Madaktari wapigwa stop kufanya kazi private

Hospitali+by+Beda+Msimbe.jpg

Wamelazwa, wakipatiwa dripu ya maji ktk dispensari picha na Beda Msimbe source:mjengwablogspot.com.
 
Bwana mkubwa,

Ule mchezo wa daktari wa kumwandikia kipimo mgonjwa, na kumuelekeza kafanyie hospitali fulani(kwa mkyuba sijui wapi) halafu mnaenda kuvuta mshiko kulingana na wagonjwa mliyowaandikia waende huko toka hospitali za serikali mnazofanya sio mzuri ni njaa ya wazi. Pia mgonjwa unaenda hospitali ya serikali daktari anakuambia ukitaka kuniona vizuri njoo hospitali fulani au operesheni mazingira haya ya serikali hayafai. Kwa kweli hicho ndicho kinachonikera kwa madaktari wengi wa serikali, eti kipimo hiki kafanye hospitali fulani. nimeshuhudia wiki hii mtu kaambiwa picha hiyo ya X ray haifai ulipopigia nenda kafanyiwe sehemu fulani. Hata kama ni njaa sio kihivyo, uhai muhimu kwanza. Kwa nini msitafute namna ya kupata hela ya halali kama fast track n.k? Wagonjwa twaenda vile tunashida tu.

Nawakilisha, na ninaunga mkono hoja ya serikali hamna kufanya sehemu mbili. Wafanye kama watakuwa waaminifu huko walipo serikalini.

Naipongeza serikali kama kweli wamechukua hatua hii. Naungana na wewe mti-mkavu kupinga tabia ya madaktari wa serikali kutumia muda mwingi kwenye hospitali binafsi kuliko kule walikoajiliwa na serikali; huo ni ufisadi ambao ni kinyume na kiapo chao cha udaktari wao!! Siku hizi watu wengi wanaugua cancer za aina mbali mbali, lakini wakienda Ocean Road hospital huduma haziridhishi na madawa ni duni lakini huambiwa waende hospitali binafsi huko Mwenge ambako madaktari na manesi wa Ocean Road huhudumia; na kule huduma ni bora na hata madawa hupatikana ingawa kwa gharama kubwa ambazo ni matajiri tu ndio wanaozimudu!! Mbaya zaidi ni kwamba viongozi wa Ocean Road hospital ndio wamiliki wa hospitali ya mwenge. Kwamtindo huu serikali imechukua hatua thabiti kabisa.
 
Mishahara tu haitoshi kuwa suluhisho la moja kwa moja...!!! Hivi maafisa TRA wanapata salary kiasi gani..lkn mbona wanaendelea kutokuwa waaminifu?Mijizi hakuna mfano...!!!

Hata ma-dr leo wakipewa 2-3M bado wapo watakaokuwa si waaminifu...Labda waulizwe ni salary kias gani kinawatosha?...

Tukitaka tulinganishe Maisha na Nchi zingine kuna wakati tutashindwa...itakuwa just kuwaongopea wananchi.

Tuna Tatizo la Mfumo Mzima, ambalo kama halitarekebishwa Hali itazidi kuwa mbaya. Mfumo huu ni uwajibikaji wa kila mmoja. Leo hii km upo private huwezi ongezewa salary kienyeji, lazima ufanyekazi ipasavyo...Sasa Hawa madr..km basi wafanye vizuri ile kazi yao, then wananchi waone na serikali ione then hapo mnaweza pata watetezi...lkn kwa utaratibu huu kufanyakazi Hamtaki, then mnataka salary kubwa inakuwaje?

hao Ma-dr kwa muda mchache wanaofanyakazi, basi wafanye vizuri basi alau hayo masaa 2 wanayaoamua kukaa kazini...!!!
 
Mti mkavu,
Nakuunga mkono sana.. Hali ilifikia kuwa mbaya sana kwa wagonjwa nchini na hakika wanaotetea Madaktari wa serikali kufanya kazi private wanashindwa kuelewa mfumo mzima ulivyokuwa mbovu. KJama hawa madaktari wanataka kuendesha biashara zao binafsi wafanye kazi huko full time na sio kuchukua wagonjwa wa hospital za serikali, kuwaghiribu kisha kuwalipisha gharama kubwa ktk Hospital zao binafsi ati ndiko kwenye huduma nzuri..The same person atakuwaje anahudumia vizuri kwake na siko alikoajiriwa?

Hapa hawa Madaktari wanachezea maisha ya binadamu kabisa, na kulipwa mishahara midogo sio sababu ya kutoa huduma hafifu ktk hospital za serikali..,mshahara mdogo acha kazi fungua yako na ufanye kazi vizuri sio kwenda Muhimbili ili mradi upate kuiba wateja baada ya kazi. Swala la walimu na viongozi ni swala linaloweza kutazamwa pia lakini kwa uangalifu zaidi ya madaktari kwa sababu hawa madaktari wamefikia kucheza na Uhai wa watu.

Hawakatazwi na mtu yeyote kufungua biashara zao binafsi na kutotegemea mshahara wa serikali lakini unapoajiriwa na serikali kisha muda mrefu unautumia ktk hospital yako hii inapunguza huduma za hospital za serikali na matokeo yake kila hospital ina pungukiwa madaktari. Yanayotokea leo hospitali za serikali hayatokani na ukosefu wa Madakari au madawa isipokuwa ni UFISADI wa Madaktari unaoharibu kabisa huduma nzima ya Afya nchini..

Kwa uhakika huduma za Hospital za serikali zmepungua kuliko wakati wowote toka tupate Uhuru.. Wanawake wajawazito wanakugfa kuliko wakati wowote, Malaria, Kufia kikuu ni magonjwa yanayotibika lakini yanaua kuliko hata Ukimwi.

Wanataka ushindani wafungue za kwao na watafute wateja na sii kuwachukua wale wasio na jinsi na kuwahadaa kwa maradhi yasiyoponyeka isipokuwa ktk hospital zao. Halafu sii kweli daktari anaweza kukutibu vizuri ktk zahanati yake kuliko Muhimbili hali kule hana vifaa vya kutosha, huu ni wizi mtupu na maranyingi wanaiba hata madawa na vifaa toka hospital za serikali.

Ikiwa shule au mwalimu sii mzuri unaweza kuondoka sahule hiyo at least mhudumiwa ana choice lakini sii ktk Maradhi. Hao viongozi wetu kufanya biashara ni swala la muda tu...Hili linaangukia ktk miiko na maadili ya viongozi (Siasa) na kama sikosei JK tayari alikwisha piga marufuku viongozi wa serikali kujihusisha na Biashara.. Aliwaomba wachague aidha siasa au Biashara, hivyo kama unamjua Kiongozi yeyote ngazi ya juu serikalini akijihusisha na biashara nadhani bila shaka huyu kiongozi anavunja sheria..Mahakama ya miiko na maadili imeshafunguliwa hivyo ni swala la ku report tu mtuhumiwa.
Tatizo umejisahau. keki ni ya wote siyo TRA, BOT na Wanasiasa tu. Wao mbona hawalipwi kidogo ili wakatafute kazi kwingine kama unavyopendekeza kwa madaktari na walimu? Huna hoja. Nchi ni yetu sote. Mkijipendelea na sisi (madaktari, walimu) tutajipendelea fullstop. Wala huwezi kututisha maanake una kura moja tu kama mimi na tuna haki sawa mbele ya katiba yetu.
 
Pamoja na hayo yote ni siasa chafu na uongozi mbovu wa serikali, just imagine Docta moja kusoma hapa nchini degree ya kwanza mpaka aitwe Dr miaka 5. gharama atakazo tumia si chini ya milion 40,000,000/= halafu serikali inamwajiri kwa mshahara wa tsh, 889,000/= kwa mwezi, ukitoa makato yote take home, 500,000/= kama alikuwa anapata mkopo waserikali anapaswa kukatwa tena, hiyo ni moja,
pili, iliupate masters hunapaswa kuenda tena miaka 4 chuo, then, ulipwe mshahara wa tsh, 1,000,000/= hadi 1,700,000/= kadiri mshahara unavyoongezeka makato nayo yanaongezeka, sasa angali umesoma miaka 9, hujahesabu ya sekondari, mshahara ndo huo,
mfanyakazi wa TRA, mwenye diploma acha degree, analipwa mshahara wa tsh 2,000,000/= chuo kasoma miaka 3.daktari pamoja na kwamba kasoma miaka mingi, amepoteza muda mwingi, anafanya kazi kwenye mazingira hatarishi, kwa kupata maambukizi toka kwa wagonjwa, analipwa hivyo,atapataje moyo wakufanya kazi kwa bidii!

saa zingine daktari anamwambia ngonjwa kapimwe pale si kwamba anahitaji kitu, utakuta hospitali haina vifaa vyakupimia ila daktari anahitaji kujua shida ya mgonjwa wake, sisi tunaanza kulalamika ohh wanataka hongo, jamani, tuwaonee huruma, ndoyo labda kunawahivyo lakini si wote,
afadhali hata huyo anayekutuma ukapimwe je angekuandikia tu dawa,ukaenda kumeza madawa hujui unaumwa nini! ndiyo bora,

ndugu zangu watanzania kwa mliokuwepo 2005 mnakumbuka madaktari walivyo goma muhimbili, kwaajili ya maslahi duni, wanasiasa walipiga kelele, sana, lakini chakushangaza walipoingia mbugeni tu cha kwanza, wanataka mishahara mikubwa kweli, hivi wanafanya kazi gani ngumu kule njengoni, mbuge haijalishi amesoma au la mshahara milion 7. posho kwa siku 160,000/= travel allowance 80,000/= kwa kazi gani ngumu wanayo fanya? kusogeza kiti mbele na nyuma, na kupiga, na kulala bungeni, embu jaribu kulala wewe kazini, kama hujanyukwa viboko na diwani wa darasa la saba, na midegree yako.

watanzania serikali yetu inadharau wanajipenda wenyewe na familia zao, wanajua kabisa mshahara huo si haki kabisa, lakini yanini kwani wao na familia zao wanatibiwa nje, pesa zipo, hospitali iwe na vifaa isiwe nayo, iwe na madawa isiwe nayo, yakazi gani wakati anadaktari wake nje, matibabu yake marekani, uswis, shida gani! lakini kuwa tungia wenzao misheria na kutamka hawajambo.

punda unaweza kumkokota mtoni lakini ujue hautamlazimisha kunywa maji, Dr anaweza kukaa kituoni asubuhi mpaka jioni lakini asitibu vizuri, huko private tutakwenda wenyewe hata bila kuambiwa, maana pale serikalini unaweza kwenda asubuhi utapata huduma lakini wadawa hakuna sanasana utaambulia parasetamo.

mimi nawaomba wa Tanzania, tuwashinikize hao wanasiasa wawajali wafanyakazi wapewe maslahi nzuri iliwafanye kazi kwa moyo, vinginevyo tutaumia sisi walala hoi na familia zetu, tuwachague viongozi wanaojali wananchi wao, kwa kuwawekea wafanyakazi,wenye nia na moyo wa kazi,

serikali iwalipe wafanyakazi mishahara mizuri, Watanzania tusikubali kunyanyaswa huduma ni haki yetu, uwezo wa kupata huduma nzuri tunao ila uelewa ndogo wa serikali yetu, nakuelezeni cheza na mtu yeyote duniani lakini si madaktari si kwamba na wafagilia, hata serikali yenyewe inajua hilo,

mimi wala si shangai kwa maana sisi wapiga kura ndo tunayafanya haya, kiongozi ameongoza miaka 20, jimboni hakuna maji, hospitali halina madawa, wafanyakazi wamekimbia, sisi tunaendelea kumchagua tu, sasa tunaanza kuwalalamikia madaktari wafanyeje wafenjaa. na sasa hivi wamegundua, wakisha maliza mafunzo kazi nje, au kwenye siasa kunakolipa, ingependeza kama mtu ni mwl akienda kwenye siasa ahame na mshahara wako uleule wa ualimu, au daktari, ambaye hana taaluma alipwe kima cha chini cha sekta binafsi 135,000/= kwa mwezi, tuone kama wangeng'amg'ania huko, lakini sasa wao ndo wanao panga kila kitu.
 
kama suala ni hilo basi lisichague taaluma, kama ifuatavyo
1. mbunge asiwe mwenyekiti wa bodi wala mfanyabiashara wala mkulima
2. walimu vyuo vikuu wasiwe na vyuo kadhaa vya kufundisha wala wasifanye consultant work kokote
3. wahasibu wasifanye kazi za auditing kampuni yoyote

ila la msingi kuliko yote ni kwamba, watu wote wawe wanaingia kazini saa mbili na kutoka saa kumi na moja, atayeweza kwenda kokote nje ya muda huo, rukhsa kwani atakua ametimiza wajibu wake wa msingi then akajitafutie ziada!
 
Back
Top Bottom