Madereva, mafundi, matrafiki na wataalamu wa pikipiki tushauriane lini na wapi utatumia breki ya mkono wa kulia.

Freed Freed

JF-Expert Member
Jun 27, 2017
6,224
6,468
Habari zenu familia ya JF. Mada hapo juu yajifafanua. Kumekuwa na ajali nyingi za pikipiki humu nchini na hutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na matumizi ya sehemu mbalimbali za pikipiki. Je ni lini na wapi mwendesha pikipiki atatumia breki ya mkono wa kulia awapo barabarani? Ikumbukwe breki hii ni hatari sana na huogopwa na wengi. Jamani tushauriane maana breki hii ishaniangusha na kuniumiza sana. Tanbihi: Mods huu Uzi muiache muda mrefu kwenye safu za mbele kwani ni elimu mahususi ya USALAMA BARABARANI hivyo mchango wake utapunguza ajali za pikipiki na ulemavu ktk jamii.
 
breki ya mbele inashikwa wakati ambapo ushakanyaga breki ya nyuma pikipiki imepunguza mwendo,ikiwa speed unashauriwa uipige kwa kushtukiza kama ziara za wapenda kiki wa siku hizi,
 
kwa vyombo vya tairi 2 napenda sana kutumia breki ya mbele ya nyuma naigusa kidigo hasa kwenye kona na miteremko mikali. lakini katika pikipiki isaidiane na gia nzito mfano namba 3/2 au hata 1 bila kuzima injini wala kukamata clutch.

wengi hujikuta matatani kwa kuibinya kwa pupa na kwa nguvu zaidi hali pikipiki ikiwa neutral/clutched. hapa lazima paji la uso 'liubusu' udongo.

kujihami na mieleka ya pikipiki na gari kwa kiasi fulani usijihami kwa breki za kushtukiza unapokumbana na dharula kama shimo, mnyama, binadamu anayekatiza barabara ghafla. badala yake punguza gear/gia ili injini iwe nzito na kushusha rotation; kisha apply brake zote mbele na nyuma (pikipiki) kwa taratibu sana hali chombo kikiserereka. kwa pikipiki usilegeze usukani hata chembe, hata ukipanda matuta, kubali kung'ang'ania ili isikurushe.

kwa matokeo mazuri, dhibiti mwendo kasi wako lau uwe wa kadri na tahadhari ya misuko suko kama hiyo.

# nimetumia uzoefu. ninaendesha pikipiki toka 2003. zinanijaribu kiasi lakini si kwa madhara yasiyoepukika!
 
Back
Top Bottom