Madhara ya kufanya mapenzi mara kwa mara

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono. Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.

Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa mahari. Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.

Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana hata kwenye nguzo ya umeme na chini ya miti kwa vile tu miili imetaka kufurahika. Twende pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.

KUPOTEZA HAMU YA TENDO

Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara. Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.

Aidha kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA

Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani?

Watu wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake. Hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi. Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.

KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO

Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako. Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!

KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI

Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili. Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha. Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

KUPATA MAGONJWA

Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

Baada ya kungalia madhara hayo machache ni vema kwa wapenzi kupunguza kiwango cha kufanya mapenzi ili kuifanya miili iwe na uvumilivu unaoweza kumsaidia mtu kukaa kwa muda mrefu bila kumsaliti mpenzi wake hata kama atakuwa amesafiri mbali naye kimasomo, kikazi au kibiashara
 
Mkuu MziziMkavu, what about the opposite? Yaani madhara ya kutofanya mapenzi mara kwa mara?
Mkuu WA-UKENYENGE Hizi sababu kwa aji ya wale wanaopenda kila wakati kubadilisha wapenzi Wazinzi sio wenye wake zao mkuu. Na kila kitu ukizidisha kina madhara yake ukipunguza pia kina madhara yake inatakikan uwe unafanya kila kitu kwa kipimo chake kati kwa kati usizidishe wala kupunguza.

Mkuu hizi sababu labda unaongelea watu wanaobadilisha kila siku lakini kwa wapendanao naona kama ni opposite vile
Mkuu StayReal Ni Sawa unavyosema hii kwa ajili ya wale Wazinifu sio wale wenye Wake zao au mpenzi Mmoja tu . Je kuna watu wana mpenzi Mmoja tu?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu WA-UKENYENGE Hizi sababu kwa aji ya wale wanaopenda kila wakati kubadilisha wapenzi Wazinzi sio wenye wake zao mkuu. Na kila kitu ukizidisha kina madhara yake ukipunguza pia kina madhara yake inatakikan uwe unafanya kila kitu kwa kipimo chake kati kwa kati usizidishe wala kupunguza.

Mkuu StayReal Ni Sawa unavyosema hii kwa ajili ya wale Wazinifu sio wale wenye Wake zao au mpenzi Mmoja tu . Je kuna watu wana mpenzi Mmoja tu?

Wapo mkuu!
 
mkuu wewe ukioa utafanya mara ngapi kwa wiki na mke wako? au ndo mwezi mpk mwezi utapigiwa ndugu mkeo unatakiwa umpatie raha za dunia.RAHA YA MAPENZI MKOJO WAKO TU!
Mkuu MASOUD NYUMBANYINGI inatakikana umfanye mke wako kwa wiki mara 3 tu sio tena kila siku kwani

huyo mke wako amegeuka mpira wa kuchezea uwanjani? Mke wako au mpenzi wako Hachoki kufanywa kila siku? Mkuu amka kuzidisha kitu kuna

madhara yake makubwa hata chakula ukila sana mwisho wake utavimbirwa na kupatwa na maradhi ya ajabu kila kitu kina wastani

wake. Jaribu kila kitu kuweka kati kwa kati Wastani kila kitu fanya kwa kipimo fanya mapenzi kwa Afya yako sio

kumkomowa mpenzi wako au Mke wako una haraka ya nini? kufanya kila siku mapenzi naye mke wako? jiulize kisha

utapata jibu lako wewe mwenyewe ninakuacha hapo. Nallog off.
 
Last edited by a moderator:
Average Number of Sexual Partners

In the survey conducted by the National Center for Health Statistics on 6,237 adults between the ages of 20 to 59 from 1999 to 2002, it was found that 29% of men had 15 or more sexual partners, and 9% of women had sex with 15 or more men.
In the same survey, it¡¯s reported that 46% of black men and 13% of black women had 15 or more sexual partners in their lifetime and 17% of men and 10% of womenhad 2 or more sexual partners in the previous year.
It¡¯s also reported that 25% of women and 17% of men reported they had no more than one sexual partner in their entire life.

Statistics on Infidelity

In general, infidelity affected 80% of marriages and 16% of the respondents had cheated on their partners.
The percentage of men committing infidelity was 57%. The number of men who cheated on their wives was double the number of women who cheated on their husbands. Suggesting that women were more conservative.
The Average Number of Times in a Week Married Couple Has Sex

34% of married couple had sex about 2 to 3 times in a week and 7% had sex more than 4 times in a week. Doctors advise couples to have sex at least once a week for women to stay healthy.
 
Average Number of Sexual Partners

In the survey conducted by the National Center for Health Statistics on 6,237 adults between the ages of 20 to 59 from 1999 to 2002, it was found that 29% of men had 15 or more sexual partners, and 9% of women had sex with 15 or more men.
In the same survey, it¡¯s reported that 46% of black men and 13% of black women had 15 or more sexual partners in their lifetime and 17% of men and 10% of womenhad 2 or more sexual partners in the previous year.
It¡¯s also reported that 25% of women and 17% of men reported they had no more than one sexual partner in their entire life.

Statistics on Infidelity

In general, infidelity affected 80% of marriages and 16% of the respondents had cheated on their partners.
The percentage of men committing infidelity was 57%. The number of men who cheated on their wives was double the number of women who cheated on their husbands. Suggesting that women were more conservative.
The Average Number of Times in a Week Married Couple Has Sex

34% of married couple had sex about 2 to 3 times in a week and 7% had sex more than 4 times in a week.
Code:
[SIZE=4][COLOR=red]Doctors advise couples to have sex at least once[/COLOR] a week for women to stay healthy[/SIZE]
.
kah!!! mara moja tu? / week?? hawako serious hawa ma dr
 
Mkuu MziziMkavu aminia baba. Ukiendekeza mapenzi na hasa enzi hizi za magonjwa kila aina bila shaka siku zako za kuishi zinapungua mara dufu. Mimi na mke wangu tukizidisha sana ni mara mbili kwa wiki. Huwa tuna-enjoy weekend na kila mtu anaondoka ameshiba haswa. Kwa staili hiyo, stamina yangu ni nzuri na nimekuwa nikimridhisha mke wangu kwa kiwango cha juu sana.
 
Mkuu MziziMkavu aminia baba. Ukiendekeza mapenzi na hasa enzi hizi za magonjwa kila aina bila shaka siku zako za kuishi zinapungua mara dufu. Mimi na mke wangu tukizidisha sana ni mara mbili kwa wiki. Huwa tuna-enjoy weekend na kila mtu anaondoka ameshiba haswa. Kwa staili hiyo, stamina yangu ni nzuri na nimekuwa nikimridhisha mke wangu kwa kiwango cha juu sana.
Mkuu NdasheneMbandu hongera sana kwa kufanya hivyo hata kama utazidisha mara1 ikiwa utafanya mara 3 kwa wiki itakuwa sio mbaya kuliko kufanya kila siku kwanza utakuwa huna afya nzuri na hutaweza kufanya tendo kwa raha zaidi inatakikana uwe unapumzika japo kwa wiki mara 2 au 3 ndio mzuri kwa afya yako asante mkuu ubarikie.
 
Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono. Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.

Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa mahari. Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.

Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana hata kwenye nguzo ya umeme na chini ya miti kwa vile tu miili imetaka kufurahika. Twende pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.

KUPOTEZA HAMU YA TENDO

Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara. Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.

Aidha kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA

Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani?

Watu wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake. Hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi. Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.

KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO

Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako. Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!

KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI

Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili. Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha. Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

KUPATA MAGONJWA

Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

Baada ya kungalia madhara hayo machache ni vema kwa wapenzi kupunguza kiwango cha kufanya mapenzi ili kuifanya miili iwe na uvumilivu unaoweza kumsaidia mtu kukaa kwa muda mrefu bila kumsaliti mpenzi wake hata kama atakuwa amesafiri mbali naye kimasomo, kikazi au kibiashara

dah kaazi kweli kweli , hiyo ni kweli kabsaa kuna shwaiba mmoja yani yeye kabla hajaoa alikuwa kashapitia karibu mtaa mzima bana , alivyotangaza nia ya kuoa wazazi wa huo mtaa walifurahi wakasema afadhali mabinti zetu wapumue , asa ameoa ana mtoto mmoja ila wife wake analalamika hovyo kwamba mumewe yaweza pita miezi mitatu hata hajamgusa jamaa anadai hana appetite , asa mkewe hana furahi kabisa na ndoa yao ina miaka 3 tu , asa wife anahisi jamaa ana kidemu kingine so kila wakati unampigia simu mumewe UKO WAPI UKO NA NANI ? yani mwanamke ana wivu wakupitiliza ila hana raha na ndoa asa sijui mumewe kwa vile alipiga mechi nyingi sana au mkewe haoneshi manjonjo kama yale aliyokuwa akiyapata mechi za ugenini ? yani wanawake tuna kazi ya ziada . yani mwanaume anafanya comparison kati ya mkewe na yule demu wa mechi za ugenini afu anafanya evaluation afu kama hapati utility ya kutosha kwa mkewe anakuwa ana mnyima haki mkewe , dah quite unfair
 
Mkuu NdasheneMbandu hongera sana kwa kufanya hivyo hata kama utazidisha mara1 ikiwa utafanya mara 3 kwa wiki itakuwa sio mbaya kuliko kufanya kila siku kwanza utakuwa huna afya nzuri na hutaweza kufanya tendo kwa raha zaidi inatakikana uwe unapumzika japo kwa wiki mara 2 au 3 ndio mzuri kwa afya yako asante mkuu ubarikie.

Mara 2 au 3 kwa wiki lkn he unapiga goli ngapi kwa kila game?. Assume mmoja anapiga goli moja kila usiku kwa usiku 7 yaan goli 7 kwa wiki na mwingine anacheza 3 kwa wiki lkn kila mchezo goli 3 yan goli 9 kwa wiki sasa hapo nani atakuwa ana madhara zaidi
 
Back
Top Bottom