Madaktari huu ni ubinafsi, wekeni uzalendo mbele acheni maslai binafsi

gango2

JF-Expert Member
Aug 31, 2011
1,939
2,250
WanaJF
Habari zenu,



tafadhari hili jambo sio la mzaha, kweli madaktari wanamadai (kama ya msingi haya kama sio ya msingi sawa), lakini lazima tukubali kuwa mgomo sio suruhu wa matatizo jamani, watu wanakufa mahospitalini, najua kuna watu humu ndani wanashabikia sana mgomo, ukweli ni kuwa wengi wetu tulio na uwezo hata wa kubrows net tunaweza kuenda Marie stopes, mikocheni shop au hospital nyingine yoyote ya private.


Leo nimetembelea pale mwananyamala na amana hali ni mbaya jamani, watu wanakufa ambao wanaweza kupona kama watapata huduma, hebu try to imagine umempeleka mzazi wako hospital (mama au baba yako) kisha unafika pale unapewa kauli na muhudumu ‘bora afe mbona wengi wamekufa toka asubuhi’ utajisikiaje??



Tusishabikie mgomo kwa kuwa tunauwezo wa kwenda private hospital hebu fikiria Yule asiyeweza kwenda private anavyo umia. Leo humu kuna watu wanajifanya wanadiriki kushabikia mgomo kwakuwa wapo wazima na hawaumwi lakini kumbukeni kuna watu wako serious wanahitaji huduma ya haraka.


Hiki ni kipindi cha soko huria, mi nafikiri ukiona huridhiki na mshahara wa selikarini ni vizuri ukatafuta kazi private sector, kuliko kuomba kazi kisha hutaki kufanya kazi eti unagoma kudai mshahara zaidi
Madaktari msitumie umuhimu wa taaluma yenu kuwaadhibu watu wasio na hatia, hebu kuwani na moyo wa huruma. Kwani hayo mzingira bora ya kazi mnayodai si huko nyuma yalikuwa hivyo hivyo, mbona walimu wanapelekwa vijijini wanajitahidi na wale wanaoshindwa wanaacha kazi.


Najua kuna watu wao kazi yao kushabikia tuu tena ushabiki usio na maana!! Hebu katika hili tusiwe kama watoto wadogo, lamsingi warudi hospitalini kufanya kazi zao, hoja kuwa udaktari ni kazi sana kuusomea haina tija, tena ni sababu dhaifu sana kwenu, watu wengine mbona waliona bora wasomee fani nyingine ili kuondoa kadhia kama hizi kwa wagonjwa sasa nyie mliopewa nafasi msitutese bila sababu ya msingi>
 
Comrade Gango2, hii mada yako mbona ni kama kachumbali?!, umechanganya issues mno: hivi Amana na Mwanyamala nao wako kwenye Mgomo?!, hivi kweli umepata nafasi ya kupitia madai ya madaktari vizuri?!, mbona madai ya nyongeza ya mshahara ni moja kati ya madai mengi ya kuboresha mazingira ya kazi hasa uwepo wa vifaa bora?!, pitia vizuri orodha ya madai yao kabla hujawa one sided kwenye maamuzi.
 
Comrade Gango2, hii mada yako mbona ni kama kachumbali?!, umechanganya issues mno: hivi Amana na Mwanyamala nao wako kwenye Mgomo?!, hivi kweli umepata nafasi ya kupitia madai ya madaktari vizuri?!, mbona madai ya nyongeza ya mshahara ni moja kati ya madai mengi ya kuboresha mazingira ya kazi hasa uwepo wa vifaa bora?!, pitia vizuri orodha ya madai yao kabla hujawa one sided kwenye maamuzi.

tafadhari, inawezekana hujafika hapo bali nenda kaone wewe pale, ndio hawa watu wanamadai lakini kwanini wagome ile hali kazi zao zinahusiana na kuokoa maisha ya mwanadamu?. wanamkomoa nani? serikali au mwananchi? nani hajui maisha mabovu anayoishi mwalimu wa leo? mbona wao hawagomi? KUMBUKA UHAI HAUJI MARA MBILI KAKA!!

Hamna kitu muhimu na chenye dhamani kama uhai wa mwanadamu, sasa kwanini wewe usababishe upotee??? je niwangapi wanaomtegemea nyuma??
 
Kaka mimi ni daktarri nimefanya kazi vijijini many years na degree yangu, nimetibu kina mama usiku na mchana bila kuchoka nugu yangu, nimepikia wagonjwa wanaotoka maili nyingi chakula na kuwapa nauli, nimechangia wagonjwa damu many times...

Mimi ni mzalendo tena sana, mazingira magumu sasa basi yametosha,,, hivi unajua watu wanakufa vijijini kwa kuwa hakuna mipira ya kulishia puani ambao moja haufikii sh 5000?

Tuna serikali kweli sisi?tunaendesha upuuzi wa sabasaba na nane na week ya utumishi wa umma....ila watu wanakufa kwa hili dogo....UZALENDO!!!!

Kama wewe mzalendo sana kasomee udaktari hujachelewa Am sure then utajua kwa nini tunagoma, na tutaendelea kugoma ndugu yangu....migari ya serikali kila siku mipya,,,,,,dawa hawaleti vifaa hawaleti.....wazalendo sana na wao wakosomee udaktari, walimu they do not want to dare...WE CAN DARE ...
 
Kaka mimi ni daktarri nimefanya kazi vijijini many years na degree yangu, nimetibu kina mama usiku na mchana bila kuchoka nugu yangu, nimepikia wagonjwa wanaotoka maili nyingi chakula na kuwapa nauli, nimechangia wagonjwa damu many times...

Mimi ni mzalendo tena sana, mazingira magumu sasa basi yametosha,,, hivi unajua watu wanakufa vijijini kwa kuwa hakuna mipira ya kulishia puani ambao moja haufikii sh 5000?

Tuna serikali kweli sisi?tunaendesha upuuzi wa sabasaba na nane na week ya utumishi wa umma....ila watu wanakufa kwa hili dogo....UZALENDO!!!!

Kama wewe mzalendo sana kasomee udaktari hujachelewa Am sure then utajua kwa nini tunagoma, na tutaendelea kugoma ndugu yangu....migari ya serikali kila siku mipya,,,,,,dawa hawaleti vifaa hawaleti.....wazalendo sana na wao wakosomee udaktari, walimu they do not want to dare...WE CAN DARE ...

Ndugu yangu huo ndio uhalisia wa mazingira yetu, tena sio tu Tanzania bali almost Africa nzima, na sio kwamba leo au kesho yatatatuliwa, HIVI KAMA MAZINGIRA HAYO YAMEKUSHINDA KWANINI USITAFUTE PRIVATE hospital uende huko, sio kwamba watu wameshindwa kusomea udaktari ili nadhani walifikiri mwanzo kuondoa kadhia hizo za kugoma bora waende sekta nyingine na natumai kama wewe usingesomea udaktari ungetoa chansi kwa mtu mwengine asomee.
 
Hiki ni kipindi cha soko huria, mi nafikiri ukiona huridhiki na mshahara wa selikarini ni vizuri ukatafuta kazi private sector, kuliko kuomba kazi kisha hutaki kufanya kazi eti unagoma kudai mshahara zaidi
Madaktari msitumie umuhimu wa taaluma yenu kuwaadhibu watu wasio na hatia, hebu kuwani na moyo wa huruma. Kwani hayo mzingira bora ya kazi mnayodai si huko nyuma yalikuwa hivyo hivyo, mbona walimu wanapelekwa vijijini wanajitahidi na wale wanaoshindwa wanaacha kazi.
 
salaam ndugu wapendwa!
ni kweli inauma na kusikitisha unapofika na mgonjwa kisha madaktari wanakuangalia
kama vile umekwenda kuuza sura. mgonjwa analia huna lakufanya. huruma imewatoka, mafunzo wameyasahau ubinadamu hawana tena. wamesahau muda wote wapo masomoni ni fedha za watanzania hawahawa wagonjwa wakiwemo wakilipa kodi ziwasomeshe wao na leo wanaendelea kulipa kodi walipwe mishahara na dawa zinunuliwe.
watoto hawa ambao leo ni watuwazima wengi wao wametoka vijijini. wamesahau maisha waloishi mwanzo wamejitenga na jamii na kujiona wao ni daraja la juu kuliko wafanyakazi wote nchini. wanatuangalia tukifa wazazi wao, walimu wao tulowafundisha leo hii wakawa madaktari, marafiki zao tuliosoma nao toka msingi,sekondari na vyuo, tukawasupport
kwa hali na mali. wapi bwana hawasikii la kuu wala la mjukuu. wao na maslahi wao na maisha ya juu.

hapana tuwakumbushe hawa madaktari wakumbuke haya.
watuhudumie, tunateseka ndugu zao,watanzania wenzao sisi,
sie sio wakimbizi kwanini wanatutesa tumekosa nini? kwanini wasiache kazi kama mshahara mdogo?
 
Kaka mimi ni daktarri nimefanya kazi vijijini many years na degree yangu, nimetibu kina mama usiku na mchana bila kuchoka nugu yangu, nimepikia wagonjwa wanaotoka maili nyingi chakula na kuwapa nauli, nimechangia wagonjwa damu many times...

Mimi ni mzalendo tena sana, mazingira magumu sasa basi yametosha,,, hivi unajua watu wanakufa vijijini kwa kuwa hakuna mipira ya kulishia puani ambao moja haufikii sh 5000?

Tuna serikali kweli sisi?tunaendesha upuuzi wa sabasaba na nane na week ya utumishi wa umma....ila watu wanakufa kwa hili dogo....UZALENDO!!!!

Kama wewe mzalendo sana kasomee udaktari hujachelewa Am sure then utajua kwa nini tunagoma, na tutaendelea kugoma ndugu yangu....migari ya serikali kila siku mipya,,,,,,dawa hawaleti vifaa hawaleti.....wazalendo sana na wao wakosomee udaktari, walimu they do not want to dare...WE CAN DARE ...

Wewe sio daktari, usingezungumza hivyo bila kuwaonea huruma wagonjwa maana hivyo unavyoongea ni kinyume hata ya kiapo cha udaktari. Usitangulize vifaa mbele sema kwa uhakika mishahara ndio kipaumbele chenu msihadae watanzania na vifaa ili tuwaunge mkono. Ungechukua kwa hesabu wagonjwa wanaokufa mkiwa kazini na sasa mkiwa katika mgomo utapata picha gani??? Hivi kwa usomi wako sasa hivi mnamwadhibu nani, Serikali au mgonjwa?????????? Acheni kilio cha mamba bwana!!!!!!!!!!!!!!! kuweni wakweli na muwe na huruma na wananchi wanyonge wa nchi hii. Hii laana ya vifo vya watu wasio na hatia haitawaacha salama nyie na familia zenu. Narudia msitumie uongo na mgongo wa vifaa kudai mishahara mikubwa kwa gharama ya damu za watanzania zinazomwagika bila kuwa na hatia. Eleweni kodi za hawa mnaowaache wafe sasa ndio zimewasomesha hadi kuwa madaktari, wengine kama sio hizo kodi leo mngekuwa waganga wa kienyeji. Muwe na huruma.
 
Acha wagome na bado walimu (km wanaweza lkn), serikali gani isiyojua vipaumbele vya maendeleo, vipaumbele vya serikali hii ni safari zisizo na tija za jk na msururu wa watu, kusheherekea miaka 50 kwa mabilion, kuongeza mikoa na wilaya ili kuwapa maswahiba ulaji. Serikali yetu imekuwa tajiri kwa kauli na sera zisizotekelezeka, mara kilimo kwanza, mkukuta, vision 2025, what a nonsense!
 
WanaJF
Habari zenu, CCM hoiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii



tafadhari hili jambo sio la mzaha, kweli madaktari wanamadai (kama ya msingi haya kama sio ya msingi sawa), lakini lazima tukubali kuwa mgomo sio suruhu wa matatizo jamani, watu wanakufa mahospitalini, najua kuna watu humu ndani wanashabikia sana mgomo, ukweli ni kuwa wengi wetu tulio na uwezo hata wa kubrows net tunaweza kuenda Marie stopes, mikocheni shop au hospital nyingine yoyote ya private.


Leo nimetembelea pale mwananyamala na amana hali ni mbaya jamani, watu wanakufa ambao wanaweza kupona kama watapata huduma, hebu try to imagine umempeleka mzazi wako hospital (mama au baba yako) kisha unafika pale unapewa kauli na muhudumu ‘bora afe mbona wengi wamekufa toka asubuhi' utajisikiaje??



Tusishabikie mgomo kwa kuwa tunauwezo wa kwenda private hospital hebu fikiria Yule asiyeweza kwenda private anavyo umia. Leo humu kuna watu wanajifanya wanadiriki kushabikia mgomo kwakuwa wapo wazima na hawaumwi lakini kumbukeni kuna watu wako serious wanahitaji huduma ya haraka.


Hiki ni kipindi cha soko huria, mi nafikiri ukiona huridhiki na mshahara wa selikarini ni vizuri ukatafuta kazi private sector, kuliko kuomba kazi kisha hutaki kufanya kazi eti unagoma kudai mshahara zaidi
Madaktari msitumie umuhimu wa taaluma yenu kuwaadhibu watu wasio na hatia, hebu kuwani na moyo wa huruma. Kwani hayo mzingira bora ya kazi mnayodai si huko nyuma yalikuwa hivyo hivyo, mbona walimu wanapelekwa vijijini wanajitahidi na wale wanaoshindwa wanaacha kazi.


Najua kuna watu wao kazi yao kushabikia tuu tena ushabiki usio na maana!! Hebu katika hili tusiwe kama watoto wadogo, lamsingi warudi hospitalini kufanya kazi zao, hoja kuwa udaktari ni kazi sana kuusomea haina tija, tena ni sababu dhaifu sana kwenu, watu wengine mbona waliona bora wasomee fani nyingine ili kuondoa kadhia kama hizi kwa wagonjwa sasa nyie mliopewa nafasi msitutese bila sababu ya msingi>
:bolt:
 
WanaJF
Habari zenu,





tafadhari hili jambo sio la mzaha, kweli madaktari wanamadai (kama ya msingi haya kama sio ya msingi sawa), lakini lazima tukubali kuwa mgomo sio suruhu wa matatizo jamani, watu wanakufa mahospitalini, najua kuna watu humu ndani wanashabikia sana mgomo, ukweli ni kuwa wengi wetu tulio na uwezo hata wa kubrows net tunaweza kuenda Marie stopes, mikocheni shop au hospital nyingine yoyote ya private.


Leo nimetembelea pale mwananyamala na amana hali ni mbaya jamani, watu wanakufa ambao wanaweza kupona kama watapata huduma, hebu try to imagine umempeleka mzazi wako hospital (mama au baba yako) kisha unafika pale unapewa kauli na muhudumu ‘bora afe mbona wengi wamekufa toka asubuhi' utajisikiaje??



Tusishabikie mgomo kwa kuwa tunauwezo wa kwenda private hospital hebu fikiria Yule asiyeweza kwenda private anavyo umia. Leo humu kuna watu wanajifanya wanadiriki kushabikia mgomo kwakuwa wapo wazima na hawaumwi lakini kumbukeni kuna watu wako serious wanahitaji huduma ya haraka.


Hiki ni kipindi cha soko huria, mi nafikiri ukiona huridhiki na mshahara wa selikarini ni vizuri ukatafuta kazi private sector, kuliko kuomba kazi kisha hutaki kufanya kazi eti unagoma kudai mshahara zaidi
Madaktari msitumie umuhimu wa taaluma yenu kuwaadhibu watu wasio na hatia, hebu kuwani na moyo wa huruma. Kwani hayo mzingira bora ya kazi mnayodai si huko nyuma yalikuwa hivyo hivyo, mbona walimu wanapelekwa vijijini wanajitahidi na wale wanaoshindwa wanaacha kazi.


Najua kuna watu wao kazi yao kushabikia tuu tena ushabiki usio na maana!! Hebu katika hili tusiwe kama watoto wadogo, lamsingi warudi hospitalini kufanya kazi zao, hoja kuwa udaktari ni kazi sana kuusomea haina tija, tena ni sababu dhaifu sana kwenu, watu wengine mbona waliona bora wasomee fani nyingine ili kuondoa kadhia kama hizi kwa wagonjwa sasa nyie mliopewa nafasi msitutese bila sababu ya msingi>

We hujui unachoongea, Huko nyuma kwani watu walikuwa hawafi!!, umeuliza kwanini walikuwa wanakufa na madaktari wapo!!.
 
Acha wagome na bado walimu (km wanaweza lkn), serikali gani isiyojua vipaumbele vya maendeleo, vipaumbele vya serikali hii ni safari zisizo na tija za jk na msururu wa watu, kusheherekea miaka 50 kwa mabilion, kuongeza mikoa na wilaya ili kuwapa maswahiba ulaji. Serikali yetu imekuwa tajiri kwa kauli na sera zisizotekelezeka, mara kilimo kwanza, mkukuta, vision 2025, what a nonsense!

tell them"LIWALO NA LIWE"
 
A doctor can go on holiday not on strike!


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kuna nguvu kubwa sana naona inaanza kutumika hasa kuanzia jana mchana ya kutaka kugeuza hili swala la madaktari ili lionekane ni mishahara tu. Kwa makusudi kuna watu hawataki kuongelea hoja 'kamili' kama madaktari walivyokubaliana na waziri mkuu.

Kwa nini watu hawaongelei wagonjwa kulala chini? kwanini watu hawataki kuongea kuhusu ukosefu wa dawa muhimu, hivi kama hakuna x-machine daktari atamtibu mgonjwa kwa kupiga ramli? Kama doctor hana dawa atamtibu mgonjwa kwa kuimba? Au wagonjwa watapona kwa kuona watu walivaa makoti meupe tu? Kwa nini hatutaki kuongea issue nzima?
 
madaktari naona swala la vifaa hio ni zuga tu. Kama kweli mngekua ni vifaa ndo vyawagusa sana basi mlipoongezewa posho za ON CALL na EXTRER SHIFT Pamoja na hio ya "posmotum" si mngeikataa kwanza na kuishauri serekali iwanunulie vifaa kwanza? Jamani mimi siijui sekta iliokamilika vifaa hapa nchini. kwa nn hawa jamaa wanatugeuza wagonjwa ndio ngao ya kukinga mishale kwenye vita yao na serekali? Mm siungi mkono hata kidogo kwani tatizo la upungufu wa vifaa lipo sehem zote; ukienda Polisi utaambiwa kanunue karatasi au jaza mafuta tumfuate mhalifu wako. Shule ndo usiseme, tunanua vitabu, daftari, kalam hata chaki twachangishwa kununua. Madaktari semeni tu mmetuchoka. Kwani kila kukicha mnabadilika. Mlianzia na mgogoro wa ma dk wanafunzi, ikabadilika mkauvaa mgomo nyie. Mkamtosa Pinda kwenye usuluhishi, mkakomaa waziri atimuliwe na wasaidizi wake (wakatimuliwa) mkaenda ikulu mkarudi. Hatujakaa sawa mmegoma tena. Yaani sijui hata agenda yenu ni ipi. Kama leo sh 1,500,000/= haiwatoshi basi hata kama mtapewa hizo ml 3.5 kamwe hazitokidhi tamaa zenu. Wacha sisi tufe ili nyie mtimiziwe mradi wenu. Inaniuma sana
 
jana kwenye taarifa ya habari ITV wameonyesha ajali ya pikipiki ilibeba mshkaki, mmoja wa majeruhi amepondeka vibaya mguu na anatoka damu kichwani, alipelekwa hospitali ya Bombo, madaktari hawajamtibu maana hakuna mashine ya XRAYS.

Na mkuu wa kitengocha xray amesema wazi kuwa hospitali haina mashine ya xray.... Na inapotokea matatizo kama hayo hushauri kuoeleka wagonjwa kupiga xray kwenye hospitali zenye huduma hiyo...

Sasa unategemea hali ya majeruhi huyu iweje? Kama xray hawana vipimo vingine itakuwaje??? Ataishia kupata huduma ya kwanza then what next?

Ingawa mgomo huu unaumizq na kusikitisha, ila kuna joja za msingi nyuma yake....
 
tafadhari, inawezekana hujafika hapo bali nenda kaone wewe pale, ndio hawa watu wanamadai lakini kwanini wagome ile hali kazi zao zinahusiana na kuokoa maisha ya mwanadamu?. wanamkomoa nani? serikali au mwananchi? nani hajui maisha mabovu anayoishi mwalimu wa leo? mbona wao hawagomi? KUMBUKA UHAI HAUJI MARA MBILI KAKA!! Hamna kitu muhimu na chenye dhamani kama uhai wa mwanadamu, sasa kwanini wewe usababishe upotee??? je niwangapi wanaomtegemea nyuma??
wewe kama muhanga wa mgomo umefanya/umeisisitiza vipi serikali iboreshe huduma za afya na iwajali madaktari? DAKTARI ANAKUTUMIKIA NAWEWE MSAIDIE SI KULALAMIKA TU
 
Acheni wagome. Mandela asingeikubali jela A.Kusini isingejipatia uhuru. Sisi wenyewe tukienda mahospitalini
huwa tunaziba pua. Lakini madkt ndimo wanamoshindia. Sisi tuko kwenye viyoyozi wa wamo matanuruni.
Tunataka huduma za afya ziboreshwe. Kama serikali haitafanya kwa hiyari basi njia mbadala zitatumika.
Lakini hekima ya kujishusha kwa serikali ndiko kunakotakiwa.

Mwenyeji ndiye akuambie matatizo yake na si wewe kujiamulia juu ya matatizo yake. Kama kweli tunataka
kusonga mbele kimaendeleo.

Angalia pesa zilizotengwa kwa ajili ya madkt toka nje. Je hazitoshi kununulia mtambo wa kusindika unga
wa mahindi na kuuuza huko sudani na kwingineko kwenye njaa Afrika?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom