wananchi. Demokrasia ni maisha/mila inayoanza kwenye utawala wa familia. Kila mwanafamilia kwa kiasi kikubwa anajengewa mazingira ya kujisikia kuwa na uhuru wa maoni. Mtoto hupewa nafasi ya kufanya maamuzi kwa mwongozo wa mzazi. Mke hupewa fursa ya kushiriki katika maamuzi anayoyafanya mumewe kwa sababu demokrasia katika jamii hizo ni utamaduni unaoanzia kwenye familia na sio matamanio hewa ya kisiasa.

Ninapofikiria madai yetu haya ya kutaka watawala wetu wawe wana-demokrasia, maswali kadhaa yanajitokeza. Ninajiuliza, kwa mfano, tunaweza kweli kudai kuwa sisi ni jamii inayoamini katika demokrasia kuanzia ngazi ya familia? Je, demokrasia ni utamaduni wetu?

Je, sisi wanaume wa ki-Afrika hatutishwi na kukua kwa demokrasia kwenye ngazi ya familia zetu? Tunawashirikisha kweli wake zetu katika maamuzi bila kuwawekea mipaka? Tunaheshimu maoni ya watoto wetu kama tunavyotaka watawala wetu waheshimu maoni yetu? Ni lini kwa mfano wazazi hukaa na watoto wao kujadili bajeti ya familia?

Wanaume ili tuweze kujenga taifa linaloamini uhuru wa mawazo kweli kweli, tuanze kujenga demokrasia ya kweli ndani ya familia zetu

Tuanze kuwashirikisha wake zetu katika maamuzi bila kuogopa kuonekana 'tumeshikiliwa'. Tuanze kuthamini na kuheshimu maoni/mahitaji ya Watoto wetu na kuyasikiliza
 
Naomba kujenga hoja kwamba ili tuweze kujenga uhalali wa kudai demokrasia ni muhimu sisi wenyewe tuoneshe mfano wa kuwa wanademokrasia kweli. Ninatumia dhana kwamba, mara zote, utawala wa nchi ni sura halisi ya utamaduni wa wananchi wake. Kwamba viongozi/watawala wa nchi hubeba tabia/ na hulka za jamii wanazoziongoza.

Haiwezekani kutarajia watawala wawe tofauti na wananchi wanaowaongoza kwa sababu utawala wa nchi huzaliwa na wananchi. Ndio maana, kwa mfano, wananchi wanaothamini elimu, hutafuta na kuchagua miongoni mwao viongozi wanaothamini elimu kama wao. Kinyume chake, wananchi wasiothamini elimu (wajinga) huweza, na kwa kweli hufurahia, kuchagua wajinga wenzao kuwa watawala wao. Kadhalika, wananchi wanaopenda njia za mkato kujipatia kipato, huthamini wenzao wajanja wenye kujua kutafuta fedha kirahisi na hatima yake wananchi hawa hujichagulia viongozi wanaokuja baadae kufahamika kama mafisadi. Ndio kusema viongozi hawawezi kuwa tofauti na wananchi.

Tukizitazama nchi zinazosifika kwa demokrasia tunabaini kuwa demokrasia katika nchi hizo ni utamaduni wa wananchi. Demokrasia ni maisha/mila inayoanza kwenye utawala wa familia. Kila mwanafamilia kwa kiasi kikubwa anajengewa mazingira ya kujisikia kuwa na uhuru wa maoni. Mtoto hupewa nafasi ya kufanya maamuzi kwa mwongozo wa mzazi. Mke hupewa fursa ya kushiriki katika maamuzi anayoyafanya mumewe kwa sababu demokrasia katika jamii hizo ni utamaduni unaoanzia kwenye familia na sio matamanio hewa ya kisiasa.

Ninapofikiria madai yetu haya ya kutaka watawala wetu wawe wana-demokrasia, maswali kadhaa yanajitokeza. Ninajiuliza, kwa mfano, tunaweza kweli kudai kuwa sisi ni jamii inayoamini katika demokrasia kuanzia ngazi ya familia? Je, demokrasia ni utamaduni wetu?

Je, sisi wanaume wa ki-Afrika hatutishwi na kukua kwa demokrasia kwenye ngazi ya familia zetu? Tunawashirikisha kweli wake zetu katika maamuzi bila kuwawekea mipaka? Tunaheshimu maoni ya watoto wetu kama tunavyotaka watawala wetu waheshimu maoni yetu? Ni lini kwa mfano wazazi hukaa na watoto wao kujadili bajeti ya familia?

Wanaume ili tuweze kujenga taifa linaloamini uhuru wa mawazo kweli kweli, tuanze kujenga demokrasia ya kweli ndani ya familia zetu

Tuanze kuwashirikisha wake zetu katika maamuzi bila kuogopa kuonekana 'tumeshikiliwa'. Tuanze kuthamini na kuheshimu maoni/mahitaji ya Watoto wetu na kuyasikiliza
Bira mzee umeongea vizur
 
Wazo zuri, tukifanikiwa kuwa na familia zisizo na udikteta means tutajenga na kukuza jamii yenye misingi ya kidemokrasia.. Changamoto ni utamaduni wetu.
 

Naomba kujenga hoja kwamba ili tuweze kujenga uhalali wa kudai demokrasia ni muhimu sisi wenyewe tuoneshe mfano wa kuwa wanademokrasia kweli. Ninatumia dhana kwamba, mara zote, utawala wa nchi ni sura halisi ya utamaduni wa wananchi wake. Kwamba viongozi/watawala wa nchi hubeba tabia/ na hulka za jamii wanazoziongoza.

Haiwezekani kutarajia watawala wawe tofauti na wananchi wanaowaongoza kwa sababu utawala wa nchi huzaliwa na wananchi. Ndio maana, kwa mfano, wananchi wanaothamini elimu, hutafuta na kuchagua miongoni mwao viongozi wanaothamini elimu kama wao. Kinyume chake, wananchi wasiothamini elimu (wajinga) huweza, na kwa kweli hufurahia, kuchagua wajinga wenzao kuwa watawala wao. Kadhalika, wananchi wanaopenda njia za mkato kujipatia kipato, huthamini wenzao wajanja wenye kujua kutafuta fedha kirahisi na hatima yake wananchi hawa hujichagulia viongozi wanaokuja baadae kufahamika kama mafisadi. Ndio kusema viongozi hawawezi kuwa tofauti na wananchi.

Tukizitazama nchi zinazosifika kwa demokrasia tunabaini kuwa demokrasia katika nchi hizo ni utamaduni wa wananchi. Demokrasia ni maisha/mila inayoanza kwenye utawala wa familia. Kila mwanafamilia kwa kiasi kikubwa anajengewa mazingira ya kujisikia kuwa na uhuru wa maoni. Mtoto hupewa nafasi ya kufanya maamuzi kwa mwongozo wa mzazi. Mke hupewa fursa ya kushiriki katika maamuzi anayoyafanya mumewe kwa sababu demokrasia katika jamii hizo ni utamaduni unaoanzia kwenye familia na sio matamanio hewa ya kisiasa.

Ninapofikiria madai yetu haya ya kutaka watawala wetu wawe wana-demokrasia, maswali kadhaa yanajitokeza. Ninajiuliza, kwa mfano, tunaweza kweli kudai kuwa sisi ni jamii inayoamini katika demokrasia kuanzia ngazi ya familia? Je, demokrasia ni utamaduni wetu?

Je, sisi wanaume wa ki-Afrika hatutishwi na kukua kwa demokrasia kwenye ngazi ya familia zetu? Tunawashirikisha kweli wake zetu katika maamuzi bila kuwawekea mipaka? Tunaheshimu maoni ya watoto wetu kama tunavyotaka watawala wetu waheshimu maoni yetu? Ni lini kwa mfano wazazi hukaa na watoto wao kujadili bajeti ya familia?

Wanaume ili tuweze kujenga taifa linaloamini uhuru wa mawazo kweli kweli, tuanze kujenga demokrasia ya kweli ndani ya familia zetu

Tuanze kuwashirikisha wake zetu katika maamuzi bila kuogopa kuonekana 'tumeshikiliwa'. Tuanze kuthamini na kuheshimu maoni/mahitaji ya Watoto wetu na kuyasikiliza
Umeongea vizur mnooo rafiki angu napenda sana kupata hata namba ya alie andika andiko hili nataman kukaa na watu wenye akili kubwa
 
ndoa nyingi zinavunjika siku hizi sababu ya kuleta democrasia
ukiwa na democrasia wenzetu wa upande wa pili wanakuchukulia wewe ni bwege
 
...Tuanze kuwashirikisha wake zetu katika maamuzi bila kuogopa kuonekana 'tumeshikiliwa'. Tuanze kuthamini na kuheshimu maoni/mahitaji ya Watoto wetu na kuyasikiliza
Mkuu, demokrasia inategemea mambo mengi, unaeza kuwa 'democratic' kwa baadhi ya mambo, kwa mengine ukawa kama jiwe (hupangiwi na mtu, unaamua mwenyewe tu)..

Mfano, kama wife ni mwenyeji wa Pwani, ukimwachia akili "akushikie", kila siku atakesha kwny ngoma, muda si mrefu utashangaa huna mke tena!!!
 
Asilimia kubwa ya nyumba nyingi, decision hufanywa na kina mama. Wanaume wengi kabla ya kuoa huaga mawazo ya kujenga nyumba ni kama hua hayapo kiviiile, subiri mama mwenye nyumba aingie sasa, utasikia habari za utafutaji wa viwanja inavyokua. Kuna uzi humu, nadhani na twitter upo, kuna mtu aliandika hivi, "Nilipokua kwa wazazi, niliwachukia sana wazazi wangu kwa kunilazimisha kurudi nyumbani mapema, nikajipa hope nikianza maisha nitakua narudi home muda ninao utaka, shit; baada ya kuoa ndio imekua more worse" mchangiaji mmoja akaandika hivi, "huku kwa wake zetu sasa ndio noma, mtu unaogopa hadi kurudi kwako"

Nimesikia kwenye matamko ya wanawake (niliisikia Kenya na sasa Bongo tena, juzi tu hapo wakati wa siku ya kina mama )kwamba eti, "vitabu vya dini vinasema, mwanaume ni kichwa cha nyumba" sasa na sisi wanawake ndio shingo, shingo ndio inayoigeuza kichwa itakavyo.
Mwisho namalizia, kwa vijana ambao bado wanakaa na watu ambao sio wazazi wao, ukitaka kuishi muda mrefu kwenye hiyo nyumba, jitahidi unavyoweza, patana na mama mwenye nyumba, baba mwenye nyumba itakuja auto (ushauri wangu mimi kama mzee), again wanaume wenzangu (watu wazima wenye 40+ years ) kwanini mwanaume anaweza kuzaa nje ya ndoa but akashindwa kumleta mwanae kwenye nyumba alijenga mwenyewe but wapo wanawake wamebebeshwa mimba nje na huyo mtoto akaishi na kulelewa kwenye nyumba yako? May be hiyo ni kama udhalilishaji, inaweza isipate sana uungwaji mkono humu, weka hivi, kabla hujaoa may be ulipata mtoto kwa mwanamke ambaye hukumuoa, kwanini hua ngumu sana kumleta kwako akaishi na huyu mama mpya but ni rahisi sana mama aliyekwisha kuzaa akaishi na mtoto wake kwenye nyumba ya baba ambaye sio baba yake? Kama kwenye maswali yangu yote haya naungwa mkono, then sio kweli kwamba eti majumbani kwetu hakuna demokrasia, kina mama ndio waamuzi wa mambo mengi sana majumbani mwetu, ndio wanao amua tule na kunywa nini!
 
Naelewa concern yako, ila sio kila mahala ulete demokrasia, kuna muda wa kufanya maamuzi magumu na sahihi kwa manufaa ya familia.
 
Status
Not open for further replies.
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom