Madaktari wote waliogoma kufukuzwa kazi na utumishi!

hii nchi tunaipeleka pabaya sasa,kwanini kila siku migomo na mogogoro hawa ma Dr. tutauuwa wangapi kwa mogomo,athari ya migomo ya migomo kama ni mbaya sana.
 
Kwa mujibu wa chanzo muhimu katika wizara ya afya, Serikali imejiandaa kuchukua hatu kali kwa madaktari wote waliogoma ifikapo kesho Ikiwa ''Ni pamoja kuwafukuza kazi na utumishi'' baada ya juhudi za Serikali na za Kimahakama ''KUTOHESHIMIWA''. Pamoja na hatua hizo pia taratibu za kuandaa madktari mbadala toka taasisi nyingine za Serikali ikiwa ni pamoja na uwezekano wakupata msaada wa dharura wa Madaktari toka mojawapo ya Nchi za Afrika Mashariki, zinaendelea vizuri. Aidha ulinzi nao unaendelea na utaendelea kuimarishwa katika sehemu na maeneo mbalimbali.

Kauli hii bila shaka ina underline tamko la Serikali leo Bungeni kuwa '' LIWALO NA LIWE''
Je wagonjwa wetu itakuwaje??
 
sasa hao madaktari mbadala wakija ndo watwaboreshea mazingira ya kazi? au hao mbadala wao hawajali kufanya kazi bila vitendea kazi? na hao mbadala watakuwa wanawasubiri wao kwa ajili ya kutatua matatizo yao? mbona aliyeongea inaonekana kaongea kwa jazba na vitisho vya kiuoga namna hiyo? Sidhani kama ni busara kuacha hili tatizo bila kutatuliwa na kukimbilia solution ya mda mfupi. Inabidi serikali iwe makini sana na maamuzi yake kwani hakuna hata siku moja kitu chochote duniani kimefanikiwa kwa mabavu na wananchi wake, sanasana wanazidi kujijengea maadui kwani hata hao madaktari wana wapenzi wao huko mitaani wakiamua kuungana sidhani kama serikali itashinda nguvu ya umma.
 
Hakuna cha kuandaa madaktari mbadala wala kupata msaada wa madaktari kutoka east africa, madaktari/manesi wote
wakiamua kugoma serikali ni lazima inywee...

Mkuu inaonekana ujui nguvu ya dola weye!
 
Wachina wanaweza kuichukua hospitali nzima na hao wafanyakazi kulipwa na serikali yao ya uchina ,kuna madaktari kama milioni moja hawana kazi nchini China.

Siyo kweli. Hakuna nchi hata moja ambayo ina madaktari wasio na kazi labda kama hawataki kuajiriwa. China ina upungufu wa madaktari, na inawategemea zaidi madaktari wa jadi kuliko madaktari wenye western medicine profession ambao ndiyo tunayoitumia Watanzania.
 
Watanzania acheni uoga,na hili nalilekeza kwa madaktari wetu,ni hi kama kweli ni madaktari wa ukweli sio kama JK,nawaomba msihofu kwa lolote,na wala msifikiri hakuna maisha nje ya ajira za serikalini,maisha yapo tu na kama ingelikuwa hivyo basi ni watu wngi sana wangelikuwa wameshakufa,ajira zipo kupita kujiajiri au kuajiriwa nje ya serikalini.msiogope juu ya haya maisha na hii ni mwanzo tu kwamba safari ya ukombozi ndio imeeaza,na kwenu niynyi wasomi sitegemei kama mtatishika na kufukuzwa au vyovyote,maaan hawana maana hawa mmemsikia Pinda amesema liwalo na liwe.hiyo ipokeeni na muikabili.
Umoja ni nguvu
 
Wanashida gani hawa mafisadi wakati hata wakiugua mafua tu wanadandia pipa na kutua ughaibuni kwa matibabu?

Wenye shida ni Mi na wewe mrusha uzi huu!

Ila hakika nawaambia ya kwamba mwisho wao waja hawa mafisadi!

Hili HALIKUBALIKI KAMWE KWA TULIKOFIKIA KWA SERIKALI DHAIFU KAMA TULIYONAYO.
 
Inapokuja ishu ya Job Security wabongo huwa hawaaminiki kabisa, kusalitiana dakika yoyote. Job Security ndio inamfanya Nape anageuka vuvuzela, sitashangaa kama itawafanya madaktari wasitishe mgomo. Hapo Pinda kawatishia njaa madaktari, tuone ubavu wao.

Kumbe nawewe umeona, sasa tusubiri kuona nani atalinda chakula chake ili kisiliwe na mdudu anayefahamika kwa jina la SEREKALI DHAIFU.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
 
Issue ya madaktari ni ngumu sana kama serikali inadhani kuwafukuza ndio njia muafaka, kabla ya kutekeleza uamuzi huo iende kujifunza hapo Kenya walipotangaza kuwafukuza kazi walifanikiwa kwa kiwango gani? Mwisho wa siku waliwarudisha kazini wote bila masharti yoyote.

Hata uingereza juzi tu madaktari wamegoma na hatukusikia serikali huko ikitangaza kuwafukuza ama kwenda mahakamani. Walikaa kwenye meza ya mazungumzo na kuyamaliza.
Serikali yetu ijifunze kuzungumza na kuwa wakweli kutekeleza makubaliano, vinginevyo migomo hii haitakwisha kamwe hata kama watatumia nguvu nyingi na vitisho kiasi gani.

Mkuu Nyahende Thomas usilinganishe Kenya au Uingereza na Tanzania. Haya mawazo ya madaktari ndo yalinifanya this time nisiwasapoti kabisa, it's narrow thinking and lacks objectivity. Hizo nchi unazolinganisha nazo uchumi wake uko juu kinoma. Kwa taarifa yako budget ya Kenya innajitosheleza kwa 100%, sema tu wanataja 90-95% ili wanaendelee kupata misaada toka nchi za nje. Tanzania tunajitegemea kwa 60% tu, forty zote ni misaada ya wahisani. Kwa mantiki hii huwezi kumlipa daktari wa TZ sawa na wa Kenya au Rwanda wereva. Pigeni kazi acheni ubinafsi madaktari, yaani mnataka keki yote ya nchi mle peke yenu? Yaani safari hii mnachekesha hadi wananchi wa kawaida wanawaona hamna maana ktk jamii.

Muhimu tupiganie rasilimali za nchi zilete mchango mkubwa ktk kukuza uchumi wa nchi yetu, tupigane na ufisadi ili kuokoa pesa zinazonufaisha watu wachache. Then, uchumi ukipanda logically ina make sense kudai mishahara mizuri.
 
Watanzania acheni uoga,na hili nalilekeza kwa madaktari wetu,ni hi kama kweli ni madaktari wa ukweli sio kama JK,nawaomba msihofu kwa lolote,na wala msifikiri hakuna maisha nje ya ajira za serikalini,maisha yapo tu na kama ingelikuwa hivyo basi ni watu wngi sana wangelikuwa wameshakufa,ajira zipo kupita kujiajiri au kuajiriwa nje ya serikalini.msiogope juu ya haya maisha na hii ni mwanzo tu kwamba safari ya ukombozi ndio imeeaza,na kwenu niynyi wasomi sitegemei kama mtatishika na kufukuzwa au vyovyote,maaan hawana maana hawa mmemsikia Pinda amesema liwalo na liwe.hiyo ipokeeni na muikabili.
Umoja ni nguvu

jigoku usiwape moyo bure (hapo pekundu). Hivi unajua kuna madaktari wangapi Tanzania? Halafu unajua kuna private hospitals ngapi Tanzania, na unajua zina uwezo wa kuajiri madaktari wangapi?.

Kama una kumbukumbu nzuri, miaka ya 90 serikali ilistopisha ajiri zote, nadhani uliona madaktari, manesi kibao walivyokuwa wamejaa mitaani bila kazi.
 
Wacha kuota ndoto za jioni wewe! Suluhu nini kila Dr mmoja serikali imlipe milioni 13 kwa mwezi?

sasa Ritz mie siafiki hiyo mil 13..kwa serikali ipi walipwe pesa yote hiyo..
Lakini kuna madai mengine kama ya hali bora za maeneo ya kazi hayo serikali haiongelei..suala la mshahara 13mil..hapana its too much.
 
dola dhaifu nayo unaiita dola?

Haya basi subiri uone udhaifu wake! Hivi unakumbuka mwaka ule madaktari wa muhimbili walivyogoma (Zakia M akiwa waziri wa afya) serikali iliwafanyaje?

Unajua mkuu unapokosa back-up ya wananchi (kama ilivyo safari hii kwa madaktari) ni bora ukubali kile unachoambiwa na serikali.
 
jigoku usiwape moyo bure (hapo pekundu). Hivi unajua kuna madaktari wangapi Tanzania? Halafu unajua kuna private hospitals ngapi Tanzania, na unajua zina uwezo wa kuajiri madaktari wangapi?.

Kama una kumbukumbu nzuri, miaka ya 90 serikali ilistopisha ajiri zote, nadhani uliona madaktari, manesi kibao walivyokuwa wamejaa mitaani bila kazi.
kelele za nini mwehu wewe! si usubiri watimize km wanaubavu huo wa kufukuza madk wote! sijui manesi na watalaam wengine unawatoaje kwny mgogoro huu, miaka ya 90 siyo leo!
 
mbona hata mgomo uliopita walisema tunafukuzwa kazi?

Dr.Chichi kumbe bado hujaona tofauti ya mgomo uliopita na huu wa sasa! Ule wa mwanzo hakukua na amri ya serikali, hivyo serikali ingewafukuza kazi ingebidi iwalipe, which is another burden to the gvt. Safari hii imecheza tricky ambayo wengi wenu hamjaijua, ukifukuzwa hupati chochote maana umedharau amri halali ya mahakama, chezeya dola weye!

Halafu mkuu mjifunze kusoma alama za nyakati. Safari hii hamna back-up ya wananchi, watu wengi hawako upande wenu kwa sababu mmekuwa too demanding and not considerate!
 
Zile billion 300 zingekuwa haziwekezwi Swiss na wajanja nafikiri mishahara isingekuwa tatizo!!

watu sita tu wana own 303 bn ni wastani wa kila mtu ana own shs bn.50.5!! haya ndio yanakatisha watu tamaa, doctor amepiga book ngumu na anafanya kazi ngumu ya kutumia akili muda wote unamlipa 300,000/- wakati mbunge ambaye ni form iv au std 7 hana profession yoyote anasinzia na kudondokwa udenda bungeni unamlipa 10,000,000 kwa mwezi acheni wagome na sekta nyingine pia tugome ili kuwepo na usawa kwenye keki ya taifa!
 
Dr.Chichi kumbe bado hujaona tofauti ya mgomo uliopita na huu wa sasa! Ule wa mwanzo hakukua na amri ya serikali, hivyo serikali ingewafukuza kazi ingebidi iwalipe, which is another burden to the gvt. Safari hii imecheza tricky ambayo wengi wenu hamjaijua, ukifukuzwa hupati chochote maana umedharau amri halali ya mahakama, chezeya dola weye!

Halafu mkuu mjifunze kusoma alama za nyakati. Safari hii hamna back-up ya wananchi, watu wengi hawako upande wenu kwa sababu mmekuwa too demanding and not considerate!

madaktari ni badly needed south africa, botswana, Namibia, Ethiopia na nchi nyingi za kiarabu wala tishio la kuwafukuza sio issue, profession ya udaktari sio ualimu ambao hata failures wanafundisha watoto wetu!!
 
Back
Top Bottom