Madaraka ya Rais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba

...wee Sikonge....inabidi ufanye h/work yako sawa sawa kabla ya kubandika judgements zako humu.......kama una-claim Rais ana madaraka madogo...hebu tuwekee facts ulizonazo kuthibitisha claim yako

Kwa wote mliochangia,

Naona mnachanganya vitu vingi sana. Mie siyo mwana Siasa. Mie ninachosema ni kwa kuangalia mambo yanavyotendeka. Nchi nyingi huwa zinatabia za BOSS anagawa kazi kwa wadogo na kuwasukumia mambo machafu yote. Mambo yakikwama basi husema ni PM au Waziri ndiyo alifanya hivi. Tuangalie swala la RICHMOND au Kiwira. Kila mtu anaona kabisa kuwa ni Marais walishiriki kwa namna moja au nyingine. Lowassa alilivalia njuga hasa kwa kutoa AMRI kwa mdogo kwa wafanyaji wa chini. Sasa ukitaka ku-prove kuwa nani alifanya kosa utakuta kuwa SI RAIS wala SI PM. Ila ukweli kila mtu anauona wazi kabisa.

Mie ninachosema ni kuwa au PM awe kiongozi wa Mawaziri kwa kuwachagua yeye na SERIKALI yote kweli iwe chini yake. Au PM aondolewe na RAIS awe kiongozi wa SERIKALI yaani kwa maana nyingine RAIS AONGEZEWE MADARAKA. Hii sijui kama inahitaji kusoma KATIBA YOTE. Mie POINT yangu ni hiyo tu na hii ndiyo inayoendelea pale TANZANIA. Kuhani kama sivyo basi kweli mie HAZINITOSHI. Maana inaonekana huwa naona mambo KIVYANGU.

Kwa mawazo yangu ni kuwa kama RAIS au ATAONGEZEWA madaraka na yeye awe PM pia au KUPUNGUZIWA kama nilivyosema hapo juu, itaondoa utata wa NANI KAFANYA KOSA HILI kama la RICHMOND. Kila mtu anafahamu kuwa Helmet Cohl kwa kuchukua KICKBACK kutoka kampuni la mafuta la Kifaransa la ELF, aliubeba yeye mwenyewe MSALABA. Hakuweza kusema kuwa Ohh, ni mfanyakazi fulani kwani chama kilivyo, ni yeye tu anajibu mazuri na mabaya yote ya chama. Tanzania Kikwete anataka sifa zote ziende kwake na yakija mabaya hata kama ni yeye alitoa amri, ananawa mikono na kusema kuwa NI PM au Waziri au SERIKALI.

Sijui kama utakuwa umenielewa au bado utanituma zaidi kwenda kusoma katiba ambayo MILELE sintakujaisoma. Kama kuna mtu amenielewa na anaweza ielezea vizuri hii ISSUE basi ntashukuru.
 
Originally Posted by sikonge

Wana JF,
Mie nimekuwa nafikiri kuwa Rais wetu anapata shida na mafisadi kwa sababu MADARAKA aliyonayo Rais wetu ni kidogo sana. Ninaombi kwa Wabunge na Mawaziri waliopo hapa JF kuwa huko BUNGENI ibadilishwe katiba ili UWEZO wake uwe Mkubwa zaidi. Hiyo itasaidia sana kupambana na mambo mengi ambayo kwa sasa hawezi kwani KATIBA hamruhusu.

Quote:

Sikonge,

Katiba sasa hivi inasemaje?

Quote:
Originally Posted by sikonge

Kuhani ehh,
Mie niko huku kijijini ntaijuwa wapi KATIBA?

Sina swali lingine.

Kuhani,
Imesemwa kuwa HAKUNA SWALI LA KIJINGA, ila lipo JIBU LA KIJINGA.
Not person issue anyway.....
 
Mbona madaraka yanatosha tuu, issue ni kuwa na guts za kufanya maamuzi.Sijui una maana gani kusema hana madaraka?what will happen is once he opens the Pandora's box every evil will come out, including things that will implicate him and his allies.
 
Awe mwangalifu. Ndio maana baadhi yetu bado tunatafakari thread ya kudumbukiza humu!
 
Mujuni2,

Tatizo langu si kuwa HANA au ANAYO YA KUTOSHA. Mie ninachosema ni kuwa madaraka aliyonayo na jinsi katiba ilivyokaa inampa mwanya kufanya mambo kwa kutumia Migongo ya watu kama akina Yona, Lowassa, Pesambili nk. Kikiwaka basi unakuta Rais anasema hiyo ni serikali na yeye SI SERIKALI. Ila ukweli kila mtu ataujua kuwa SERIKALI ya Tanzania ni RAIS. PM yuko pale kama PAMBO TU. Hawezi hata kumuondoa kazi waziri wake kwani wote wameteuliwa na Mkuu.

Ninachosema mie ni kuwa KATIBA iwekwe au iandikwe kiasi kwamba ijulikane HASA nani KIONGOZI WA SERIKALI. Kama Rais ndiye anatauwa mawaziri basi ni yeye awe BOSS wao. Na kama ni PM aongezewe madaraka na kuwa KIONGOZI wa serikali na si BUNGE basi na iwe hivyo. Sasa hii ni kuwa au Rais APUNGUZIWE au AONGEZEWE MADARAKA ili kikiwaka mtu asikimbilie kujificha kwenye Mgongo wa PM au WAZIRI.

Kama Ufisadi unaofanyika sasa tungelikuwa na PM kweli kweli, basi ni yeye angelibeba Mzigo. Ona sasa ambavyo hata riport zikiandikwa za mabaya ya serikali zinakwenda kwa RAIS. Ila wakati huo huo kikifanyika kitu RAIS anasema muoneni PM. Huyu jamaa yupo kama KINGA. Sijui katiba inaseme ila kwenye PRACTICAL mie naliona hilo.
 
Last edited by a moderator:
Wana JF,
Mie nimekuwa nafikiri kuwa Rais wetu anapata shida na mafisadi kwa sababu MADARAKA aliyonayo Rais wetu ni kidogo sana. Ninaombi kwa Wabunge na Mawaziri waliopo hapa JF kuwa huko BUNGENI ibadilishwe katiba ili UWEZO wake uwe Mkubwa zaidi. Hiyo itasaidia sana kupambana na mambo mengi ambayo kwa sasa hawezi kwani KATIBA hamruhusu. Ikibidi basi hata cheo cha PM kife na ibaki Rais na makamu wake. Mbona UK wana PM tu bila Rais?
Walau kila BAYA tutajua nani alaumiwe.

Mkuu wenzio tunafikiria Rais apunguziwe madaraka wee unaongelea kumwongezea?haya sasa mie nakupa tipu,ili upitie katiba ili kujiridhisha na madaraka aliyonayo ukiacha yale yaliyoainishwa kwenye sheria mbalimbali.Nie yeye tu kuamua kutumia au la.please see the attachment.
 
Sikonge,

Katiba sasa hivi inasemaje?

Kuhani,

Nilikuwa na lengo jingine kabisa kuanzisha hii MAKALA. Naona NIMEJIINGIZA na UMENIINGIZA kwenye jambo ambalo siku zote nilikuwa silitaki. kwa mara ya kwanza nimejitahidi na kusoma KATIBA ambayo kumbe iko ndani ya JF. Ila Kuhani siku nyingine Mvutie tu mtu mistari miwili mitatu na kumpa kuliko kumuacha na UMBUMBU WAKE. Si watu wote wako sawa katika dunia hii ya dotcom. Jitahidi kuandika vingine ili kutoa chalenge kwa watu na siyo kuwakatisha tamaa. Anyway jibu lako kwangu limekuwa kama changamoto na kunipeleka kusoma hii katiba. Ila sidhani wengine wangelifanya kama mie. Kitabu cha THE GODFATHER, jamaa anaambiwa "Jifunnze kusema hapana inayosikika kama NDIYO.."

Sasa ukija kwenye KATIBA kwa kweli naanza KUJUA mengi sasa. Nafikiri KESI ya RICHMONDULI inatakiwa kuwa RICHBAGAMOYO. Kama ni UFISADI wote Tanzania unaofanywa na SERIKALI basi anayetakiwa kujibu ni RAIS. nashindwa kujua kwa nini tunaandama MAWAZIRI au WAZIRI MKUU wakati katiba inasema wazi kabisa kuwa KINGOZI WA SERUIKALI ni RAIS na yeye anateuwa WASAIDIZI tu yaani MAWAZIRI na PM...

Kuhani asante tena kwa challenge yako......... Kuanzia leo nimejua kuwa VITA yetu juu ya MAFISADI tunaonea watu wasio na makosa au wana makosa nusunusu na siku zote tunauacha mzizi wa fitina. Thanx yoo!!
 
Akili kweli ni mali kila mtu ana zake!, binadamu akishakuwa msanii hakuna dawa wala msaada! Eti rais wa Tanzania hana madaraka ya kutosha?
 
Wana JF,
Mie nimekuwa nafikiri kuwa Rais wetu anapata shida na mafisadi kwa sababu MADARAKA aliyonayo Rais wetu ni kidogo sana. Ninaombi kwa Wabunge na Mawaziri waliopo hapa JF kuwa huko BUNGENI ibadilishwe katiba ili UWEZO wake uwe Mkubwa zaidi. Hiyo itasaidia sana kupambana na mambo mengi ambayo kwa sasa hawezi kwani KATIBA hamruhusu. Ikibidi basi hata cheo cha PM kife na ibaki Rais na makamu wake. Mbona UK wana PM tu bila Rais?
Walau kila BAYA tutajua nani alaumiwe.


Ndugu Sikonge,

Inawezekana umeshajibiwa huko nyuma, ila kwa taarifa yako ni kuwa Rais wetu ana madaraka makubwa mno; ndiyo maana serikali yake haiwajibiki kwa wananchi. Tutakiwa tupunguze madaraka ya rais wetu ya kuteua na kuachisha kazi viongozi wa aina mbalimbali; kwa kufanya hivyo rais hatakuwa na mamlaka ya kuchagua rafiki yake na kuwapa madaraka ambayo baadaye anaona aibu kuwanyang'anya kutokana na urafiki wao.
 
Nafikiri hatujamuelewa sikonge.....nahisi anachotaka kusema yeye ni kuwa rais awe katika nafasi ya kuweza kubebeshwa kila zuri na baya linalotokea Tanzania.

Kwa sababu sasa kukitokea tatizo tunajibiwa kosa ni la PM na anapaswa kujiuzulu pamoja na waziri husika.

Yeye anachotaka kusikia ni kukitokea kashfa basi wa kujibu ni rais mwenyewe na mawaziri wake bila ya kuwa na buffer zone (PM) hapa kati kati.

Nafikiri amekosea kwa kusema rais aongezewe madaraka, .......ila yeye alitaka kitu kifanyike ili rais aweze kujibu shutuma za kashfa moja kwa moja.
 
Gaijin

Hata hivyo hiyo inarudi kule kule kwenye kumpunguzia madaraka rais siyo kumwongezea madaraka. Akishapunguziwa madaraka yakahamishiwe Bungeni, basi atakuwa analiogopa sana bunge. Sasa kule Bungeni nako kunatakiwa muundo mpya utakaopanua demokrasi kwa kumpunguzi madaraka Spika pia. Tukishatawanya madaraka kutoka kwa mtu mmoja mmoja na kuyafanya kuwa collective ndipo tutaweza kuwawajibisha viongozi wote.

Marekani sasa hivi wanalalamika kwa vile Bunge la Republican lilimkubalia Rais Bush kujilimbikizia madaraka na unaona matokeo yake.
 
Last edited by a moderator:
nafikiri hatujamuelewa sikonge.....nahisi anachotaka kusema yeye ni kuwa rais awe katika nafasi ya kuweza kubebeshwa kila zuri na baya linalotokea tanzania.
kwa sababu sasa kukitokea tatizo tunajibiwa kosa ni la PM na anapaswa kujiuzulu pamoja na waziri husika.
yeye anachotaka kusikia ni kukitokea kashfa basi wa kujibu ni rais mwenyewe na mawaziri wake bila ya kuwa na buffer zone (PM) hapa kati kati.
nafikiri amekosea kwa kusema rais aongezewe madaraka, .......ila yeye alitaka kitu kifanyike ili rais aweze kujibu shutuma za kashfa moja kwa moja .
Mtendaji mkuu wa serikali yetu ni waziri mkuu, unless mnataka tuiondoe hiyo nafasi ili rais awe nusu mungu sasa!
FMES na GAIJIN,
Kwanza niseme kuwa Gaijin umeileza hasa na hata KUNIKOSOA VEMA na kuandka vile ilivyotakiwa kuandikwa. FMES naomba usome ujumbe wa GAIJIN hapo juu na sahau nilichandika mie na hapo UTAELEWA nini hasa nilitaka kusema.

Rais wa Tanzania ni Mungu. Anaweza watuma mawaziri na hata PM kwa mdomo kuwa WAIBE PESA. Wakigoma anawafukuza, na wakikubali na wakashikwa basi anasema Hawa jamaa ni wezi na yeye anakaa pembeni. Hali ilivyo inatoa mwanya mzuri sana kwa hilo. Ukweli PM yupo pale kama picha tu. Hana chochote kwani yeye ni msaidizi wa Rais na Rais ndiyo BOSS wa serikali.

Sasa kwangu mie ni kuwa AU TUMUONDOWE PM na KIJULIKANE kimoja kuwa RAIS NDIYO FISADI na hakuna kujificha kwa mgongo wa PM(Lowassa). Au PM awe PM kweli kwa kuwa BOSS wa SERIKALI yetu na yeye ndiye achague Mawaziri. Hivyo kukitokea UFISADI ijulikane MOJA KWA MOJA kuwa ni SERIKALI na SERIKALI ni PM na Mawaziri wake.

Baada ya kusoma Katiba nimeona kuwa kweli Rais anamadaraka makubwa sana. Hivyo Ningeomba Mada hii iwe PM AONDOLEWE AU AONGEZEWE MADARAKA kwa kumfanya kuwa Mkuu za SERIKALI na Rais abaki mtu wa kuweka Sahihi kukubali YANAYOFANYWA na Bunge na mawaziri, kuchagua Mabalozi, kukagua miradi na Kikwete kwa hili anafaa maana anapenda sana kutembea na kuhamasisha.
 
@kichunguu umegonga juu ya mstari...

Rais ana madaraka utasema Mungu mdogo, lakini madaraka hayo hayo yanamziba yeye kubebeshwa lawama ya kashfa inayotokana na mawaziri wake aliowachagua kwa kuwa pia alimchagua na Waziri Mkuu.

Nafikiri Bunge na Mahakama yatakapopewa nafasi zake stahili, haya tunayoyaona sasa yangeliondoka......na kila kiongozi angefanya na kuujua wajibu wake kimisingi ya sheria.

Hhivi sasa sheria zipo, lakini kwa vile mahakama na bunge halina nguvu, ndio tunakuta rais na hata mawaziri wakati mwengine wanajivua lawama na kuwatupia watu waliowachagua.
 
Madaraka aliyonayo raisi anaweza kuagiza kichwa chako kipelekwe ikulu na kikapelekwa!
 
Madaraka aliyonayo raisi anaweza kuagiza kichwa chako kipelekwe ikulu na kikapelekwa!
Mchukia fisadi,
Kila Rais ana uwezo huo. Ila tofauti ni kwamba Kwa Tanzania atakayebebeshwa Lawama ni PM au Waziri wa Mambo ya Ndani au Boss wa Polisi. Rais atajianya hajui kitu kabisa na Masikini wa Mungu mnamuonea wakati yeye ni CHAGUO LA MUNGU.
 
Mchukia fisadi,
Kila Rais ana uwezo huo. Ila tofauti ni kwamba Kwa Tanzania atakayebebeshwa Lawama ni PM au Waziri wa Mambo ya Ndani au Boss wa Polisi. Rais atajianya hajui kitu kabisa na Masikini wa Mungu mnamuonea wakati yeye ni CHAGUO LA MUNGU.
Sikonge ni kweli. Ndiyo maana kama walivyokuwa wanalalamika Kenya, hata sisi shida iko hapo hapo. Mtawala wetu siku zote anawatumia wasaidizi wake kama remote. tunayoyaona ujue ndio uamuzi wake yeye binafsi pia.

Ukisikia ufisadi ujue is part of it, ndiyo sababu hachukui hatua kwa wahusika hata kama kuna ushahidi 100%.

Tunaitaji mabadiliko makubwa katika katiba yetu. Otherwise hata kwenda ikulu watu watafika mahala wata-force maana ukifika uko your everything.

Tutafute mabadiliko kwa kila namna.
 
MAONI YA KAFULILA KUHUSU MAMLAKA YA RAIS MCHAKATO WA KATIBA MPYA:

Jana wakati nachangia kwenye mjadala wa wabunge wote kuhusu namna ya kuenenda katika mjadala wa katiba nilijaribu kuweka msimamo wangu wa ujumla kuhusu misingi ya kufanya mjadala huu ufike salama na kufikia matokeo tunayotaka kama Taifa. Msingi huo ni Trust(imani). Hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sasa imepunguza kiasi kikubwa cha kuaminiana. Na hii sio Tanzania tu bali nchi nyingi masikini duniani. Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ndugu Ban Ki Mon akifungua mkutano wa Bunge la Dunia Oktoba 15, 2011 alisema; TATIZO KUBWA KWA NCHI MASIKINI DUNIANI SASA SIO NAKISI YA BAJETI (BUDGET DEFICT) BALI NAKISI YA IMANI YA UMMA KWA WATAWALA (TRUST DEFICIT) NA UFUMBUZI WA TATIZO HILI NI UWAZI NA WATAWALA KUKUBALI MAMLAKA YA UMMA...

Tatizo la umma kupoteza imani kwa watawala ndio msingi hata wa kuhitaji katiba mpya, maana zamani enzi za Mwalimu Nyerere Katiba ilikuwa mbaya kuliko tuliyonayo leo, ilifika mahala Mwalimu Nyerere akasema hii katiba inamtosha Rais kuwa Dikteta lakini kwakuwa Umma uliamini kwa waliopewa madaraka hoja ya katiba haikuwa agenda..


Huu ndio msingi wa msimamo wangu kusisitiza umuhimu wa kupunguza mamlaka ya Rais katika mchakato huu.
Baadhi ya maeneo ambayo nashauri yatazamwe ili kupunguza mamlaka ya Rais ni pamoja na;


KUHUSU TUME

1. Ibara ya 5 ya muswada inaeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kushauriana na Rais wa Zanzibar ndiye mwenye mamlaka ya kuunda Tume. Mimi nashauri Rais apendekeze majina ya wajumbe wa Tume yatangazwe gazeti la Serikali uwepo muda wa Umma kutafakari majina hayo na kisha yapitishwe na Bunge. Pia kwenye kuwaondoa isiwe kama inavyotamkwa kwenye ibara.........kwamba wakifanya makosa wanaondolewa bila mchakato mgumu wa kumwondoa. Tuweke mchakato mgumu kama ilivyo kwa majaji, kwamba kumwondoa mjumbe Rais atoe pendekezo na kiwepo chombo cha kupitia pendekezo hilo ili kuthibitisha uamuzi wa Rais kumwondoa mjumbe husika. Tukifanya hivi tutakuwa tumeihakikishia Tume mamlaka na Uhuru wa kutosha kuweza kufanya kazi bila hofu ya aliyewateua. Lakini kubwa zaidi utaratibu huu utaijengea Tume uhalali wa kisiasa (political legitimacy) kwamba Umma una imani na Tume. Hiki ni kitu muhimu sana.


2. Ibara ya 8(1) Hadidu za rejea kutolewa na Rais kwa kushauriana na Rais wa Zanzibar. Hapa panaweza kuwa na hofu ya Rais kuamua matokeo ya maoni kutokana na mfumo wa hadidu atakazotoa. Hadidu za rejea ni kitu kikubwa sana kwenye kuamua matokeo ya kura ya maoni. Hivyo ni muhimu Hadidu za rejea ziwe sehemu ya sheria kabisa kuondoa hofu hiyo. Hadidu za rejea zikiwa sehemu ya sheria sio rahisi kuchezewa na mamlaka yoyote bila utaratibu wa sheria kufuatwa.



SEKRETARIET YA TUME

Ibara ya 13(2) Rais atateua Katibu wa Sekretarieti ya Tume. Hiki ni chombo cha kiutendaji chini ya mamlaka ya Tume. Kama Tume itapatikana kwa namna niliyoeleza hapo juu, nashauri sekretarieti ya Tume iteuliwe na Tume yenyewe kwa kuzingatia vigezo ilikuifanya sekretariet iwajibike kwa Tume na kuepusha nguvu na mamlaka za Rais katika shughuli za utendaji wa Tume. Hapa nazingatia uzoefu wa Sekretarieti ya Tume ya Profesa Shivji ambapo analalamikia uzembe kutokana na Tume kukosa mamlaka ya kuidhibiti.



Ibara ya 13(5) Inaelezwa kuwa wajumbe wa Tume na Sekretarieti watalipwa na Waziri ambaye ni mteule wa Rais kadiri atakavyo amua kulingana na sheria na kanuni za nchi. Hapa nashauri viwango na utaratibu wa malipo viwekwe wazi, na kuondoa uwezekano wa serikali kuamua mwelekeo wa kiutendaji wa Tume kwakuwa majaaliwa ya utendaji yamefungwa mikononi mwa wizara. Ni muhimu uwepo mfuko maalumu kwa kazi hii kuepusha visingizio vya sababu za kibajeti kuathiri utendaji wa Tume. Hapa tunao uzoefu mzuri wa nchi ya Uganda ambapo Serikali iliyumbisha mchakato wa katiba kwasababu za kibajeti kwa malengo ya kisiasa.


Ibara 18(1). Inasema baada ya Tume kukamilisha kazi yake itawasilisha ripoti kwa Rais na Rais wa Zanzibar na Ibara ya 18(2) inasema Baada ya kushauriana na kukubaliana na Rais wa Zanzibar na baada ya kukamilisha majadiliano kuhusu masuala ya kisera, taratibu na kiutendaji, Rais atamwagiza waziri kuwasilisha muswada wa Katiba katika Bunge la Katiba na Ibara ya 26(2) kinasema baada ya kuvunjwa Bunge la Katiba bado Rais anayo mamlaka ya kuliitisha Bunge la Katiba lenye wajumbe wale wale siku zijazo kwa ajili ya kutunga masharti ya katiba kabla ya kuzindua katiba inayopendekezwa kwa lengo la kuboresha masharti yaliyomo kwenye katiba inayopendekezwa.
Haya ni maeneo yanayo onesha mamlaka ya Rais kuamua katiba iwe ya namna gani. Kwanza Bunge likipitisha katiba inayopendekezwa haifai Rais tena aboreshe na badala yake katiba inayopendekezwa inapaswa kupelekwa kwa wananchi. Pili, Baada ya Tume kukamilisha kazi yake haipaswi kuwasilisha ripoti kwanza kwa Rais, inapaswa kwanza iwasilishwe kwa wananchi kwa kuchapwa kwenye gazeti na uwepo muda umma kujiridhisha kama hicho kilichochapwa ndio maoni yao?.. na ndipo ripoti akabidhiwe Rais.. Mwenyekiti wa Tume ndiye anaepaswa kuwasilisha ripoti ya Tume kwenye Bunge la Katiba badala ya Waziri..Hii ni kwasababu ripoti sio ya serikali ni ya tume lakini pia Mwenyekiti wa Tume ndiye aliyeshiriki mchakato wa kukusanya maoni hivyo anao uwezo na mamlaka ya kujibu hoja za wabunge wa Bunge la Katiba kuhusu ripoti yake.


Ibara ya 20(1) Inasema Rais ataunda Bunge la Katiba, Pia 20(4) Rais ndiye atakayeteua wajumbe 116 kutoka Taasisi za kidini, asasi zisizo za kiserikali, vyama vya siasa vilivyo na usajili wa kudumu, taasisi za elimu ya juu na makundi yenye mahitaji maalumu katika jamii.
Hapa kwanza nashauri tuondoe kabisa dhana ya Rais kuunda Bunge la Katiba kwa ujumla wake. Pia kama haiwezekani kuendesha mchakato wa uchaguzi kupata wabunge wa Bunge la katiba kwa nchi nzima, bado wajumbe waliobanishwa kutoka taasisi tajwa hapo juu wasiteuliwe na Rais moja kwa moja, badala yake taasisi tajwa zipewe mamlaka ya kuchagua wajumbe wa kuwakilisha taasisi husika kwenye Bunge la Katiba. Hii itazipa mamlaka taasisi hizo kuamua mtu sahihi ndani yao badala ya kuamuliwa na Rais.


Mwisho mchakato wa kura ya maoni kwa mujibu wa muswada utaendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Lakini Umma hauna imani na Tume ya Uchaguzi kutokana na namna inavyo undwa na kufanya kazi. Tume tuliyo nayo bado inaonesha mamlaka ya Rais kuamua, hivyo ni muhimu kupata Tume mpya itakayopata uhalali wa kisiasa kuweza kusimamia kura hiyo ya maoni kuondoa uwezekano mkubwa wa wananchi kupinga baadhi ya matokeo kwa kigezo cha imani ya umma kwa Tume.



HAYA NI BAADHI YA MAENEO YANAYOPASWA KUREKEBISHWA KUPUNGUZA MAMLAKA ZA RAIS NA KUONDOA MCHAKATO WA KATIBA MIKONONI MWA DOLA KUWA MIKONONI MWA UMMA.



SOURCE: GAZETI LA DIRA
 
Back
Top Bottom