Kwanini wanyama hawafanyi mapenzi kinyume na maumbile?

Siwatetei wanawake ila hata wanaume wanapenda. n iambo tunalolichochea sisi wanaume. hivi mwanamke ana uume? kama mwanaume akikataa n wazi mwanamke hana ujanja. kuzidi kujadili hii ishu n kuipa promo
 
Mchezo huu umekuwa ukipendwa sana na wanaume wengi ambao wengi wao huwa hawatumii kinga na kusababisha wengi kupata magonjwa ya zinaa pamoja na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Lakini mchezo wa kuruka ukuta umekuwa na madhara makubwa sana kwa wanaume wanaoufanya kwa muda mrefu.

Tulipoangalia upande wa wanawake, tuliona sehemu kubwa ya wanaopenda mchezo huu ni wanaume ambao wengine wamebatizwa majina ya ‘basha’, wakimaanisha mwanaume mpenda kuruka ukuta bila kujali kumtumia mwanaume mwenzake au mwanamke.

Kwa vile nia ya kona hii ni kuelimisha madhara ya mtu kupenda kuruka ukuta ili aache mara moja, tunaendelea kutoa elimu ya bure ili mtu yakimkuta ajue yamempata kwa kiburi chake na kwa kupenda starehe ya kipuuzi.

Madhara anayoyapata mwanaume anayependa mchezo huo ni kama ifuatavyo:

Kwanza: Husababisha kusinyaa au kuweka makovu kwenye njia ya haja ndogo.

Pili: Njia ya haja ndogo kuziba kiasi au kuziba kabisa.

Tatu: Kupata saratani (kansa) ya tezi za figo (prostate gland).

Nne: Kupata magonjwa sugu ya uti wa mgongo.Tano: Kuharisha.

Sita: Maambukizi ya VVU ambapo mwisho wake ni Upungufu wa Kinga Mwilini (Ukimwi)

Saba: Baadaye mhusika kupata msongo wa mawazo au sonona kwa kujutia tendo hilo.

Nina imani ndugu yangu umeona madhara mabaya sana ya tabia hiyo mbaya. Inawezekana umezoea mchezo huo wa kuwaingilia wenzako na kuona raha lakini tumeona madhara yake, ambayo kwa hakika kama wewe ni mmoja wao, unatakiwa kuacha mara moja kwa vile mwisho wake ni majuto na mateso.

Jiepushe kuiga mambo bila kujua faida na hasara zake pia usimtie mwenzako majaribuni kwa kumlazimisha kuingia kwenye mchezo huo.

Wanawake wengi wamekuwa wakilazimishwa na wanaume kuingiliwa kinyume na maumbile kwa kuwatishia kuwaacha kama watakataa.Swali linakuja, kipi bora, kuharibiwa au kuachana?

Kumbuka baada ya kuharibikiwa, thamani yako hushuka na sifa yako ikiwafikia waharibifu wa watu, basi unageuzwa jamvi la mtaa na hatimaye unakufa kwa msongo wa mawazo au mateso ya ugonjwa utakaupata baada ya kukubali kuingiliwa kinyume na maumbile.

Unaweza kushangaa baada ya kuelezea madhara yanayowapata wanaume nimehamia kwa wanawake.

Ukweli mchezo huu umewaathiri sana wanawake ambao wengi wanaujutia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wale wanaume wa sodoma waliotaka kulala na wageni(wanaume) wa lutu kimwili pamoja na wageni (malaika) kuwapiga upofu bado waliendelea kupapasa ili waupate mlango walale na wageni hao kwa nguvu,,,

Hayo yalikuwa ni moja ya madhara ya moja kwa moja ya tabia yao ovu lakini hawakusikia na kujutia uovu wao na baadae wakaangamizwa kwa moto kwa sababu sikio la kufa halisikii dawa laiti wangetubu na kuacha uovu huo wangeokoka usiku ule na lutu...

Hata leo watu wamefanya ni fasheni na sehemu ya maisha ndio sababu hata hapa kebehi ni nyingi kumlenga mtoa mada ila ukweli ni kuwa ndugu msipobadilika na kumuhofu Mungu na kuacha hayo matendo maovu kweli siku ipo karibu ambapo anguko na kilio kwenu vitakuwa mzigo mzito unaelemea.... Wapenzi Tubadilike kuna kila sababu ya kumuhofu Mungu na kufanya yote tufanyayo kwa utukufu wake
 
Back
Top Bottom