Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 747
- 3,059
Madereva wa daladala, Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wamegoma kusafirisha abiria baada ya kupandishiwa gharama za maegesho.
Wasafiri kwenda maeneo mbalimbali mkoani humo wameshindwa kusafiri kutoka stendi ya mabasi Bukoba baada ya kutokea kwa mgomo leo asubuhi
Wanapinga ongezeko la ushuru kotoka Tsh. 1,000 hadi Tsh. 2,000 kwa magari madogo(Hiace) na Tsh. 2,000 hadi Tsh. 4,000 kwa Coster huku kukiwa hakuna maboresho yaliyofanyika kituoni
Mwenyekiti Chama cha Kutetea Abiria Kagera(CHAKUA), Samidu Bashiru amepinga ongezeko hilo na kuongeza stendi hiyo haina choo wala jengo la kupumzikia abiria
Aidha, kufuatia mgomo huo, abiria waliokuwa wasafiri kutoka wilaya mbalimbali kwenda mjini Bukoba wanadaiwa kushindwa baada ya kukosekana kwa usafiri
Kamanda wa Polisi Bukoba, Revocatus Malimi amesema jeshi hilo linafuatilia mgomo wa madereva uliotokea kwenye manispaa hiyo kwa kile kilichodaiwa ni kupinga baadhi ya tozo zilizowekwa na manispaa hiyo.
Kwa mujibu wa Kamanda Malimi, Jeshi la Polisi linafuatilia kwa ukaribu ili kufahamu kuwa waliogoma ni madereva au ni wamiliki wa magari, na hivi karibuni jeshi hilo litatoa taarifa juu ya mgomo huo.
Akizungumza na www.eatv.tv Kamanda Revocatus Malimi amesema “taarifa ni za kweli ila jeshi letu linafuatilia lijue madai yao ni nini, pia tunahitaji kujua waliogoma ni wasafirishaji au ni abiria, na tumeambiwa ni mgomo baridi wa kutokutoa huduma.”
Mapema leo majira ya saa 3 asubuhi zilianza kusambaa taarifa juu ya kutokea kwa mgomo wa madereva wa daladala kutokutoa huduma za usafiri wakielekeza malalamiko yao kwa manispaa ya Bukoba.
Mbali na madai hayo pia inaelezwa kuwa madereva hao pia wanagomea juu ya ubovu wa miundombinu kwenye eneo ambalo wamekuwa wakiegesha magari yao.
Wasafiri kwenda maeneo mbalimbali mkoani humo wameshindwa kusafiri kutoka stendi ya mabasi Bukoba baada ya kutokea kwa mgomo leo asubuhi
Wanapinga ongezeko la ushuru kotoka Tsh. 1,000 hadi Tsh. 2,000 kwa magari madogo(Hiace) na Tsh. 2,000 hadi Tsh. 4,000 kwa Coster huku kukiwa hakuna maboresho yaliyofanyika kituoni
Mwenyekiti Chama cha Kutetea Abiria Kagera(CHAKUA), Samidu Bashiru amepinga ongezeko hilo na kuongeza stendi hiyo haina choo wala jengo la kupumzikia abiria
Aidha, kufuatia mgomo huo, abiria waliokuwa wasafiri kutoka wilaya mbalimbali kwenda mjini Bukoba wanadaiwa kushindwa baada ya kukosekana kwa usafiri
Kamanda wa Polisi Bukoba, Revocatus Malimi amesema jeshi hilo linafuatilia mgomo wa madereva uliotokea kwenye manispaa hiyo kwa kile kilichodaiwa ni kupinga baadhi ya tozo zilizowekwa na manispaa hiyo.
Kwa mujibu wa Kamanda Malimi, Jeshi la Polisi linafuatilia kwa ukaribu ili kufahamu kuwa waliogoma ni madereva au ni wamiliki wa magari, na hivi karibuni jeshi hilo litatoa taarifa juu ya mgomo huo.
Akizungumza na www.eatv.tv Kamanda Revocatus Malimi amesema “taarifa ni za kweli ila jeshi letu linafuatilia lijue madai yao ni nini, pia tunahitaji kujua waliogoma ni wasafirishaji au ni abiria, na tumeambiwa ni mgomo baridi wa kutokutoa huduma.”
Mapema leo majira ya saa 3 asubuhi zilianza kusambaa taarifa juu ya kutokea kwa mgomo wa madereva wa daladala kutokutoa huduma za usafiri wakielekeza malalamiko yao kwa manispaa ya Bukoba.
Mbali na madai hayo pia inaelezwa kuwa madereva hao pia wanagomea juu ya ubovu wa miundombinu kwenye eneo ambalo wamekuwa wakiegesha magari yao.