Madaktari wa Wanyama (TVA) walaani uteketezaji wa Vifaranga 50,000 wa Kuku

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,365
8,097
Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania (TVA) kimetoa taarifa ya kupinga na kuonesha kusikitishwa kwake juu ya kitendo cha Kampuni ya Uzalishaji Vifaranga wa Kuku ya Kibo Poultry kuteketeza Vifaranga 50,000 hadharani kwa madai ya kukosa soko.

TVA wamesema pamoja na kutambua matakwa ya Kanuni za vituo vya Utotoleshaji (GN 959 of 2019 Regulation 11: Restriction to Rearing of Chicks beyong 72 at Hatcheries) zinazoruhusu kuahribu vifaranga waliokaa zaidi ya saa 72 kwa njia zinazoruhusiwa na kuheshimu Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154, Chama kinalaani kitendo hicho na hakijaridhishwa na njia zilizotumika katika uteketezaji wa Wanyama hao kwa kuwa ni za mateso na hasa ikifahamika kwa kuku ni viumbe wenye hisia (Sentient Beings) na ni kinyume cha Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154: (Sheria namba 19 ya mwaka 2008 kifungu cha 4, 29 na 32 na kanuni zake.

Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania kinaziomba Mamlaka husika kuchukua hatua stahiki ili kudhibiti tabia za ukiukwaji wa Sheria ya Ustawi wa Wanyama na Kanuni zake unaoendelea kujitokeza mara kwa mara nchini.

Soma zaidi Uteketezaji huu wa vifaranga ni unyama uliopitiliza

Fj9CD0MWYAATtOQ
 
Hawa walikuwa wapi pia kulaani na kusikitika kipindi cha mwendazake vifaranga vya wafanyabiashara walioingiza kutokea Kenya na vikachomwa hadharani

Maana hatukuwasikia achilia mbali kuwaona wakituonyesha hivyo vifungu, waache double standard

Kipindi cha mwendazake kwenye ule uzi nilipinga na hata hawa kibo nao nawapinga kwa uamuzi wa kiuendawazimu, kama ni kukosa soko si wangeuza bei ya hasara au kuvigawa bure tu
 
Hawa walikuwa wapi pia kulaani na kusikitika kipindi cha mwendazake vifaranga vya wafanyabiashara walioingiza kutokea Kenya na vikachomwa hadharani

Maana hatukuwasikia achilia mbali kuwaona wakituonyesha hivyo vifungu, waache double standard

Kipindi cha mwendazake kwenye ule uzi nilipinga na hata hawa kibo nao nawapinga kwa uamuzi wa kiuendawazimu, kama ni kukosa soko si wangeuza bei ya hasara au kuvigawa bure tu
Mwache apumzike baba wa watu.(wanavyosema wenyewe)
 
Hawa walikuwa wapi pia kulaani na kusikitika kipindi cha mwendazake vifaranga vya wafanyabiashara walioingiza kutokea Kenya na vikachomwa hadharani

Maana hatukuwasikia achilia mbali kuwaona wakituonyesha hivyo vifungu, waache double standard

Kipindi cha mwendazake kwenye ule uzi nilipinga na hata hawa kibo nao nawapinga kwa uamuzi wa kiuendawazimu, kama ni kukosa soko si wangeuza bei ya hasara au kuvigawa bure tu
Vifaranga vya wakenya vya nini? Sasa hivi vimechomw vya viwanda vya Tanzania na watu wamekosa ajira
 
Hawa walikuwa wapi pia kulaani na kusikitika kipindi cha mwendazake vifaranga vya wafanyabiashara walioingiza kutokea Kenya na vikachomwa hadharani

Maana hatukuwasikia achilia mbali kuwaona wakituonyesha hivyo vifungu, waache double standard

Kipindi cha mwendazake kwenye ule uzi nilipinga na hata hawa kibo nao nawapinga kwa uamuzi wa kiuendawazimu, kama ni kukosa soko si wangeuza bei ya hasara au kuvigawa bure tu
Kilichofanyika hapo ni kutengeneza tension kwa serikali ipige marufuku uagizwaji wa vifaranga kutoka nje ya nchi. Japo hawajafanya kwa njia sahihi.

Sheria inaruhusu kuteketeza vifaranga walio kosa wananuzi baada ya masaa 72 ya kuanguliwa.

Hata hivyo siyo kwa njia ya moto na sio hadharani kama Kibo walivyo fanya. Vifaranga wanaweza teketezwa smoothly kwa kutumia Carbondioxide gas.

Naungana na (Tanzania Veterinary Association)TVA kulaani kitendo hicho, aidha mamlaka nyingine kama Veterinary Council of Tanzania(VCT) wanatakiwa nao watoe adhabu/Onyo kwa taasisi hii Ili kukomesha hizi tabia.

Tuzilinde na kuziheshimu haki za wanyama.
 
Vifaranga vya wakenya vya nini? Sasa hivi vimechomw vya viwanda vya Tanzania na watu wamekosa ajira
Nachojiuliza kwann watu waagize vifaranga Kenya wakati Tanzania kuna vifaranga.

Shida ni nini ni bei? Ubora au Uchawi tu
 
kama idara zinashindwa kuelewana hapa tz. ni sawa na ccm kuanzia sehemu zote
 
Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania (TVA) kimetoa taarifa ya kupinga na kuonesha kusikitishwa kwake juu ya kitendo cha Kampuni ya Uzalishaji Vifaranga wa Kuku ya Kibo Poultry kuteketeza Vifaranga 50,000 hadharani kwa madai ya kukosa soko

TVA wamesema pamoja na kutambua matakwa ya Kanuni za vituo vya Utotoleshaji (GN 959 of 2019 Regulation 11: Restriction to Rearing of Chicks beyong 72 at Hatcheries) zinazoruhusu kuahribu vifaranga waliokaa zaidi ya saa 72 kwa njia zinazoruhusiwa na kuheshimu Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154: Chama kinalaani kitendo hicho na hakijaridhishwa na njia zilizotumika katika uteketezaji wa Wanyama hao kwa kuwa ni za mateso na hasa ikifahamika kwa Kuku ni viumbe wenye hisia (Sentient Beings) na ni kinyume cha Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154: (Sheria namba 19 ya mwaka 2008 kifungu cha 4, 29 na 32 na kanuni zake.

Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania kinaziomba Mamlaka husika kuchukua hatua stahiki ili kudhibiti tabia za ukiukwaji wa Sheria ya Ustawi wa Wanyama na Kanuni zake unaoendelea kujitokeza mara kwa mara nchini.

Soma zaidi Uteketezaji huu wa vifaranga ni unyama uliopitiliza

Fj9CD0MWYAATtOQ
Hivi kwanini hawakugawa bure kwa wananchi wakajaribu? Kuna sababu yoyote ya kitaalam ya kuwaangamiza?
 
Sio unafki.

Kipindi cha jiwe hata wewe ungekua mwenyekiti wa TVA usingefanya lolote kwa sababu ya mambo yalivo kua.

Hii inaleta picha kuna haja ya kuzipa kinga taasis zetu ili wataalamu wetu wafanye kazi kwa uhuru na kujiamini.


Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
Ni unafiki mkuu wala usiwatetee

Kama upo kwa ajili ya kutetea maslahi ya utaalamu wako simamia ukweli no matter what wapo waliosimamia ukweli kipindi cha mwendazake kama marehemu Mwele japo ilimgharimu lkn alisimamia alichokiamini

Sasa hawa waliufyata leo ndiyo wananyanyua vichwa na vifungu
 
'Inchi imefongolewa' tunaomba tuletewe mkaa kutoka misitu ya Amazon, maana hii ya wazawa ni mepesi sana.
 
Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania (TVA) kimetoa taarifa ya kupinga na kuonesha kusikitishwa kwake juu ya kitendo cha Kampuni ya Uzalishaji Vifaranga wa Kuku ya Kibo Poultry kuteketeza Vifaranga 50,000 hadharani kwa madai ya kukosa soko

TVA wamesema pamoja na kutambua matakwa ya Kanuni za vituo vya Utotoleshaji (GN 959 of 2019 Regulation 11: Restriction to Rearing of Chicks beyong 72 at Hatcheries) zinazoruhusu kuahribu vifaranga waliokaa zaidi ya saa 72 kwa njia zinazoruhusiwa na kuheshimu Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154: Chama kinalaani kitendo hicho na hakijaridhishwa na njia zilizotumika katika uteketezaji wa Wanyama hao kwa kuwa ni za mateso na hasa ikifahamika kwa Kuku ni viumbe wenye hisia (Sentient Beings) na ni kinyume cha Sheria ya Ustawi wa Wanyama Sura 154: (Sheria namba 19 ya mwaka 2008 kifungu cha 4, 29 na 32 na kanuni zake.

Chama cha Madaktari wa Wanyama Tanzania kinaziomba Mamlaka husika kuchukua hatua stahiki ili kudhibiti tabia za ukiukwaji wa Sheria ya Ustawi wa Wanyama na Kanuni zake unaoendelea kujitokeza mara kwa mara nchini.

Soma zaidi Uteketezaji huu wa vifaranga ni unyama uliopitiliza

Fj9CD0MWYAATtOQ
Je, hicho kiwanda hakina malengo ya uzalishaji? Yan Kinafyatua tu mavifaranga hovyo? Shame on you Kibo Hatchery. Tuanzie na kuulaani Uongozi wa kiwanda kwa kushindwa kuwa na mipango endelevu. Yaani unazalishaje bila kujua soko la uhakika lipo na uhitaji wake ni kiasi gani? Hakuna Mchumi au Mtaalam anayesimamia Uzalishaji hapo kituoni?? au hapo kituoni wanazalisha kwa mtindo wa Business as usual? Hawajali "Demand" ikoje; wao ni kutotolesha vifaranga tuuu bila kujua mnunuzi - Mteja/Mlaji ni nani. Kwa kweli jamaa hapo wamechemka mno. Kama yupo mtaalam wa mifugo hapo kituoni (animal Sc. au Veterinary) napendekeza tena strongly aachishwe /afukuzwe kazi chap. Hajaitendea haki Taaluma yake. Lakini kama ni hawa vijanadot.com sishangai sana kwani walisahau ku-Google "The effects of Over production" na What is Dumping .....na teacher kawapotezea kimtindo kawapa vyeti. Halafu wanakuja kulialia hapa eti Hakuna ajira. :oops:
 
Wanashobo tu. Au uo umoja umeanzishwa mwaka huu.
Wamejisahau au ni Uzembe kwani mojawapo ya Majukumu yao Kitaalam ni pamoja na kukagua maeneo ya Uzalishaji na Kutoa Ushauri - tena bure.
Lakini Kama mwenye Kituo alipata ushauri kuhusu umuhimu wa kuzingatia Kanuni za Uzalishaji kibiashara halafu akapuuzia, basi huyo jamaa ni BOYA kabisa.
 
Hivi kwanini hawakugawa bure kwa wananchi wakajaribu? Kuna sababu yoyote ya kitaalam ya kuwaangamiza?
Hakuna.
# Isipokuwa pale kunapokuwa na Tishio la uwepo wa Ugonjwa hatari wa kuambukiza/mlipuko
au inapokuwa ugonjwa umethibitishwa. Tofauti na hapo ni mambo ya Sheria e.g. Ukiukwaji wa Taratibu za kuingiza nchini, Kusafirisha bila kibali au Kuwatenda kikatili e.g. kuwanyima maji, chakula au hewa ya kutosha kwa kuwasonganisha mno kwa muda mrefu n.k.
# Ikumbukwe pia kwamba matumizi ya Sheria huendana na kutumia Hekima na Busara wakati wa kufanya maamuzi.
 
Back
Top Bottom