Madhira yanayowakuta Wanafunzi Shule Sekondari Mnyambe, Newala

dimango

New Member
Jul 7, 2022
3
1
Ni siku nyingi mambo ambayo Wazazi wenye Watoto wao wanaosoma katika shule ya SEKONDARI Mnyambe Wilayani Newala wamekuwa wakisikitishwa nayo na si Wazazi pekee bali jamii kwa ujumla haielewi kwanini hali hii imekuwa ikiendelea kwani Wanafunzi wamefanya Kazi za kuchimba msingi, kubeba tofali,kuchimba kisima ambacho nusura kutokee maafa kwa Mwanafunzi mmoja kama suruali yake isingedakwa na kipande kigumu ambacho kilitokeza na Kazi ingine ni kuchota mchanga kwa kutumia mikono ambayo haina kinga yoyote maana kwenye sehemu ambazo Wanafunzi hao wanalazimika kuzoa mchanga huo ni mifereji/ mitaro ambayo inabeba taka mbali mbali ikiwamo Watu kujisaidia humo haja kubwa na ndogo, na humo humo na vitu kama vipande vya bati,vyuma nyembe na kadhalika.

Je hii ni halali? Wanafunzi hao wanakutana na kipigo kikali pindi wanapo kosa kutimiza maagizo hayo kutoka kwa Waalimu wao. Kuna Wazazi kadhaa ambao wameondoa Watoto wao baada ya kupata taarifa za mambo wanayofanyiwa Watoto wao.

Kuna mengi sana ambayo ni tofauti kabisa ambayo yanaendelea pale ambayo Mamlaka husika inapaswa kuangalia bila kuchelewa.

IMG-20220628-WA0003.jpg
IMG-20220628-WA0006.jpg
 
Ni shule ya kiislam au?

Seminary watu wanaamshwa saa kumi na moja kulisha nguruwe, kumwagilia maji bustani

Hao wangesoma Seminary za kikatoliki si wangekuwa walishafukuzwa kwa uvivu na uzembe

Shule ni kazi, Hata kama kwenu hujui maana ya bustani au kumwagia maji maua Seminary utajifunza tu
Sasa hiyo shule wamevaa mabuibui wanataka wafundishwe alpha, bha, Che, kazi za mikono hawataki

Hawa vijana siku wakipewa kazi ya Sensa wataweza kweli?

Mimi watoto wangu nilifundisha kupika, kufua, Hakuna cha Mwanaume au Mwanamke nyumbani kwangu watu walipiga kazi

Leo wakiniona wanasema wewe kweli ni Master umetufanya tujiamini na hatuogopi mtu wala mazingira

Sasa hao kuchimba visiki na kuchota maji wanalia lia

Nani aje kuwachotea maji ya kuoga wenyewe?
 
Ni shule ya kiislam au?

Seminary watu wanaamshwa saa kumi na moja kulisha nguruwe, kumwagilia maji bustani

Hao wangesoma Seminary za kikatoliki si wangekuwa walishafukuzwa kwa uvivu na uzembe

Shule ni kazi, Hata kama kwenu hujui maana ya bustani au kumwagia maji maua Seminary utajifunza tu

Sasa hiyo shule wamevaa mabuibui wanataka wafundishwe alpha, bha, Che, kazi za mikono hawataki
Hapana ni mchanganyiko ila wanaopenda kuvaa hijab ruksa
 
Wazazi kwenye vikao vyao wapewe elimu kuwa mtoto atafundshwa masomo ya darasani pia atafundshwa na kaz ndogo ndogo Kama vle kulima bustan za mboga, kujenga wigo etc, ili siku akimaliza aweze kuzifanya hzo Kaz kwa faida yake mwenyewe.
 
Kuna upigaji bila shaka
 
Back
Top Bottom