Madaktari waonya kuhusu matumizi ya Vipipi Mahaba

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,206
4,699
Tahadhari hii imetolewa na Jumuiya ya Madaktari nchini kufuatia kuongezeka kwa matangazo yanayohamasisha matumizi yake.

Matumizi ya dawa mbalimbali zinazoongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa Wanawake imeelezwa yanahatarisha afya za wahusika

Baadhi ya dawa hizo hutumika kama pipi na mtumiaji huzimung'unya, zipo za kufukiza sehemu za siri na nyingi huwekwa sehemu za siri

Athari za matumizi ya dawa hizo ambazo hazijathibitishwa kitaalamu ni pamoja na kusababisha kansa ya kizazi

MCL

=====

Wakati matangazo ya vipipi vya kuongeza uwezo na hamu ya kushiriki tendo la ndoa yakizidi kushamiri mitandaoni, madaktari wameonya matumizi ya bidhaa hizo na nyingine zinazodaiwa kuwasaidia wanawake.

Madaktari waliohojiwa na Mwananchi walionya kutokana na pipi hizo kutojulikana kutengenezwa na kitu gani ndani yake, wameonya matumizi hayo kwa wanawake.

Pia madaktari hao wametahadharisha wanawake hao juu ya matumizi ya dawa na bidhaa nyingine ambazo huziweka ukeni, wakieleza kuwa ni chanzo cha magonjwa, yakiwamo fangasi na saratani.

Siku za karibuni kumekuwapo na matangazo yanayonadi pipi hizo maarufu kama ‘pipi mahaba’ ambazo pia zinauzwa kwenye maeneo yenye mikusanyiko ya wanawake, zikiwamo saluni.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili hivi karibuni umebaini kuwa wanawake wanazichangamkia pipi hizo zinazodaiwa kusaidia kuongeza uwezo, hamu ya kushiriki tendo la ndoa na kumfurahisha mwanaume.

Gazeti hili lilizitafuta mamlaka za Serikali, ikiwamo Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Baraza la Tiba Asili na Tiba mbadala na taasisi hizi zote zimeeleza kutozifahamu pipi hizo wala zinavyotengenezwa.

Pipi hizo zenye rangi nyeupe mithili ya maji zimekuwa habari ya mjini kwa sasa, kuanzia mitandaoni hadi katika maeneo yenye mikusanyiko ya wanawake.

Kulingana na wauzaji, pipi hizo ni suluhisho la matatizo ya kimwili yanayoweza kumletea vikwazo mwanamke katika ushiriki wake kwenye tendo la ndoa.

Pipi hizo ambazo huuzwa kati ya Sh5,000 hadi Sh10,000 zinatumiwa kwa kuchanganywa kwenye maji ya moto yenye tangawizi kwa pipi nne au tano, kisha mtumiaji anakoroga kabla ya kunywa na kusubiri zifanye kazi baada ya saa mbili.

Hawa Mbega, anayezunguka kuuza pipi hizo mitaa ya Kariakoo anazinadi akieleza kuwa licha ya kumuongezea mwanamke hamu ya tendo, huongeza joto na kubana sehemu za siri. “Shoga angu shoo ya vipipi sio ya kitoto, yaani kama ndio umeamua siku hiyo unachemsha chai ya tangawizi, ukiweka kwenye kikombe unaviweka vinayeyuka unakunywa.

“Baada ya saa mbili vinajibu, shemeji lazima akuulize, shoo yake sio ya mchezo, unakuwa na nguvu, huchoki na kama uke umelegea, utakaza utakuwa vizuri tu, havina madhara vimetengenezwa na miwa vinatoka nje ya nchi,” alisema na kuongeza: “Pia, nina mazagazaga kibao ambayo ukiyatumia nakuhakikishia mwanaume hakuachi, hela yake utaipata na kama ana uwezo atakufanyia kila unachotaka hata ukihitaji gari atakupa,” alijigamba Hawa ambaye pia ni kungwi.

Mwananchi ilishuhudia wanawake wakichangamkia vipipi hivyo vilivyokuwa vikiuzwa kama njugu, huku wakionyesha nia ya kwenda kujaribu kuvitumia.

Mmoja wa watu ambao wameshatumia vipipi hivyo aliyefahamika kwa jina la Suzi alithibitisha uwezo wake: “Mimi nimewahi kuvitumia, nakushauri kama kweli unahitaji kuweka mambo yako vizuri chukua hizo pipi, shoo yake si mchezo.”

Kauli hiyo ya Suzi iliwafanya wanawake watatu waliokuwa katika eneo hilo kununua pipi hizo kwa ajili ya kwenda kuzitumia ili kupata matokeo waliyoelezwa.

Mamlaka zinasemaje?

Mwananchi lilizungumza pia na Mkuu wa kitengo cha uhusiano wa TBS, Rhoida Andusamile aliyeeleza: “Kiukweli sizifahamu hizo pipi na kama unasema mtu akila zina matokeo hayo hizo sasa ni dawa, jaribu kucheki na watu wa TMDA na pia nitafuatilia”.

Akizungumzia suala hilo, Meneja na Uhusiano na Mawasiliano kwa umma wa TMDA, Gaudensia Simwanza alikiri kuna changamoto ya udhibiti wa uuzaji wa dawa katika mitandao ya kijamii. “Nashindwa kuzizungumzia dawa hizo kwa kuwa sina uhakika kama zipo kwenye kundi la dawa tunazosimamia sisi, maana inaweza kuwa ni dawa zinazoangukia kwenye tiba asili, ila wito wetu dawa hazitakiwi kuuzwa wala kutumiwa kiholela, wananchi wawe makini,” alisema Simwanza.

Kwa upande wake, Mfamasia katika Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Ndahani Msigwa alisema, “Hizo pipi hatuzifahamu na inawezekana kuna vitu vingi vinatumika, lakini kwa kuwa havijaja ofisini na kuvithibitisha basi mtu atakuwa anatumia kwa uamuzi wake na maisha yake.”

Kando na vipipi hivyo, kuna bidhaa kadhaa ambazo zinatumiwa na wanawake zikihusisha viungo vyao vya uzazi, jambo ambalo linaweza kuleta athari kiafya.

Kuna dawa inaitwa gusa unase ambayo ni majani yaliyoviringwa kwenye umbo la duara dogo ambayo huwekwa ukeni na kuachwa kwa muda, kisha hutolewa ikidaiwa kuongeza ladha ya tendo kwa mwanaume. Pia yapo mafuta yanaitwa misk ambayo nayo huwekwa ukeni kwa kazi hiyo hiyo ya kuongeza ladha na mvuto.

Zipo pia dawa za unga ambayo matumizi yake inaelekezwa kuwekwa kwenye maji ya moto yaliyochemka (steamer) kisha mwanamke kuchuchumalia maji hayo ili mvuke umuingie kwa dakika tano hadi 10. Imedaiwa kuwa dawa hiyo inasaidia kuondoa harufu ukeni, kupunguza ukubwa wa uke, kuondoa ukavu pamoja na kukaza misuli ya uke.

Wapo pia ambao hutumia udi kufukiza sehemu za siri ili ziwe na harufu nzuri.

Kauli ya madaktari

Baadhi ya madaktari waliozungumza na gazeti hili wameeleza kuwa, mwanamke anaweza kujiweka kwenye hatari kwa kutumia vitu visivyofaa kwenye viungo vyake vya uzazi na kujisababishia magonjwa, ikiwamo saratani.

Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, Ali Said alisema sehemu za siri za mwanamke zina bakteria walinzi hivyo, kutumia dawa na kemikali inaweza kuwaua bakteria hao na kuacha sehemu hizo zikiathiriwa kutokana na kukosa ulinzi wa kutosha.

“Uke ulivyoumbwa tayari una bakteria ambao kazi yao ni ulinzi, hivyo usafi wake unahitaji maji pekee, hakuna haja ya kuweka sabuni za kemikali, dawa wala mvuke wa maji ya moto ni hatari sana kiafya,” alisema.

Daktari huyo alieleza kuwa hakuna dawa ambayo imethibitishwa kuwa ina uwezo wa kumwongezea mwanamke hamu au nguvu ya kushiriki tendo la ndoa, kinachofanywa na wafanyabishara hao ni kutafuta pesa.

Chanzo: Mwananchi
 
Tahadhari hii imetolewa na Jumuiya ya Madaktari nchini

Matumizi ya Pipi zinazoongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa Wanawake imeelezwa yanahatarisha afya za wahusika

MCL
Dah kwwli izo pipi zinpigwe marufuku yaan demu mmoja nilimpapatua alikuwa amebwiaa ivyo vipipi yaan shuka ziili lowa majasho mdada hakuridhika ikabidi nilale kwake sikuniyo dah izo pipi kweli zipigwe marufuku
 
Tahadhari hii imetolewa na Jumuiya ya Madaktari nchini kufuatia kuongezeka kwa matangazo yanayohamasisha matumizi yake.

Matumizi ya dawa mbalimbali zinazoongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa Wanawake imeelezwa yanahatarisha afya za wahusika

Baadhi ya dawa hizo hutumika kama pipi na mtumiaji huzimung'unya, zipo za kufukiza sehemu za siri na nyingi huwekwa sehemu za siri

Athari za matumizi ya dawa hizo ambazo hazijathibitishwa kitaalamu ni pamoja na kusababisha kansa ya kizazi

MCL
Dah kwwli izo pipi zinpigwe marufuku yaan demu mmoja nilimpapatua alikuwa amebwiaa ivyo vipipi yaan shuka ziili lowa majasho mdada hakuridhika ikabidi nilale kwake sikuniyo dah izo pipi kweli zipigwe marufuku
Mkuu tupe uzoefu kidogo vp bi dada hakurizika una maanisha nini? au alikuwa hataki itoke uendelee kupiga zeze tu
 
mkuu tupe uzoefu kidogo vp bi dada hakurizika una maanisha nini? au alikuwa hataki itoke uendelee kupiga zeze tu
Alitaka nilale pale pale yaan akijisikia tu ana ji servia mwenyewe tena nakumbuka kauli yake moja aliniambia "ningekuwa na uwezo ninge ikata iyo zakaria ibaki na mm ww uende na li jeans lako " eh nikaona oh kheri sl nusu shari kuliko shari kamili
 
Back
Top Bottom