madindigwa
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 2,453
- 2,849
Kwa kua wao mamechanjwa ndio wanataka kiwe kilio Cha wengi sio mbona hawasemi kupima ukimwi iwe lazima na majibu yatoke hadharaniMadaktari wameishauri Serikali chanjo ya Corona iwe lazima. Si jambo baya na wapo sahihi kwa kuwa wao ni wataalamu.
Serikali haipaswi kukataa ushauri wowote wa wataalamu kwa maana mambo yakienda ndivyo sivyo watakuwa hawana wa kumwajibisha. Hivyo ushauri uzingatiwe pia.
Na mimi binafsi Sina shaka na huu ushauri wa hawa madaktari nguli kabisa, Hoja kubwa ni wataalamu wa afya kufariki wakiwa wanaendelea kupambana na ugonjwa wa corona, ila kuna mambo lazima waweke bayana.
Nimejaribu kujiuliza hivyo pia si kwa ubaya, ila vyovyote vile bado Kuna nafasi ya kupambana na huu ugonjwa na kuutokomeza.
- wataalamu wa afya wanaendelea kufa, Ina maana hawa wataalamu wa afya walikuwa hawajapata chanjo? Ikiwa hawajapata, kwanini? Na wao ndio sisi tunategemea wawe mfano kwenye kutumia sayansi kukabili huu ugonjwa, hapa pana wasiwasi.
- Ikiwa walipata chanjo, maswali yatabaki kwanini wanakufa kwa Corona ikiwa tayari walipata chanjo. Ina maana tutarudi kuwaambia watu kuwa chanjo haizuii kufa kwa corona?