TENGEFU
Senior Member
- Jan 25, 2017
- 138
- 206
Hii imetokea baada ya kijana aitwaye Kennedy Mathias Shirima kugongwa akiwa akiendesha pikipiki na Mwanajeshi ambaye ni daktari akiwa amelewa chakari majira ya saa 5 asubuhi. Mwanajeshi huyu ni kutoka kambi ya jeshi Tanganyika Parkers Arusha. Ajali hii ilitokea tarehe 08/01/2020
Mwanajeshi huyu alikuwa amelewa chakari majira ya saa 5 asubuhi alipohama upande wake na kwenda kumgonga Kennedy akiwa upande wa pili wa barabara eneo la Kilimani karibu na kilipo kituo maarufu cha kona ya Kiseriani.
Kennedy aliumia kichwani licha ya kwamba alikuwa amevaa kofia ngumu na alipelekwa hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mt. Meru. Madaktari walisema akafanyiwe kipimo cha CT scan na kwa sababu hakipatikani katika hospital ya Mt. Meru. Ndugu na majirani walimpeleka hospital ya NSK na kufanyiwa kipimo hicho na ripoti pamoja na picha zikaletwa hospitali ya MT. Meru alipokuwa amelazwa chumba cha majeruhi na hapa ndipo mchezo wa kummaliza ukaanza. Dakatari wa jeshi aliyemgonga kwa kushirikiana na madaktari wa MT. Meru wakahakikisha kipimo hakisomwi wala kufanyiwa matibabu stahiki ili Kennedy apoteze Maisha na hivyo kupoteza Ushahidi wa kesi inayomkabili Daktari mwanajeshi. Taarifa za ajali hii ya kizembe lipo kituo kikuu cha polisi Arusha.
Madaktari walikataa kusoma kipimo kwa sababu za kitoto ambazo ni (i) hawawezi kusoma ripoti ya CT scan bila kuwa na picha na CD, (ii)wametoka kufanya upasuaji wamechoka, (iii) wanasikia njaa wanaenda kula. Mimi nilikwenda personally kumuuliza nurse na aliniambia madaktari wamemaliza operesheni ya mwisho sasa hivi wanasikia njaa na wamechoka hawawezi kusoma kipimo labda kesho yake. Wakati huo hali ya mgonjwa ilikuwa siyo nzuri kwani alikuwa analalamika maumivu makali ya kichwa na hakuwa anaweza kuongea vizuri.
Siku ya tatu ndipo Madaktari walikuja kusoma kipimo na kusema picha imepigwa upande mmoja na inabidi ikapigwe na ya upande wa pili ndipo waweze kusoma. Hawakuonyesha udharura wowote wala kujali chochote kuhusu hali ya Kennedy.
Siku ya jumanne tarehe 14/01/2020 Kennedy akiwa katika hali mbaya akapewa discharge kurudi nyumbani. Lengo lilikuwa akafie nyumbani. Hali yake ilizidi kuwa mbaya na tarehe 15/01/2020 ndugu zake tulimchukua na kumpeleka katika hospital nyingine na madaktari walimpokea kama mgonjwa wa emergency na walivipokea na kuvisoma vipimo vilevile vya CT scan na kusema anatakiwa afanyiwe upasuaji wa haraka within 12hours la sivyo tutampoteza. Vipimo hivi hivi madaktari wa Mt. Meru walikataa kuvisoma kwa sababu ambazo ni very unprofessional.
Ilionekana kuna damu inavuja taratibu kichwani na ingeachwa basi alikuwa siku si nyingi apoteze Maisha. Tunaomba Mungu operesheni hii ifanyike kwa mafanikio.
Madaktari wa Mt. meru walijua kila kitu kuhusu hali ya Kennedy lakini kwa sababu mhusika wa ajali ni Daktari mwenzao tena Mwanajeshi basi wakaamua kula njama ili atoweke kumnusuru mwenzao.
Naiomba serikali iwachukulie hatua Madaktari hawa ambao wamekula njama chafu ambazo ni kinyume na kiapo chao cha udaktari.
Ninataka niamini kuna watu wengi wamepoteza Maisha si kwa sababu Mungu alipenda ila kwa sababu ya Madaktari wachache wala rushwa na wasio na chembe ya utu. Hata kama serikali na hususani wizara ya afya itashindwa kuwashughulikia nina imani Mungu hatawaacha salama labda watubu warudishe fahamu za utu na waache kutanguliza mbele maslahi yao
Mwanajeshi huyu alikuwa amelewa chakari majira ya saa 5 asubuhi alipohama upande wake na kwenda kumgonga Kennedy akiwa upande wa pili wa barabara eneo la Kilimani karibu na kilipo kituo maarufu cha kona ya Kiseriani.
Kennedy aliumia kichwani licha ya kwamba alikuwa amevaa kofia ngumu na alipelekwa hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mt. Meru. Madaktari walisema akafanyiwe kipimo cha CT scan na kwa sababu hakipatikani katika hospital ya Mt. Meru. Ndugu na majirani walimpeleka hospital ya NSK na kufanyiwa kipimo hicho na ripoti pamoja na picha zikaletwa hospitali ya MT. Meru alipokuwa amelazwa chumba cha majeruhi na hapa ndipo mchezo wa kummaliza ukaanza. Dakatari wa jeshi aliyemgonga kwa kushirikiana na madaktari wa MT. Meru wakahakikisha kipimo hakisomwi wala kufanyiwa matibabu stahiki ili Kennedy apoteze Maisha na hivyo kupoteza Ushahidi wa kesi inayomkabili Daktari mwanajeshi. Taarifa za ajali hii ya kizembe lipo kituo kikuu cha polisi Arusha.
Madaktari walikataa kusoma kipimo kwa sababu za kitoto ambazo ni (i) hawawezi kusoma ripoti ya CT scan bila kuwa na picha na CD, (ii)wametoka kufanya upasuaji wamechoka, (iii) wanasikia njaa wanaenda kula. Mimi nilikwenda personally kumuuliza nurse na aliniambia madaktari wamemaliza operesheni ya mwisho sasa hivi wanasikia njaa na wamechoka hawawezi kusoma kipimo labda kesho yake. Wakati huo hali ya mgonjwa ilikuwa siyo nzuri kwani alikuwa analalamika maumivu makali ya kichwa na hakuwa anaweza kuongea vizuri.
Siku ya tatu ndipo Madaktari walikuja kusoma kipimo na kusema picha imepigwa upande mmoja na inabidi ikapigwe na ya upande wa pili ndipo waweze kusoma. Hawakuonyesha udharura wowote wala kujali chochote kuhusu hali ya Kennedy.
Siku ya jumanne tarehe 14/01/2020 Kennedy akiwa katika hali mbaya akapewa discharge kurudi nyumbani. Lengo lilikuwa akafie nyumbani. Hali yake ilizidi kuwa mbaya na tarehe 15/01/2020 ndugu zake tulimchukua na kumpeleka katika hospital nyingine na madaktari walimpokea kama mgonjwa wa emergency na walivipokea na kuvisoma vipimo vilevile vya CT scan na kusema anatakiwa afanyiwe upasuaji wa haraka within 12hours la sivyo tutampoteza. Vipimo hivi hivi madaktari wa Mt. Meru walikataa kuvisoma kwa sababu ambazo ni very unprofessional.
Ilionekana kuna damu inavuja taratibu kichwani na ingeachwa basi alikuwa siku si nyingi apoteze Maisha. Tunaomba Mungu operesheni hii ifanyike kwa mafanikio.
Madaktari wa Mt. meru walijua kila kitu kuhusu hali ya Kennedy lakini kwa sababu mhusika wa ajali ni Daktari mwenzao tena Mwanajeshi basi wakaamua kula njama ili atoweke kumnusuru mwenzao.
Naiomba serikali iwachukulie hatua Madaktari hawa ambao wamekula njama chafu ambazo ni kinyume na kiapo chao cha udaktari.
Ninataka niamini kuna watu wengi wamepoteza Maisha si kwa sababu Mungu alipenda ila kwa sababu ya Madaktari wachache wala rushwa na wasio na chembe ya utu. Hata kama serikali na hususani wizara ya afya itashindwa kuwashughulikia nina imani Mungu hatawaacha salama labda watubu warudishe fahamu za utu na waache kutanguliza mbele maslahi yao