Madereva waandamana kwenda LATRA wanataka Uber, Bolt wapandishe bei ya nauli

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Dereva1.jpg

Dereva.jpg

DERE.jpg


Madereva wa taxi za mitandao (Uber na Bolt) wameamua kuandamana mpaka makao makuu ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhnj(LATRA), kudai kupandishwa kwa bei elekezi ambazo licha ya kupandishwa wahusika bado hawazifanyii kazi hali hiyo inatokana na kuendelea kupanda kwa bei ya mafuta

Source: Dar Mpya


==========================================

Madereva wa taksi za mitandao wameandamana mpaka makao makuu ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) Jijini Dar es Salaam kudai kupandishwa kwa bei elekezi ambazo licha ya kupandishwa bado kuna wahusika awazifanyii kazi hali hiyo inatokana na kuendelea kupanda kwa bei ya mafuta.

Madereva hao ambao ni wanachama wa Chama cha Madereva wa Mtandaoni (Tanzania Online Drivers Association - TODA) wamedai kuwa wamiliki wa huduma ya Uber na Bolt ndiyo ambao hawataki kupandisha bei ya nauli kitu ambacho kinawaumiza wao.

"Tumekuja LATRA kwa kuwa wao ndiyo waliowapa leseni Uber na Bolt, kuna App nyingine zimeshaongeza bei ya nauli, lakini wao hawataki, hivyo wateja hawawezi kwenda kwenye App yenye bei kubwa.

"Tunataka LATRA wafanye maamuzi, tulikuwa nao leo asubuhi (Aprili 12, 2022) pale Leaders Club, tukashindwana kwa kuwa wao wanaishia kusema wamewaandikia Uber na Bolt barua, kila siku hivyohivyo, ndiyo maana tumewafuata ofisini kwao watuleleze vizuri.

"Muda huu kuna wenzetu wachache tumewachagua wameingia ndani wanazungumza na viongozi, tunasubiri majiu yao," alisema dereva mmoja wa walioandamana.

 
Madereva wa taksi za mitandao (Uber na Bolt) wameamua kuandamana mpaka makao makuu ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kudai kupandishwa kwa bei elekezi ambazo licha ya kupandishwa wahusika bado hawazifanyii kazi hali hiyo inatokana na kuendelea kupanda kwa bei ya mafuta


Source: Dar Mpya

========================================

Hali hiyo inatokana na kuendelea kupanda kwa bei ya mafuta.

Mmoja wa madereva ambaye jina lake tumelihifadhi amedai kuwa madereva wanataka mamlaka iwanyang’anye leseni au kwa ufupi izime hizo App maana kuna App ambazo wametii agizo la Serikali kama vile ping, little ride na paisha.
Kwani Majaliwa kasema je?

IMG_20220407_154536_192.jpg
 
Mafuta yameongezeka kutoka wastani wa shs 2540 mpaka kufikia 2861 ambapo ongezeko ni tshs 321 ongezeko hilo ni sawa na 13% ila sasa cha kushangaza huko mitaani wasafirishaji wanaongeza nauli kwa ongezeko la mpaka 100% mfano kuna baadhi ya maeneo ambako nauli ilikuwa ni Tshs 500 wameongeza imekuwa 1,000 ambayo ni ongezeko la 100% hii si sawa

Hata hao wanaoandamana waruhusiwe tu kuongeza bei ya nauli kwa 13% kukata mzizi wa fitina otherwise watajiongezea wenyewe wapate pa kupigia hela
 
Mafuta yameongezeka kutoka wastani wa shs 2540 mpaka kufikia 2861 ambapo ongezeko ni tshs 321 ongezeko hilo ni sawa na 13% ila sasa cha kushangaza huko mitaani wasafirishaji wanaongeza nauli kwa ongezeko la mpaka 100% mfano kuna baadhi ya maeneo ambako nauli ilikuwa ni Tshs 500 wameongeza imekuwa 1,000 ambayo ni ongezeko la 100% hii si sawa

Hata hao wanaoandamana waruhusiwe tu kuongeza bei ya nauli kwa 13% kukata mzizi wa fitina otherwise watajiongezea wenyewe wapate pa kupigia hela
Ni wahuni, Leo nilimkodi uber mmoja akanieleza uber walikuwa wanachaji sh 500 per km, ongezeko wanalo dai ni ifikie 900 per km.

Ukiangalia kiasi cha fedha iliyoongezeka kwenye lita ya mafuta na ongezeko wanaloomba haviendani hata kidogo.
 
Ila serikali kwenye swala ili walipaswa kuwa mstari wa mbele sana katika kukemea upandaji na wangebaki na kauli ya kusema hii hali tunategemea baada kipindi kifupi kijacho mafuta kushuka bei
 
Ila serikali kwenye swala ili walipaswa kuwa mstari wa mbele sana katika kukemea upandaji na wangebaki na kauli ya kusema hii hali tunategemea baada kipindi kifupi kijacho mafuta kushuka bei
Serikali ipi? Ya Chama au Kivuli? Si alisema KILA KITU KITAPANDA BEI, nauli zitapanda n.k?

Subiri Mei Mosi, atapandisha pia
 
Back
Top Bottom