Madereva wa SU punguzeni kiburi

Ichobela

JF-Expert Member
Jan 7, 2012
326
156
Ni muda huu wa saa tisa na nusu nnapita barabara ya Sahara tokea barabara ya Pamba naelekea kafiwa katoliki kwa mnaoijua Mwanza mjini mmenipata vizuri na mtakuwa mnaijua vizuri barabara ilivyo na mawe kwani kuamka kupishana Ni hadi mawe wastaarabu bila hivyo mnaweza kumaliza masaa mkitazamana sababu ya mawe yaliyopo maana unaweza kuliacha gari lako hadi. Nmefika Landcruiser ya SU imepaki kwenye mteremko na ndani dreva yumo nikamwashia Taa kwa alone mawe kidogo maana pale alipopaki kapana sana sehemu ya kupishana, jamaa akaamua na kulala kabisa kwenye usukani, ikabidi nishuke ilivyo nimwombe alone kidogo ili nipite bila madhara kwa magari yote magari, alichonijibu Ni kwa mbona magari mengine ya nnapiga? Nikamwashia inawezekana lakini unaona sehemu uloiacha ili tupite? Jamaa kasema nimekujibu kistarabu sana naomba nikae kimya na ndicho alikifanya.....
Ombi langu jamaa kwa mnaoendesha magari ya SU mjitahidi kwa wastaarabu barabarani hayo magari yamenunuliwa kwa pesa yetu na mishahara mlinalipwa pesa zetu.
 

Attachments

  • IMG-20160717-WA0000.jpg
    IMG-20160717-WA0000.jpg
    65.5 KB · Views: 47
Halaf hamna watu wambea, wanafiki, majungu na wachonganish kama madereva wa V8 ama STK na SU serekalini sisemi wote lakin nauhakika 99.99% na ushirikina juu.

USHAHID NINAO
Nakuunga mkono Kwa 1000% wengi wakiwa chini ya miti wakati maboss wapo maofisini story zao ni Umbea mtupu , majungu Kwa wingi na kujisifu juu ya michepuko na speeds kubwa barabarani pasipo Tochi kuwagusa .
 
Hizo STK Kwa kutanua na kuvunja sheria za barabarani zinaongoza sana , wakiwa barabarani wanataka kila Gari iwapishe hawana nidhamu kwenye matumizi ya barabara kabsa , Kwa kifupi madereva wa Magari ya SU na STK na wenzao hawana mfano wa kuigwa pindi wakiwa barabarani .
 
Mleta mada na wewe ni mzembe mbona barabara pana vile tatizo unaogopa kupitisha gar kwenye mawe wakati iyo ni gari kubwa, ....wacha SU, STK, DFP WAkufunze kutumia barabara
 
Du hii na yenyewe habari ya siasa? Mods JF wako wapi watu wakichukuliana mademu uswahilini wanakimbilia JF kutoa stress zao.

Sasa hapa kesi sijui iko wapi manake ukiangalia picha unaona maluweluwe.
 
Mleta mada na wewe ni mzembe mbona barabara pana vile tatizo unaogopa kupitisha gar kwenye mawe wakati iyo ni gari kubwa, ....wacha SU, STK, DFP WAkufunze kutumia barabara
Hiyo barabara napita kila siku naijua zaidi ya unavyofikiria na Mimi si kichaa ndugu yangu,sehemu isiyokuwa na sababu ya kuharibu gari kwa nini nifanye majaribio?Angalia vizuri hizo mawe sharp kwa nyuma ya hiyo SU kuna sehemu kubwa tu anaweza kupaki na kusiwe na tatizo lolote na ndo nilimwomba apaki pale. Kumbuka alikuwa kapaki na kazima gari si kama tulikuwa tukipishana,my point is,kwa mini apaki hapo atuhangaishe sisi watumiaji wenzie!?
 
Mkuu bosi wake atakua yupo kwa mchepuko kwaiyo lazima kiburi kiwepo bosi yupp karibu
 
Back
Top Bottom