Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,848
- 2,669
Katika gazeti la mwananchi la leo kuna picha ya daktari mstaafu ambaye serikali imemuajiri kwa mkataba maalum. Watakuwa wengi. Hawa wastaafu wanatumika kuziba pengo la madaktari waliogoma. Ni halali kwao kufanya hivyo? Haikuwa kwao sawa kuwaunga wenzao mkono katika kudai maslahi yao? Au kwa vile wao enzi zao zimepita na hawana cha kupoteza. Labda kwa wakati fulani walishiriki kuihujumu Muhimbili na hospitali zingine kwa kuiba wagonjwa na madawa na vifaa vingine wakahamishia kwenye zahanati zao. Nafikiri ilikuwa wakati muafaka kwao kuwaunga mkono wenzao. Serikali kitu ambacho ingeweza kufanya ni kwenda huko makambi ya jeshi na kuwachukua madaktari wanajeshi kuja kutumika kwenye hiki kipindi cha mputo