Madaktari wa Meno Amana tofautisheni kati ya Kung'oa misumari mabatini na meno midomoni mwetu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Mmesemwa sana ila hamsikii na leo ‘ nawachana ‘ live / mubashara humu JF kuwa tafadhalini hebu tofautisheni basi kati ya Kung’oa misumari katika Mabati na Kung’oa Meno yetu haya yaliyo katika midomo yetu.

Nyie ndiyo Madaktari pekee wa meno hapa nchini ambao mnamfanya Mgonjwa wa meno kabla ya kuja Kwenu kwanza huko huko alipo aanze Kusali sana kwa Mwenyezi Mungu ili ampe nafuu ya maumivu au inambidi huyo Mgonjwa kabla ya kuja Kwenu ahakikishe amenunua dawa zote za kutuliza maumivu kwani akija tu Kwenu hawezi kutoka salama.

Ili muone mlivyo na matatizo kwanza mnavyompokea tu Mgonjwa anayetaka Kung’oa meno kwenu tayari ni ‘ adhabu ‘ tosha kwani kuwa mnakuwa na ‘ jazba ‘ sana na sasa ‘ shughuli ‘ nzima Mgonjwa atakutana nayo huko ndani akiwa anang’oa jino lake.

Wengi wenu mkiwa mnatung’oa meno yetu huwa mnakuwa mmenuna ( Sura Limao ) halafu hata hivyo Vifaa vyenu huwa mnaviingiza katika midomo yetu kwa nguvu kubwa utadhani ‘ Dereva ‘ wa Lori anaweka gia ili apandishe vizuri Mlima Kitonga.

Na ndiyo maana siku hizi mnakimbiwa mno na Wagonjwa wa Meno na mnawapata tu hao Mangumbaru / Washamba ambao hawawajui ila hata wao wakishapata ‘ maumivu ‘ yenu nao ‘ hujanjaruka ‘ na kusepa Hospitali zingine.

Nimewaheshimu sana na sitaki niwaharibieni Kazi ila najua kwa uzi huu ‘ Madaktari ‘ husika mtakuwa mmejijua japo hata kwa majina yenu nawafahamu ila leo nawaweka ‘ Viporo ‘ nikiwa na matumaini makubwa kuwa baada ya GENTAMYCINE leo ‘ kuwashtueni ‘ basi mtabadilika upesi na kuanza Kutung’oa meno Kiutaratibu, Kiumakini na Kiurafiki kabisa.

Hospitali ya Amana ni nzuri sana na inafanya vyema ila tatizo kubwa lipo tu kwa hao wang’oa misumari / wang’oa meno wenu ambao kiukweli wanatuachia ‘ Maumivu ‘ na ‘ Majeraha ‘ makubwa mno sisi Wagonjwa wa Kutukuka wa Meno.

Shikamooni Madaktari wote wa Meno wa Hospitali ya Amana!

Nawasilisha.
 
Mmesemwa sana ila hamsikii na leo ‘ nawachana ‘ live / mubashara humu JF kuwa tafadhalini hebu tofautisheni basi kati ya Kung’oa misumari katika Mabati na Kung’oa Meno yetu haya yaliyo katika midomo yetu.

Nyie ndiyo Madaktari pekee wa meno hapa nchini ambao mnamfanya Mgonjwa wa meno kabla ya kuja Kwenu kwanza huko huko alipo aanze Kusali sana kwa Mwenyezi Mungu ili ampe nafuu ya maumivu au inambidi huyo Mgonjwa kabla ya kuja Kwenu ahakikishe amenunua dawa zote za kutuliza maumivu kwani akija tu Kwenu hawezi kutoka salama.

Ili muone mlivyo na matatizo kwanza mnavyompokea tu Mgonjwa anayetaka Kung’oa meno kwenu tayari ni ‘ adhabu ‘ tosha kwani kuwa mnakuwa na ‘ jazba ‘ sana na sasa ‘ shughuli ‘ nzima Mgonjwa atakutana nayo huko ndani akiwa anang’oa jino lake.

Wengi wenu mkiwa mnatung’oa meno yetu huwa mnakuwa mmenuna ( Sura Limao ) halafu hata hivyo Vifaa vyenu huwa mnaviingiza katika midomo yetu kwa nguvu kubwa utadhani ‘ Dereva ‘ wa Lori anaweka gia ili apandishe vizuri Mlima Kitonga.

Na ndiyo maana siku hizi mnakimbiwa mno na Wagonjwa wa Meno na mnawapata tu hao Mangumbaru / Washamba ambao hawawajui ila hata wao wakishapata ‘ maumivu ‘ yenu nao ‘ hujanjaruka ‘ na kusepa Hospitali zingine.

Nimewaheshimu sana na sitaki niwaharibieni Kazi ila najua kwa uzi huu ‘ Madaktari ‘ husika mtakuwa mmejijua japo hata kwa majina yenu nawafahamu ila leo nawaweka ‘ Viporo ‘ nikiwa na matumaini makubwa kuwa baada ya GENTAMYCINE leo ‘ kuwashtueni ‘ basi mtabadilika upesi na kuanza Kutung’oa meno Kiutaratibu, Kiumakini na Kiurafiki kabisa.

Hospitali ya Amana ni nzuri sana na inafanya vyema ila tatizo kubwa lipo tu kwa hao wang’oa misumari / wang’oa meno wenu ambao kiukweli wanatuachia ‘ Maumivu ‘ na ‘ Majeraha ‘ makubwa mno sisi Wagonjwa wa Kutukuka wa Meno.

Shikamooni Madaktari wote wa Meno wa Hospitali ya Amana!

Nawasilisha.
Duh!
 
Alafu haya yote yanajili kipindi hiki Rais anaposema hataki watu walipwe posho wafanye kazi tu.
 
Huna uwezo wa kuwaharibia kazi madaktari. Unataka wakung'oe jino huku wanakuchekea ili iweje? Hukawi kudai wamekuambukiza TB kwa vile waliacha mdomo wazi wakati wanakuhudumia



Kwa maneno hayo ujumbe umefika na kama ni dozi umewapa[/QUO
 
Hakuna hospitali yeyote ya serikali utakayong'olewa jino bila kutoka machozi. Usipolia machoni basi utalia moyoni.

Shida iliyopo ni vitendea kazi. Ganzi ya kuchomwa mtu mmoja mnachomwa 4...lazima ushikwe wazimu. Ukiumwa jino likawa beyond repair, chukua elfu 10 yako, funga safari hadi Ubungo. Nenda Kibangu Mission Hospital ukang'olewe jino. Hutajua kuwa tayari limeshatolewa maana hutasikia kitu.

Kung'oa jino kwa bajeti ya serikali hakujawahi kumuacha mtu salama
 
Hakuna hospitali yeyote ya serikali utakayong'olewa jino bila kutoka machozi. Usipolia machoni basi utalia moyoni.

Shida iliyopo ni vitendea kazi. Ganzi ya kuchomwa mtu mmoja mnachomwa 4...lazima ushikwe wazimu. Ukiumwa jino likawa beyond repair, chukua elfu 10 yako, funga safari hadi Ubungo. Nenda Kibangu Mission Hospital ukang'olewe jino. Hutajua kuwa tayari limeshatolewa maana hutasikia kitu.

Kung'oa jino kwa bajeti ya serikali hakujawahi kumuacha mtu salama
Acha urongo
 
Hospitali nzuri ya serikali kwa huduma ya kung'oa meno ni Mnazi Mmoja. Pale kuna madaktari wenye uwezo wa hali ya juu sana kuhusu magonjwa ya meno na kinywa.
 
Mkuu gharama za kufanya rootcanal zipoje?? na hospital gani nzuri kwa hii tiba??
Root canal huanzia elfu 70-90 kwa hospitali za serikali. Kwa Private inaanzia 100,000-200,000/= kulingana na jino.
Sasa kuhusu hospitali ipi inafanya vizuri siwezi kulisemea.
Ila Daktari wa meno anayeweza kuifanya tiba hiyo ni kuanzia mwenye Degree moja (DDS) na kuendelea juu masters (Mdent).
Sasa nenda kwenye hospitali ambayo utampata daktari mwenye qualifications hizo.
 
Back
Top Bottom