Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Kuna mambo kadhaa ambayo ningependa kuyatolea maoni kwa namna tofauti kwani tangu siku ile ya Jumatano usiku sijapata muda wa kutulia kuweza kuweka mawazo yangu juu ya yanayotokea. Baada ya kusoma (na kusikiliza kidogo hotuba ya Rais) nimejikuta sina mengi ya kusema ila kwamba madaktari wakikubali tu kurudi kazini wakati 'status quo' bado ipo basi wao wamejimaliza na kwa hakika watakuwa wameshindwa kutengeneza mazingira bora kwa madaktari wetu wanaokuja.
Kikwete kafanya hili ni la "madaktari hawa"
Mojawapo ya vitu ambavyo naamini vinaweza kuangaliwa kwa makosa ni kujifikiria madaktari hawa; kwamba madai yao ni madai ya wao peke yao; kwamba madai ya madaktari ni ya watu wa wakati huu au kizazi hiki tu. Kama - labda nitumie herufi kubwa hapa - KAMA madaktari wanaamini wanadai vitu ambavyo ni kwa ajili yao wao wenyewe tu na kwamba wanataka kujifurahisha au kufurahishwa wao tu kama madaktari wa sasa ili nao waonekane wanakula ile keki ya taifa basi NI LAZIMA warudi kazini bila masharti.
LAKINI - kama kinachowaongoza ni kufikiria mazingira ya sekta ya afya na maslahi ya wahudumu wake wa sasa na wa kizazi kijacho basi kurudi mara moja kazini (kumaliza mgomo) kutakuwa ni kosa kubwa ambalo japo litawahakikishia wao chakula na malazi na kutuliza munkari wa wanasiasa kwa hakika litakuwa ni jambo la kuja tena kushughulikia na vizazi vijavyo vya madaktari.
Binafsi ninaamini hili siyo suala la madai ya "madaktari hawa" tu bali ni suala la sekta nzima na madaktari wanaokuja nyuma yao. Kwa mbali hili linaonekana kwenye madai ya madaktari "wanafunzi" ambao leo hii tunaweza kuona kutoka mbali kuwa watakuja kuongoza mgomo mwingine. Hivi Ulimboka na wenzake kwani wameanza juzi? Si walianza tangu wakiwa wanafunzi wa udaktari? Wakati kina Ulimboka wakiwa shule na walipokwarizana na watawala wakaahirisha lakini likaja kutokea tena mapema mwaka huu na sasa na kwa hakika bila kulimaliza inavyopaswa hili litatokea tena.
Uhalali wa mgomo wa madaktari hautokani na sheria
Mojawapo ya mambo ambayo yanahitaji kufikiria ni kuwa je sheria yaweza kutumika kuwakandamiza watu? Je mara zote sheria inapaswa kutiiwa hata kama inakandamiza jamii au kundi la watu? Wana filosofia na wanaharakati duniani wanatambua kuwa sheria ikiandikwa ili kukandamiza watu basi watu wana haki (inayotokana na ukuu wa dhamira zao) kutoitii sheria hiyo. Madaktari inawezekana kabisa wanagoma bila kufuata sheria lakini itakuwaje kama wamegundfua kwamba sheria iliyopo inawakandamiza? Je waitii tu? Sheria kandamizi na dhalimu haipaswi kutiiwa. Hili ni somo toka Afrika ya Kusini, India, Marekani na nchi nyingine ambapo watu wametambua kuwa watawala hutumia "sheria" kukandamiza watu.
Serikali ilipitisha sheria ambazo zimekuwa ni kandamizi kwa haki za wafanyakazi. Sheria zimejengwa ili kuwalinda watawala wasisumbuliwe na watawaliwa. NI sawasawa na kundi la ng'ombe kutengeneza sheria za kudhibiti nyangenyange wasitue migongoni mwao. Tumeliona hili hata kwenye suala la maandamano ya kisiasa ambapo sheria zimeundwa ili kuzuia maandamano ya kisiasa (japo wenyewe wanasema kwa ajili ya kulinda amani na utulivu!).
Wameshavunja sheria kwa kusimamia maslahi yao; hawawezi kuvunja zaidi!
Kama maneno ya RAis Kikwete ni ya kweli (nami naamini ni ya kweli) kwamba mgomo huu hauna uhalali kwa mtazamo wa sheria iliyopo basi madaktari tayari wameshavunja sheria. Na kuwa tayari hatua zimeshaanza kuchukuliwa dhidi yao ni uthibitisho kuwa serikali inaamini mgomo huu ni haramu. Sasa kama hili ni kweli hivyo madaktari wakiendelea kugoma wanajidhuru nini zaidi ya vile ambavyo wameshajidhuru? Tayari wako kwenye mgomo "haramu" sasa kuendelea kugoma hakuufani mgomo huo kuwa "haramu zaidi"! Kwa msingi huo kusitisha mgomo na kurudi kazini bila suluhisho la mezani kunasaliti msimamo wao wote.
Madaktari wasijifikirie wao wenyewe kwani wataogopa
Madaktari wakiamua kujifikiria wao wenyewe wataogopa; wataogopa kwa sababu kama yameweza kumtokea Ulimboka yanaweza kumtokea mtu mwingine yeyote kati yao. Je itakuwaje kama watapoteza ajira zao (na hili JK kaliashiria)? watoto wao watakula wapi? Je zile nyumba wanazoishi itakuwaje? Sasa hapa ndio kuna tofauti ya wale wenye kuamini wanachosimamia na wale wanaofuata mkumbo. Kama wanaamini wako sahihi kudai maslahi ambayo siyo tu yatanufaisha wao bali pia madaktari na wafanyakazi wengine wa sekta hiyo huko mbeleni basi msimamo kwao ni: Kuendelea na mgomo.
Serikali inaweza kumaliza mgomo ndani ya masaa 24 bila kumfukuza daktari hata mmoja
Kama nilivyosema wakati ule (Machi) nguvu ya kumaliza mgomo huu iko ndani ya serikali siyo madaktari. Serikali ndiyo inatunga sera, sheria na kupanga bajeti ya sekta hiyo. TAyari tunajua sera yao ya afya ni mbovu imaeshindwa na sheria zake zinaonekana zina matatizo na kama ni bajeti ni hafifu mno na tegemezi. Kama haya yote ni kweli basi changamoto iko kwa serikali kukaa chini na kufikiria wafanye nini kukidhi madai ya madaktari? Binafsi nina pendekezo langu lakini nitaangalia suala hili linaenda vipi.
Madaktari walisharudishwa kazini mara moja baada ya kikombe cha chai Ikulu. Safari hii hakuna cha chai wala juisi ya machungwa; Je watarudi? Baada ya tukio la Ulimboka...?
Madaktari waongozwe na kumjali mgonjwa
Jambo hili llina mitazamo tofauti; je madaktari kurudi kwenye mazingira yale yale mabovu, bajeti finyu na mfumo mbaya wa utendaji kazi ambapo wamejikuta wakishindwa kutoa huduma inayostahili kwa wagonjwa kutafanya hali hiyo ibadilike kwa vile "madaktari wamerudi kazini"? Je kurudi katika mazingira yale yale (CT Scans hakuna, vipimo hadi hospitali binafsi, vitendea kazi hakuna au duni) kutaokoa maisha ya wananchi wetu? Je, hata wakati hakuna mgomo wananchi walikuwa salama mikononi mwa madaktari ambao wamechoka, hawana vitendea kazi na ambao wako kwenye mazingira magumu?
Wengine watasema "warudi tu"; sawa lakiniw arudi wakiwa wamebadilisha nini? Hivyo, mgomo huu kufanikiwa kwake ni lazima kuwe ni kubadilika kwa namna wanavyofanya kazi. Kwa mfano, waseme kuwa wanahitaji kuwe na "minimum standard" ya utendaji kazi wa hospiali. Kwamba, hospitali ya serikali ili ifanye kazi ni lazima iwe na vitu hivi na vikiwa vinafanya kazi:
X-Rays
Single Use Gloves
CT Scan/MRI within 100 miles na kwa hospitali za rufaa ni lazima ziwe na CT Scan inayofanya kazi;
Idadi ya wauguzi na waganga wasaidizi
n.k
Serikali ikikubali kama mambo haya basi madaktari wataweza kurudi kazini hata kama maslahi yao binafsi yanaweza yasiboreshwe kwa wakati huu; lakini kutaka tu warudi ilimradi warudi ni kuhukumu wagonjwa kwenye mikono isiyoweza kuokoa maisha yao hata kama akili na nia ipo.
HIvyo basi... wanavyofikiria kuamua kurudi au kuendelea na mgomo ni muhimu waangalie picha nzima ambayo ni zaidi ya wao!
Kikwete kafanya hili ni la "madaktari hawa"
Mojawapo ya vitu ambavyo naamini vinaweza kuangaliwa kwa makosa ni kujifikiria madaktari hawa; kwamba madai yao ni madai ya wao peke yao; kwamba madai ya madaktari ni ya watu wa wakati huu au kizazi hiki tu. Kama - labda nitumie herufi kubwa hapa - KAMA madaktari wanaamini wanadai vitu ambavyo ni kwa ajili yao wao wenyewe tu na kwamba wanataka kujifurahisha au kufurahishwa wao tu kama madaktari wa sasa ili nao waonekane wanakula ile keki ya taifa basi NI LAZIMA warudi kazini bila masharti.
LAKINI - kama kinachowaongoza ni kufikiria mazingira ya sekta ya afya na maslahi ya wahudumu wake wa sasa na wa kizazi kijacho basi kurudi mara moja kazini (kumaliza mgomo) kutakuwa ni kosa kubwa ambalo japo litawahakikishia wao chakula na malazi na kutuliza munkari wa wanasiasa kwa hakika litakuwa ni jambo la kuja tena kushughulikia na vizazi vijavyo vya madaktari.
Binafsi ninaamini hili siyo suala la madai ya "madaktari hawa" tu bali ni suala la sekta nzima na madaktari wanaokuja nyuma yao. Kwa mbali hili linaonekana kwenye madai ya madaktari "wanafunzi" ambao leo hii tunaweza kuona kutoka mbali kuwa watakuja kuongoza mgomo mwingine. Hivi Ulimboka na wenzake kwani wameanza juzi? Si walianza tangu wakiwa wanafunzi wa udaktari? Wakati kina Ulimboka wakiwa shule na walipokwarizana na watawala wakaahirisha lakini likaja kutokea tena mapema mwaka huu na sasa na kwa hakika bila kulimaliza inavyopaswa hili litatokea tena.
Uhalali wa mgomo wa madaktari hautokani na sheria
Mojawapo ya mambo ambayo yanahitaji kufikiria ni kuwa je sheria yaweza kutumika kuwakandamiza watu? Je mara zote sheria inapaswa kutiiwa hata kama inakandamiza jamii au kundi la watu? Wana filosofia na wanaharakati duniani wanatambua kuwa sheria ikiandikwa ili kukandamiza watu basi watu wana haki (inayotokana na ukuu wa dhamira zao) kutoitii sheria hiyo. Madaktari inawezekana kabisa wanagoma bila kufuata sheria lakini itakuwaje kama wamegundfua kwamba sheria iliyopo inawakandamiza? Je waitii tu? Sheria kandamizi na dhalimu haipaswi kutiiwa. Hili ni somo toka Afrika ya Kusini, India, Marekani na nchi nyingine ambapo watu wametambua kuwa watawala hutumia "sheria" kukandamiza watu.
Serikali ilipitisha sheria ambazo zimekuwa ni kandamizi kwa haki za wafanyakazi. Sheria zimejengwa ili kuwalinda watawala wasisumbuliwe na watawaliwa. NI sawasawa na kundi la ng'ombe kutengeneza sheria za kudhibiti nyangenyange wasitue migongoni mwao. Tumeliona hili hata kwenye suala la maandamano ya kisiasa ambapo sheria zimeundwa ili kuzuia maandamano ya kisiasa (japo wenyewe wanasema kwa ajili ya kulinda amani na utulivu!).
Wameshavunja sheria kwa kusimamia maslahi yao; hawawezi kuvunja zaidi!
Kama maneno ya RAis Kikwete ni ya kweli (nami naamini ni ya kweli) kwamba mgomo huu hauna uhalali kwa mtazamo wa sheria iliyopo basi madaktari tayari wameshavunja sheria. Na kuwa tayari hatua zimeshaanza kuchukuliwa dhidi yao ni uthibitisho kuwa serikali inaamini mgomo huu ni haramu. Sasa kama hili ni kweli hivyo madaktari wakiendelea kugoma wanajidhuru nini zaidi ya vile ambavyo wameshajidhuru? Tayari wako kwenye mgomo "haramu" sasa kuendelea kugoma hakuufani mgomo huo kuwa "haramu zaidi"! Kwa msingi huo kusitisha mgomo na kurudi kazini bila suluhisho la mezani kunasaliti msimamo wao wote.
Madaktari wasijifikirie wao wenyewe kwani wataogopa
Madaktari wakiamua kujifikiria wao wenyewe wataogopa; wataogopa kwa sababu kama yameweza kumtokea Ulimboka yanaweza kumtokea mtu mwingine yeyote kati yao. Je itakuwaje kama watapoteza ajira zao (na hili JK kaliashiria)? watoto wao watakula wapi? Je zile nyumba wanazoishi itakuwaje? Sasa hapa ndio kuna tofauti ya wale wenye kuamini wanachosimamia na wale wanaofuata mkumbo. Kama wanaamini wako sahihi kudai maslahi ambayo siyo tu yatanufaisha wao bali pia madaktari na wafanyakazi wengine wa sekta hiyo huko mbeleni basi msimamo kwao ni: Kuendelea na mgomo.
Serikali inaweza kumaliza mgomo ndani ya masaa 24 bila kumfukuza daktari hata mmoja
Kama nilivyosema wakati ule (Machi) nguvu ya kumaliza mgomo huu iko ndani ya serikali siyo madaktari. Serikali ndiyo inatunga sera, sheria na kupanga bajeti ya sekta hiyo. TAyari tunajua sera yao ya afya ni mbovu imaeshindwa na sheria zake zinaonekana zina matatizo na kama ni bajeti ni hafifu mno na tegemezi. Kama haya yote ni kweli basi changamoto iko kwa serikali kukaa chini na kufikiria wafanye nini kukidhi madai ya madaktari? Binafsi nina pendekezo langu lakini nitaangalia suala hili linaenda vipi.
Madaktari walisharudishwa kazini mara moja baada ya kikombe cha chai Ikulu. Safari hii hakuna cha chai wala juisi ya machungwa; Je watarudi? Baada ya tukio la Ulimboka...?
Madaktari waongozwe na kumjali mgonjwa
Jambo hili llina mitazamo tofauti; je madaktari kurudi kwenye mazingira yale yale mabovu, bajeti finyu na mfumo mbaya wa utendaji kazi ambapo wamejikuta wakishindwa kutoa huduma inayostahili kwa wagonjwa kutafanya hali hiyo ibadilike kwa vile "madaktari wamerudi kazini"? Je kurudi katika mazingira yale yale (CT Scans hakuna, vipimo hadi hospitali binafsi, vitendea kazi hakuna au duni) kutaokoa maisha ya wananchi wetu? Je, hata wakati hakuna mgomo wananchi walikuwa salama mikononi mwa madaktari ambao wamechoka, hawana vitendea kazi na ambao wako kwenye mazingira magumu?
Wengine watasema "warudi tu"; sawa lakiniw arudi wakiwa wamebadilisha nini? Hivyo, mgomo huu kufanikiwa kwake ni lazima kuwe ni kubadilika kwa namna wanavyofanya kazi. Kwa mfano, waseme kuwa wanahitaji kuwe na "minimum standard" ya utendaji kazi wa hospiali. Kwamba, hospitali ya serikali ili ifanye kazi ni lazima iwe na vitu hivi na vikiwa vinafanya kazi:
X-Rays
Single Use Gloves
CT Scan/MRI within 100 miles na kwa hospitali za rufaa ni lazima ziwe na CT Scan inayofanya kazi;
Idadi ya wauguzi na waganga wasaidizi
n.k
Serikali ikikubali kama mambo haya basi madaktari wataweza kurudi kazini hata kama maslahi yao binafsi yanaweza yasiboreshwe kwa wakati huu; lakini kutaka tu warudi ilimradi warudi ni kuhukumu wagonjwa kwenye mikono isiyoweza kuokoa maisha yao hata kama akili na nia ipo.
HIvyo basi... wanavyofikiria kuamua kurudi au kuendelea na mgomo ni muhimu waangalie picha nzima ambayo ni zaidi ya wao!