Ambokile H Mwaisaka
Member
- Sep 9, 2021
- 17
- 38
Hello ,Mimi ni daktari mafunzoni ,karibu katika uzi wangu.
Punde tu baada ya wapenzi wawili kukutana kimwili wengi wazo la kwanza kuja kichwani ikiwa hawajapanga kuwa na mtoto huwa ni P2(morning after pill),haijalishi wanakutana mara ngapi,kila wakutanapo ni P2 tu.
Hivi hizi ni kanakwamba hazina madhara?
Au Pipi kifua?
Sasa ni zipi njia bora zaidi za kuzuia mimba zisiyotarajiwa pamoja na njia ya kalenda au P2 ambazo ni maarufu zaidi miongoni mwa watu?
Ninakuletea njia 15 za kisayansi zinazoweza kutumika kuzuia mimba(uzazi wa mpango) pamoja na faida na hasara kwa kila njia pendekezwa,pamoja na mapendekezo yangu binafsi kama mdau wa afya.
Uzazi wa mpango ni nini?
• Wapenzi wawili wanapokaa kujadili na kuamua idadi ya watoto ambao wangependa kuwa nao na kwa wakati gani,ili wapewe mapenzi ya kutosha,matunzo na elimu bora kwa kila mtoto
• Kupanga idadi na wakati wa kuwa na watoto ni jukumu la wote wawili ,sio tu mwanaume au mwanamke tu.
Ni njia zipi za kuzuia mimba (Contraception)?
Zipo njia mbali mbali kulingana na malengo ya wapenzi, malengo yanaweza kuwa;
• Kuchelewesha mimba ya kwanza
• Kuacha muda kati ya mimba na mimba nyingine
• Kupunguza ukubwa wa familia
CATEGORIA ZA NJIA ZA KUZUIA MIMBA
1.Pharmacological and Non pharmacological
2.Short acting and Long acting contraceptives
3.Reversible and Non reversible techniques
SIFA ZA NJIA NZURI ZA KUZUIA MIMBA
1.Ni salama
2.Ifanye kazi kwa 100%
3.Free/ minimum side effects
4.Affordable
5.Acceptable to the user
6.Free of effects on future pregnancies
NJIA ZA UZAZI WA MPANGO ZINAZOTUMIA HOMONI
01.KIPANDIKIZI(IMPLANT)
Kipandikizi ni kibomba kidogo (chenye urefu wa milimita nne) ambacho huingizwa chini ya ngozi ya mkono wa mwanamke. Hutua homoni ambazo hulizuia yai la mwanamke kupevuka na kukuepusha kupata mimba.
Kipandikizi hiki kinauwezo wa kukaa kwa miaka minne lakini hakitakuzuia kupata/kuambukizwa magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 0.1%
Picha:Google
02.VIDONGE
Vidonge vya uzazi wa mpango ambavyo hutumiwa na mwanamke huwa na homoni ambazo hukuepusha kupata mimba kwa kuzuia yai la mwanamke kutokupevuka na hivi hutumiwa kila siku muda ule ule.Hivi sio sawa na P2.
Vidonge vya uzazi wa mpango havizuii maambukizi ya magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 7%
Picha:Google
03.SINDANO
Sindano nikama vidonge na kipandikizi – Huzuia yai la mwanamke kupevuka kwa kutumia homoni,hukuzuia kupata mimba na hii huchomwa matakoni au mkononi kila baada ya miezi mitatu. Njia hizi hazitakuzuia kupata/kuambukizwa magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 4%.
Picha: Google
FAIDA
• Hufanya kazi kwa muda mrefu.
• Hazina athari katika uzalishaji wa maziwa kwa mama
• Uwezekano mdogo sana kupata upungufu wa madini chuma
HASARA
• Hedhi huvurugika
• Kushindwa kuzalisha mayai kwa muda fulani hata baada ya kuacha kutumia sindano.
• Kwa watumiaji wa muda mrefu wa medroxyprogesterone,mifupa kungua uzito ni tatizo.
04.Patch
Patch hubandikwa sehemu za chini ya tumbo,matakoni na sehemu za juu za mwili pia(lakini sio kwenye matiti).Hii ni mpaka ipendekezwe na daktari.
Hufanya kazi kwa kutoa homoni kwenda kwenye damu kama njia ya vidonge na sindano.Unabandika Patch mpya mara moja kwa wiki ndani ya wiki tatu na wiki ya nne haubandiki patch ili upate siku zako.
Typical use failure rate: 7%.
Picha:Google
05.Hormonal vaginal contraceptive ring.
Hii ringi hutoa homoni kama njia nyingine,huwekwa ndani ya uke na huvaliwa kwa wiki tatu na wiki ya nne hutolewa ili kuruhusu hedhi kisha unavaa ringi mpya.
Typical use failure rate: 7%
Picha.Google
INTRAUTERINE DEVICES ( Vifaa vinavyopachikwa kwenye kuta za kizazi)
06.LEVONOGESTREL DEVICE (MIRENA)
Hiki kifaa huachia Levonogestrel kwenye kizazi(uterus).
Picha.Google
07.Copper T intrauterine device
Ni kifaa kidogo ambacho hufanana na umbile la herufi T huwekwa katika kuta za kizazi(uterus) na kinaweza kukaa mpaka miaka 10.
Typical use failure rate:0.8%
Picha.Google
KAMA UNA HALI ZIFUATAZO HUTOPASWA KUTUMIA HIVI VIFAA IUD
• Mimba au kuhisi una mimba
• PID pelvic inflammatory disease
• Uvimbe katika kuta za kizazi
• Kuvuja damu sehemu za siri bila kujua sababu.
• Suspected Cancer.
NJIA ZINAZOWEKA KIZUIZI(BARRIER METHODS)
08.DIAPHRAGM
Hivi huwekwa ndani ya uke kufunika shingo ya mlango wa kizazi(cervix) ili kuzuia mbegu za kiume kuingia.
Ina umbile la kikombe kidogo na huwekwa na chemikali zinazoweza kuua mbegu za kiume(spermicide)
Typical use failure rate: 17%
Picha.Google
09.KONDOMU
Kondomu ni njia pekee ya uzazi wa mpango ambayo
inazuia vyote, mimba, magonjwa ya ngono ukiwemo
virusi vya ukimwi. Zinazuia shahawa za mwanaume
kuingia kwenye uke wa mwanamke.
Typical use failure rate: 13%
Usitumie kondomu na mafuta ya kulainisha au chochote ,husababisha Kondomu kuchanika kirahisi.
Picha:Google
NJIA ZA ASILI ZA UZAZI WA MPANGO
Hizi huusisha kujua siku ambazo mwanamke anaweza pata mimba ili aongeze umakini au kuepuka ngono katika siku hizo.
Ubaya wake: Mabadiliko ya siku za hedhi hufanya njia hii kuwa hatari.
Na hizi ni pamoja na;
• CALENDAR METHOD
Njia hii ni nzuri na ni njia pendwa zaidi miongoni mwa watu kwasababu haihusishi maumivu ya aina yoyote wala chemikali ila inapaswa kutumika kwa tahadhari.
Itumike ikiwa tu mzunguko wa mwanamke unaenda vizuri(regular) na sio usioeleweka,Tofauti na hapo unaweza pelekea ujauzito na tumeona wengi waliotumia njia hii wakapata mimba.
• KUMWAGA NJE(WITHDRAWING)
Njia hii ina ufanisi mdogo kufananisha na njia nyingine kwasababu ni kweli unaweza ukafanikiwa vizuri kabisa kumwagia nje lakini kuna mbegu zinaweza kubaki katika kichwa cha uume na kwa asilimia fulani zikawa sababu ya mimba.
Wakati gani?. Pale ambapo mwanaume anahisi anaelekea kumwaga shahawa(ejaculation).
Na baada ya kumwaga nje kabla hajaendelea na tendo ahakikishe amesafisha vizuri uume wake au akojoe kwasababu mkojo una tindikali(acid) mbegu za kiume hufa.
• Lactation amenorrhea method (LAM)
Kwa wanawake ambao wametoka kupata mtoto na wananyonyesha hii njia ya LAM_lactation amenorrhea method inaweza kutumika ikiwa ana vifu vifuatavyo a) Hapati siku zake za hedhi b)ananyonyesha c) chini ya miezi sita baada ya kujifungua.
Hii ni nia ya muda mfupi na inapaswa itumike ikiwa mwanamke ana hizo hali tatu tajwa hapo juu.
NJIA ZA MUDA MREFU (MOJA KWA MOJA)
12.FEMALE STERILIZATION (TUBAL LIGATION OR TYING TUBES).
Mirija ya mwanamke ya falopiani inaweza kufungwa ili kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana kwaajili ya urutubishaji.Hii inaweza fanywa hospitalini tu
Typical use failure rate: 0.5%
Picha.Google
13.MALE STERILIZATION _ VASECTOMY
Hii hufanyika kuzuia mbegu za kiume kuufikia uume,hivyo manii ya mwanaume haitokuwa na seli hai za kiume za kuweza kurutubisha yai.
Typical use failure rate: 0.5%
Picha:Google
NJIA ZINAZOTUMIKA WAKATI WA DHARULA
Njia za wakati wa dharula sio njia zinazopaswa kutumika kila siku kama njia za uzazi wa mpango.Hii hutumika ikiwa wakati wa tendo la ndoa hakuna nia yoyote ya uzazi wa mpango iliyotumika au njia iliyotumika ilishindwa kukidhi vigezo mfano Kondomu kuchanika.
Copper IUD__ Wanawake wanaweza kuwekewa Copper IUD baada ya kufanya ngono zembe ndani ya siku tano.
MORNING AFTER PILL (P2)
Hii huwa na dozi kubwa ya mchanganyiko wa homoni ya estrogen na progestin au progestin tu.
Hutumika ndani ya masaa 72 ya kufanya ngono zembe. Uwezekano wa kufanya kazi vizuri zaidi huongezeka ikitumiwa mapema zaidi.
• Hakuna madhara ya muda mrefu ambayo mpaka sasa yamegunduliwa yatokanayo ya matumizi ya P2.
• Ikumbukwe kuwa P2 haipaswi kufanywa kuwa mbadala wa njia nyingine za uzazi.
• Mtu aliye na uzito mkubwa P2 inaweza isifanye kazi vizuri kuliko kwa aliye na uzito wa kawaida.
• P2 sio uhakikisho 100% kuwa hutopata mimba ,inafanya kazi 87% na ikiwa hujapata kuona siku zako kwa zaidi ya wiki moja,unashauriwa kufanya kipimo cha mimba.
ATHARI AMBAZO UNAWEZA PATA KWA KUTUMIA P2,hizi huwa ni za siku chache tu.
• Kichefu chefu au kutapika
• Kizungu zungu
• Kichwa kuuma
• Uchovu
• Matiti kujaa
• Maumivu chini ya kitovu
• Mzunguko wa hedhi kuvurugika
Asante kwa kutumia muda wako kusoma.
Punde tu baada ya wapenzi wawili kukutana kimwili wengi wazo la kwanza kuja kichwani ikiwa hawajapanga kuwa na mtoto huwa ni P2(morning after pill),haijalishi wanakutana mara ngapi,kila wakutanapo ni P2 tu.
Hivi hizi ni kanakwamba hazina madhara?
Au Pipi kifua?
Sasa ni zipi njia bora zaidi za kuzuia mimba zisiyotarajiwa pamoja na njia ya kalenda au P2 ambazo ni maarufu zaidi miongoni mwa watu?
Ninakuletea njia 15 za kisayansi zinazoweza kutumika kuzuia mimba(uzazi wa mpango) pamoja na faida na hasara kwa kila njia pendekezwa,pamoja na mapendekezo yangu binafsi kama mdau wa afya.
Uzazi wa mpango ni nini?
• Wapenzi wawili wanapokaa kujadili na kuamua idadi ya watoto ambao wangependa kuwa nao na kwa wakati gani,ili wapewe mapenzi ya kutosha,matunzo na elimu bora kwa kila mtoto
• Kupanga idadi na wakati wa kuwa na watoto ni jukumu la wote wawili ,sio tu mwanaume au mwanamke tu.
Ni njia zipi za kuzuia mimba (Contraception)?
Zipo njia mbali mbali kulingana na malengo ya wapenzi, malengo yanaweza kuwa;
• Kuchelewesha mimba ya kwanza
• Kuacha muda kati ya mimba na mimba nyingine
• Kupunguza ukubwa wa familia
CATEGORIA ZA NJIA ZA KUZUIA MIMBA
1.Pharmacological and Non pharmacological
2.Short acting and Long acting contraceptives
3.Reversible and Non reversible techniques
SIFA ZA NJIA NZURI ZA KUZUIA MIMBA
1.Ni salama
2.Ifanye kazi kwa 100%
3.Free/ minimum side effects
4.Affordable
5.Acceptable to the user
6.Free of effects on future pregnancies
NJIA ZA UZAZI WA MPANGO ZINAZOTUMIA HOMONI
01.KIPANDIKIZI(IMPLANT)
Kipandikizi ni kibomba kidogo (chenye urefu wa milimita nne) ambacho huingizwa chini ya ngozi ya mkono wa mwanamke. Hutua homoni ambazo hulizuia yai la mwanamke kupevuka na kukuepusha kupata mimba.
Kipandikizi hiki kinauwezo wa kukaa kwa miaka minne lakini hakitakuzuia kupata/kuambukizwa magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 0.1%
Picha:Google
02.VIDONGE
Vidonge vya uzazi wa mpango ambavyo hutumiwa na mwanamke huwa na homoni ambazo hukuepusha kupata mimba kwa kuzuia yai la mwanamke kutokupevuka na hivi hutumiwa kila siku muda ule ule.Hivi sio sawa na P2.
Vidonge vya uzazi wa mpango havizuii maambukizi ya magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 7%
Picha:Google
03.SINDANO
Sindano nikama vidonge na kipandikizi – Huzuia yai la mwanamke kupevuka kwa kutumia homoni,hukuzuia kupata mimba na hii huchomwa matakoni au mkononi kila baada ya miezi mitatu. Njia hizi hazitakuzuia kupata/kuambukizwa magonjwa ya ngono.
Typical use failure rate: 4%.
Picha: Google
FAIDA
• Hufanya kazi kwa muda mrefu.
• Hazina athari katika uzalishaji wa maziwa kwa mama
• Uwezekano mdogo sana kupata upungufu wa madini chuma
HASARA
• Hedhi huvurugika
• Kushindwa kuzalisha mayai kwa muda fulani hata baada ya kuacha kutumia sindano.
• Kwa watumiaji wa muda mrefu wa medroxyprogesterone,mifupa kungua uzito ni tatizo.
04.Patch
Patch hubandikwa sehemu za chini ya tumbo,matakoni na sehemu za juu za mwili pia(lakini sio kwenye matiti).Hii ni mpaka ipendekezwe na daktari.
Hufanya kazi kwa kutoa homoni kwenda kwenye damu kama njia ya vidonge na sindano.Unabandika Patch mpya mara moja kwa wiki ndani ya wiki tatu na wiki ya nne haubandiki patch ili upate siku zako.
Typical use failure rate: 7%.
Picha:Google
05.Hormonal vaginal contraceptive ring.
Hii ringi hutoa homoni kama njia nyingine,huwekwa ndani ya uke na huvaliwa kwa wiki tatu na wiki ya nne hutolewa ili kuruhusu hedhi kisha unavaa ringi mpya.
Typical use failure rate: 7%
Picha.Google
INTRAUTERINE DEVICES ( Vifaa vinavyopachikwa kwenye kuta za kizazi)
06.LEVONOGESTREL DEVICE (MIRENA)
Hiki kifaa huachia Levonogestrel kwenye kizazi(uterus).
Picha.Google
07.Copper T intrauterine device
Ni kifaa kidogo ambacho hufanana na umbile la herufi T huwekwa katika kuta za kizazi(uterus) na kinaweza kukaa mpaka miaka 10.
Typical use failure rate:0.8%
Picha.Google
KAMA UNA HALI ZIFUATAZO HUTOPASWA KUTUMIA HIVI VIFAA IUD
• Mimba au kuhisi una mimba
• PID pelvic inflammatory disease
• Uvimbe katika kuta za kizazi
• Kuvuja damu sehemu za siri bila kujua sababu.
• Suspected Cancer.
NJIA ZINAZOWEKA KIZUIZI(BARRIER METHODS)
08.DIAPHRAGM
Hivi huwekwa ndani ya uke kufunika shingo ya mlango wa kizazi(cervix) ili kuzuia mbegu za kiume kuingia.
Ina umbile la kikombe kidogo na huwekwa na chemikali zinazoweza kuua mbegu za kiume(spermicide)
Typical use failure rate: 17%
Picha.Google
09.KONDOMU
Kondomu ni njia pekee ya uzazi wa mpango ambayo
inazuia vyote, mimba, magonjwa ya ngono ukiwemo
virusi vya ukimwi. Zinazuia shahawa za mwanaume
kuingia kwenye uke wa mwanamke.
Typical use failure rate: 13%
Usitumie kondomu na mafuta ya kulainisha au chochote ,husababisha Kondomu kuchanika kirahisi.
Picha:Google
NJIA ZA ASILI ZA UZAZI WA MPANGO
Hizi huusisha kujua siku ambazo mwanamke anaweza pata mimba ili aongeze umakini au kuepuka ngono katika siku hizo.
Ubaya wake: Mabadiliko ya siku za hedhi hufanya njia hii kuwa hatari.
Na hizi ni pamoja na;
• CALENDAR METHOD
Njia hii ni nzuri na ni njia pendwa zaidi miongoni mwa watu kwasababu haihusishi maumivu ya aina yoyote wala chemikali ila inapaswa kutumika kwa tahadhari.
Itumike ikiwa tu mzunguko wa mwanamke unaenda vizuri(regular) na sio usioeleweka,Tofauti na hapo unaweza pelekea ujauzito na tumeona wengi waliotumia njia hii wakapata mimba.
• KUMWAGA NJE(WITHDRAWING)
Njia hii ina ufanisi mdogo kufananisha na njia nyingine kwasababu ni kweli unaweza ukafanikiwa vizuri kabisa kumwagia nje lakini kuna mbegu zinaweza kubaki katika kichwa cha uume na kwa asilimia fulani zikawa sababu ya mimba.
Wakati gani?. Pale ambapo mwanaume anahisi anaelekea kumwaga shahawa(ejaculation).
Na baada ya kumwaga nje kabla hajaendelea na tendo ahakikishe amesafisha vizuri uume wake au akojoe kwasababu mkojo una tindikali(acid) mbegu za kiume hufa.
• Lactation amenorrhea method (LAM)
Kwa wanawake ambao wametoka kupata mtoto na wananyonyesha hii njia ya LAM_lactation amenorrhea method inaweza kutumika ikiwa ana vifu vifuatavyo a) Hapati siku zake za hedhi b)ananyonyesha c) chini ya miezi sita baada ya kujifungua.
Hii ni nia ya muda mfupi na inapaswa itumike ikiwa mwanamke ana hizo hali tatu tajwa hapo juu.
NJIA ZA MUDA MREFU (MOJA KWA MOJA)
12.FEMALE STERILIZATION (TUBAL LIGATION OR TYING TUBES).
Mirija ya mwanamke ya falopiani inaweza kufungwa ili kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana kwaajili ya urutubishaji.Hii inaweza fanywa hospitalini tu
Typical use failure rate: 0.5%
Picha.Google
13.MALE STERILIZATION _ VASECTOMY
Hii hufanyika kuzuia mbegu za kiume kuufikia uume,hivyo manii ya mwanaume haitokuwa na seli hai za kiume za kuweza kurutubisha yai.
Typical use failure rate: 0.5%
Picha:Google
NJIA ZINAZOTUMIKA WAKATI WA DHARULA
Njia za wakati wa dharula sio njia zinazopaswa kutumika kila siku kama njia za uzazi wa mpango.Hii hutumika ikiwa wakati wa tendo la ndoa hakuna nia yoyote ya uzazi wa mpango iliyotumika au njia iliyotumika ilishindwa kukidhi vigezo mfano Kondomu kuchanika.
Copper IUD__ Wanawake wanaweza kuwekewa Copper IUD baada ya kufanya ngono zembe ndani ya siku tano.
MORNING AFTER PILL (P2)
Hii huwa na dozi kubwa ya mchanganyiko wa homoni ya estrogen na progestin au progestin tu.
Hutumika ndani ya masaa 72 ya kufanya ngono zembe. Uwezekano wa kufanya kazi vizuri zaidi huongezeka ikitumiwa mapema zaidi.
• Hakuna madhara ya muda mrefu ambayo mpaka sasa yamegunduliwa yatokanayo ya matumizi ya P2.
• Ikumbukwe kuwa P2 haipaswi kufanywa kuwa mbadala wa njia nyingine za uzazi.
• Mtu aliye na uzito mkubwa P2 inaweza isifanye kazi vizuri kuliko kwa aliye na uzito wa kawaida.
• P2 sio uhakikisho 100% kuwa hutopata mimba ,inafanya kazi 87% na ikiwa hujapata kuona siku zako kwa zaidi ya wiki moja,unashauriwa kufanya kipimo cha mimba.
ATHARI AMBAZO UNAWEZA PATA KWA KUTUMIA P2,hizi huwa ni za siku chache tu.
• Kichefu chefu au kutapika
• Kizungu zungu
• Kichwa kuuma
• Uchovu
• Matiti kujaa
• Maumivu chini ya kitovu
• Mzunguko wa hedhi kuvurugika
Asante kwa kutumia muda wako kusoma.