Ingawa inasemekana kinadharia kuwa Rais ndio anayeteua wabunge watakaoingia kwenye bunge la katiba ukweli ni kwamba mawaziri wawili wa sheria [ wa sasa na aliyeanzisha mchakato] ndio watakaokuwa wahusika wakuu wa kuchambua majina ya waliopendekezwa. Hawa wawili wote ni wanasheria na ingawa kuna mwongozo wa jinsi ya kuteua kufuatana na makundi lakini nachelea kuwa watakaochaguliwa wengi watakuwa na background ya sheria kwani kuna dhana potofu kuwa wanasheria ndio watunga katiba!!!
Ikumbukwe kuwa katika Katiba kuna mambo mengi yanayohusu ustawi wa jamii kwa ujumla wake ; itakuwa busara basi kama wanataaluma wengine kama vile wachumi wakapata nafasi ya kuwa kwenye hilo bunge ili waweze kutoa mchango wao kwenye maeneo yanayohusu taaluma zao. Bunge letu la sasa halina wachumi wengi na waliobobea kiasi cha kuamini kuwa watasaidia katika kuboresha rasimu ya katiba ;uhaba huo unajidhihilisha na uteuzi wa mawaziri uliofanywa hivi karibuni kuongoza wizara ya fedha na mipango!!
Ikumbukwe kuwa katika Katiba kuna mambo mengi yanayohusu ustawi wa jamii kwa ujumla wake ; itakuwa busara basi kama wanataaluma wengine kama vile wachumi wakapata nafasi ya kuwa kwenye hilo bunge ili waweze kutoa mchango wao kwenye maeneo yanayohusu taaluma zao. Bunge letu la sasa halina wachumi wengi na waliobobea kiasi cha kuamini kuwa watasaidia katika kuboresha rasimu ya katiba ;uhaba huo unajidhihilisha na uteuzi wa mawaziri uliofanywa hivi karibuni kuongoza wizara ya fedha na mipango!!