Madaktari Kenya wasambaza virusi vya Corona kutokana na uzembe na Elimu ndogo waliyonayo

joto la jiwe

JF-Expert Member
Sep 4, 2017
26,117
46,613
Waziri wa Afya wa Kenya wakati akitangaza kifo cha mgonjwa wa Corona hapo Jana Alhamisi, alisema kwamba mgonjwa huyo alifika Hospitalini hapo akiwa anaumwa maradhi mengine, hivyo alihudumiwa na madaktari na manesi wa kawaida na kulazwa katika wadi za kawaida pamoja na wagonjwa wengine hadi alipofariki na kupelekwa katika chumba cha maiti, muda wote huo alikua hajagundulika kama alikua ameambukizwa virusi vya Corona. Ndugu na jamaa wa mgonjwa waliomba kufanyike " Postmortem " ndio ikagundulika kwamba alikua na COVID-19.

Taarifa zisizorasimi zinadai kwamba, ndugu wamesema kwamba, huenda aliambukizwa virusi akiwa hapo Hospitalini kwasabu ni zaidi ya miezi miwili sasa hajawahi kutoka nje ya nyumba yake kwa sababu alikua na mgonjwa wa asiyeweza kutembea, na hapo nyumbani hakujawahi kutokea mtu yeyote mwenye dalili hadi sasa.

Ikumbukwe kwamba hiyo sio Mara ya kwanza kwa madaktari Kenya kuwachanganya wagonjwa wenye maambukizi ya Corona na wagonjwa wa kawaida. Wiki moja iliyopita huko katika hospitali ya KNH, mtoto wa miaka 13, alilazwa ICU pamoja na wagonjwa wa kawaida bila kujulikana kama alikua na virusi vya Corona, hadi alipofariki, jambo lililosababishwa chumba cha ICU kufungwa na wagonjwa kuhamishiwa kwengine.

Uzembe wa namna hii hadi kufikia kiasi kwamba madaktari hawajui dalili za Corona, huwezi kuukuta kwengine zaidi ya Kenya.
 
The bile and vitriol i see from Tanzanians here is detrimental to their well being...
i have never seen Kenyans celebrating calamities in TZ... but wait until something happens in Kenya... ghasia zinarukia kama nzi kwenye mavi

You guys will always play catch-up.. a civil war could happen in Kenya and burn everything...but we will rise above you all the time.

-ve energy destroys any man
 
The bile and vitriol i see from Tanzanians here is detrimental to their well being...
i have never seen Kenyans celebrating calamities in TZ... but wait until something happens in Kenya... ghasia zinarukia kama nzi kwenye mavi

You guys will always play catch-up.. a civil war could happen in Kenya and burn everything...but we will rise above you all the time.

-ve energy destroys any man
No one is celebrating calamities za hapo Kenya ila ni ukweli ndio mnapashwa,
Yaani mna tabia uzembe wenu ukianikwa humu jukwaani mnatumia silaha ya kuwa eti tuna celebrate calamities zenu,
Mlimtukana rais wetu mkamuita mkaidi mkasema mnatupa wiki Tz itakuwa kama Italy au tayari mmeshasahau maana kusahau mapema ni jadi yenu.
 
Hii Corona ni janga kweli kweli, halihitaji siasa wala cha utani wa jadi.Trump aliwakebehi wachina lakini leo ni zamu yake.
Hivi kumuonyesha mtu mapungufu yake ili ajirekebishe ni kusherehekea?, waalimu wako na wazazi wako walipokua wanakueleza mapungufu yako na wakati mwengine walikuchapa, je nao walikua wanasherehekea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
The bile and vitriol i see from Tanzanians here is detrimental to their well being...
i have never seen Kenyans celebrating calamities in TZ... but wait until something happens in Kenya... ghasia zinarukia kama nzi kwenye mavi

You guys will always play catch-up.. a civil war could happen in Kenya and burn everything...but we will rise above you all the time.

-ve energy destroys any man
Haha geza na joto huwa hawalali wakitafta negative news za kenya....sijawai ona jamaa wako na low self-esteem kama hao wawili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kumuonyesha mtu mapungufu yake ili ajirekebishe ni kusherehekea?, waalimu wako na wazazi wako walipokua wanakueleza mapungufu yako na wakati mwengine walikuchapa, je nao walikua wanasherehekea?

Sent using Jamii Forums mobile app
Korona siyo njaa wala ukabila hata watanzania wakemee boriti kwenye jicho la jirani.Tukivuka may ndo tutajua hatma yetu....hii energy tunaotumia kuchunguza wengine tungeitumia kujinusuru kwanza.
 
Ni wazi kabisa madaktari wa Kenya wanawaambukiza wagonjwa kutokana na Elimu duni waliyonayo
 
Msipende kuleta habari za mipasho na za hovyo ktk jambo hili serious la Corona......
Wakenya nawaaminia wako makini sn sio km sisi washangiliaji
 
Ila huwaona wakenya wenzako wakitafuta negative news za Tz 😂😂😂
Au ndio ule msemo wa nyani haoni kundule!
Ila sijaona Mkenya anayefurahia maafa ya Watanzania. Kwa Sasa najua furaha ni bila kifani lakini Kila mbwa na siku yake. Janga Kama hili hutaniona nikimuombea hata adui wangu kamwe.
Ikumbukwe Lamu Port vs Bagamoyo mlikesha humu , Geza Ulole alifungua nyuzi Kila dakika jinsi Lamu itafeli na Bagamoyo kunawiri but Sasa hivi Bagamoyo kwenye kaburi la sahau. Chungeni Sana haya maafa yasiwafikie kwa hiki kiburi chenu.
 
Ni wazi kabisa madaktari wa Kenya wanawaambukiza wagonjwa kutokana na Elimu duni waliyonayo
Elimu duni? Hivi umewahi kushihudia kashikashi za kitengo cha dharura mahosipitalini? Italy nchi ya ulimwengu wa kwanza imepoteza madaktari 101 sababi ya hili gonjwa tutegemee nini nchi za ulimwengu wa tatu? Muda utajibu.
 
Korona siyo njaa wala ukabila hata watanzania wakemee boriti kwenye jicho la jirani.Tukivuka may ndo tutajua hatma yetu....hii energy tunaotumia kuchunguza wengine tungeitumia kujinusuru kwanza.
Hatuwezi kuwa salama pekee kama kuna Jirani yako hayupo salama, lazima tumuambia Jirani mzembe ili ajirekebishe asiwe ndio chanzo cha kutuzamisha. Nchi zote zinazopakana zipo ndani ya meli moja, hamuwezi kumuachia mmoja wenu akitoboa eneo lake bila kumuambia, kwasababu wote tutazama kwa uzembe wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom