Madiba kama Nyerere alimuona JK kama mtu ambaye bado anakua, haya mapya

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Tumezoea kusema yale ambayo Nyerere alimwambia JK wakati akigombea urais 1995, moja wapo ni kuwa bado mdogo asubiri, katika hali ya ajabu watu tukiwa tunakuna vichwa kuwa alikuwa mdogo vipi wakati umri kikatiba ulitimia, leo JK katoa siri nyingine nzito kuhusu Mzee Madiba.

Mzee madiba akiwa mcheshi kwa maneno ya JK, wakati JK alifuatilia kurejeshea viatu vyake alivyovicha kwa mhazina wa CCM wa enzi hizo na baadaye waziri wa mipango, somebody Swai. Madiba alikutana na JK mara kadhaa ndipo akaamua kufunguka. Madiba alimwambia JK mbona unaendelea kukua kwa maana ya kimo??? JK akajibu kama sayansi inaruhusu mtu wa miaka 45 akuendelee kukua kwa kimo basi itakuwa hivyo.

Hapa naona JK aliingia kichwa kichwa mtego wa Madiba, wa kutumia fahisi kufikisha ujumbe, JK kweli hadi anasimulia leo anaamini mZee Madiba alinotisi JK kuendelea kurefuka kimo kitu ambacho kama n kweli basi madiba atakuwaa mjingaaa mno.

Siamini madiba alisema juu ya kimo, nafahamu alijua JK alikuwa anafanya utoto mwingi ktk mambo ya msingi, ama alimuona anapelea sana kiasi kwamba anahitaji kukua kimaarifa , akili na uwezo na wala sio kimo chake.

Tukumbuke Madiba ni mwandishi wa vitabu, lazima tu tafsida na fasihii ilitumika.

Cha msingi hapa ni ukweli kuwa Madiba aliona na kusema kile kile Nyerere alisema kwa staili yake. JK bado anakua????? Mkuu utaacha lini kukua???

Nawasilisha
 
Hilo ndo swali langu, je kukua ukiwa 45yrs ni sifa au kitu gani hicho Madiba alimwambia JK???
 
Watetezi watakuvamia kama vipanga,tubiri matusi ya Lumumba ingawa ulichoandika nadhani ndiousahihi wenyewe.
 
Back
Top Bottom