joshydama
JF-Expert Member
- May 10, 2016
- 4,623
- 5,036
Habari wana bodi,
Naomba kupata ufafanuzi kuhusu madaktari walio katika hospitali za watu binafsi kwa sababu wamekuwa ni kituko sana katika jamii linapokuja suala la kutoa huduma bora kwa wateja wao.
Hawa ndugu zetu wakati mwingine huwa wanafanya kazi kwa mazoea sana na si kwa uzoefu wala kwa utalaamu walio nao au huenda huwa wanakosa utalaamu katika kazi zao.
Siku moja nikiwa pale Sinza nilienda katika dispensary Fulani kwa nia ya kupata huduma ila cha kushangaza sikutamni tena nipate huduma katika ile dispensary kwa sabau ya uwezo mdogo wa kitabibu aliyouonesha yule jamaa. Hivyo basi bila kupepesa macho nikamuuliza kama yeye ni qualified Doctor au ni unqualified one. Sikujali kwamba angejisikia vibaya wala nini. Baada ya kumuuliza vile ilipelekea apaniki sana. Kutokana na kupaniki kwake nikagundua kuwa yule alikuwa siyo qualified Doctor bali ni unqualified.
Siyo Dispensary hiyo tu bali kuna dispensary nyingi sana hapa mjini Dar es salaam ambazo zimewaajiri watu ambao hawana sifa ya udaktari.
Kwanini mnanya hivyo nyie mnaowaajiri unqualified Doctors? kwa upande mwingine nyie ambao ni unqualified Doctor kwanini mnakubali kufanya kazi ambazo hamna sifa wala vigezo vya kufanya. hivyo? Hamuoni kwamba mnawadhalilisha wenye sifa zao?
Afya ni jambo la msingi sana. siyo la kulichukulia poa kabisa. Tumekuwa tukishuhudia mengi sana kuhusu nyie ambao mnafanya hizo kazi mfano unatakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa ila unafanyiwa upasuaji tumboni n.k
Kwani nyie madaktari wenye sifa mmeshindwa kudhibiti hawa vishoka waonasumbua huku mtaani? Hakika kuna umhimu wa kuanzisha mfumo wa kielektroniki wa kumtambua daktari mwenye sifa na ambao ni vishoka ili kulinda afya zetu.
Je nyie mdaktari huwa manasajiriwa ukishahitimu masomo yako au inakuwaje? mfano wahasibu lazima wawe wamesajiri katika bodi yao na kwa wanasheria iko hivyo hivyo.
Karibuni kwa michango ili tupambane na vishoka huku mtaani.
Naomba kupata ufafanuzi kuhusu madaktari walio katika hospitali za watu binafsi kwa sababu wamekuwa ni kituko sana katika jamii linapokuja suala la kutoa huduma bora kwa wateja wao.
Hawa ndugu zetu wakati mwingine huwa wanafanya kazi kwa mazoea sana na si kwa uzoefu wala kwa utalaamu walio nao au huenda huwa wanakosa utalaamu katika kazi zao.
Siku moja nikiwa pale Sinza nilienda katika dispensary Fulani kwa nia ya kupata huduma ila cha kushangaza sikutamni tena nipate huduma katika ile dispensary kwa sabau ya uwezo mdogo wa kitabibu aliyouonesha yule jamaa. Hivyo basi bila kupepesa macho nikamuuliza kama yeye ni qualified Doctor au ni unqualified one. Sikujali kwamba angejisikia vibaya wala nini. Baada ya kumuuliza vile ilipelekea apaniki sana. Kutokana na kupaniki kwake nikagundua kuwa yule alikuwa siyo qualified Doctor bali ni unqualified.
Siyo Dispensary hiyo tu bali kuna dispensary nyingi sana hapa mjini Dar es salaam ambazo zimewaajiri watu ambao hawana sifa ya udaktari.
Kwanini mnanya hivyo nyie mnaowaajiri unqualified Doctors? kwa upande mwingine nyie ambao ni unqualified Doctor kwanini mnakubali kufanya kazi ambazo hamna sifa wala vigezo vya kufanya. hivyo? Hamuoni kwamba mnawadhalilisha wenye sifa zao?
Afya ni jambo la msingi sana. siyo la kulichukulia poa kabisa. Tumekuwa tukishuhudia mengi sana kuhusu nyie ambao mnafanya hizo kazi mfano unatakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa ila unafanyiwa upasuaji tumboni n.k
Kwani nyie madaktari wenye sifa mmeshindwa kudhibiti hawa vishoka waonasumbua huku mtaani? Hakika kuna umhimu wa kuanzisha mfumo wa kielektroniki wa kumtambua daktari mwenye sifa na ambao ni vishoka ili kulinda afya zetu.
Je nyie mdaktari huwa manasajiriwa ukishahitimu masomo yako au inakuwaje? mfano wahasibu lazima wawe wamesajiri katika bodi yao na kwa wanasheria iko hivyo hivyo.
Karibuni kwa michango ili tupambane na vishoka huku mtaani.